DC Hapi aagiza baa maarufu Jijini Dar, Corner bar ifungwe!

DC Hapi aagiza baa maarufu Jijini Dar, Corner bar ifungwe!

Lissu kuna hela huku corner bar. Zungukia utengrneze mazingira.


Huyo hatumikii fedha anatumia na kuitetea taaluma yake ili ibaki kwenye heshima na madhumuni yake
 
Leseni waliyopewa ni ya biashara gani. Mwenye biashara akipata wakili mzuri anaweza lipwa fidia ya mamilioni. Shida yetu wafanyabiashara wengi wanafanya shughuli zao kimagumashi ama chini ya mwamvuli wa vyama vya siasa.
 
Dah halafu tukapone wapi ?

Mbona akili za hawa viongozi wetu ni kama mbayuwayu ?

Ukifunga Bar maana yake ni umezuia umalaya ? Hiyo ni profession kongwe duniani pengine kuliko zote
 
Kama inachochea biashara haram ya ngono naifungwe tu hakuna namna.
 
Kuifunga ni kuwaonea wamiliki.....dc aeleewe ya kuwa sehemu ya starehe kama hzo ni kawaida wauza nyuchi kwenda...
Hata masai,maisha club na sehemu zingine kuwakuta jajajaja ni jambo la kawaida...
Hata jolly club ambayo sahv ni isumba Lazima utawakuta makahaba...maana na wao wanakwenda kama wateja
Hata sehemu za masaki hoteli wanazofikia watalii lazima makahaba utawakuta....
Wangeangaliaa au kukaa chini na mmiliki waone wanafanyaje......kilimo kuifungia biashara ya mtu

Ova
 
Pale kuna bar zaidi ya moja na aita saidia cos biashara inafanyika mtaani maeneo ya pale ile inatumika tuuh kujifichia utokeapo msako ata hivyoo wanaweza ji hifadhi bar za kando yake nadhani watawaonea tuuh wamiriki kwanza sasaiv wanavaa vizuri uwez wagundua kwa haraka
 
Kuna vitu vingine ni ngumu kuvizuia.

Hao wanaojiuza wapo kote Duniani nyinyi mnaamini mtaweza kuzuia?

Dar es Salaam. Baada ya malalamiko kuzidi kutokana na kuwapo biashara zisizo rasmi katika baa maarufu ya Corner, sasa baa hiyo imeamriwa kufungwa.

Akiwa katika ziara ya kawaida leo (Jumamosi) mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amemuagiza Ofisa Biashara wa Kinondoni, Mohamed Nyasama kuifunga baa hiyo.“Hatuwezi kuvumilia vitendo hivivikaendelea kufanyika huku tukiwa kimya...

natoa agizo kesho nendeni kaifungieni hiyo baa kwa kuwa inakiuka maadili,”amesema Hapi.

Hata hivyo Nyasama amesema walishaitoza baa hiyo faini ya Sh 300,000 kwa kosa hilo.“ Mkuu hii baa ni sugu, nimeahawahi hata kuipiga faini na bado imeendelea na utaratibu huo huo wa kuruhusu kina dada kujiuza.


Kwa amri yako mkuu naanza taratibu za kuifungia leo, hadi kufikia keshoitakuwa tayari,” amesema.

Chanzo : Mwananchi Online
 
Back
Top Bottom