Kuna tatizo kubwa sana Dawasco Kimara, tangu mwezi wa tatu hawajaleta bili, tumefuatilia tukaambiwa mita imebadilishwa na hakuna kumbukumbu lini wamebadilisha, na tangu waibadilishe hawajaisoma na hawana hata ratiba ya kuisoma. Nimepiga picha mita wakadai inasoma unit zaidi ya 150 ambazo gharama yake ni zaidi ya 240000, lakini cha ajabu ni kuwa hawana kumbukumbu lini wamebadili hiyo mita, na mpaka mara ya mwisho walikuwa wakitoa bili kwenye akaunt kwa kuunganisha kwenye uniti za mita ya zamani, na hata juzi baada ya kuwafuata ofisini walitoa bili ya kukadiria kwa kutumia namba ya zamani wakati mita imeshabadilishwa.
Mita imebadilishwa bila hata taarifa kwa wahusika, hivi kama mita imetolewa kwingine ikiwa na unit nikawekewa mimi kwa visa au fundi kahongwa huko aihamishie kwangu nitaelewaje? wasiwasi mwingine mkubwa ni kulipishwa mara mbili kwa kwa sababu inaonekana mita imefungwa zamani na wakaendelea kutoa bili kwa kukadiria kwa mita ya zamani.
Na inaonyesha kama kwamba hawana uelewa na usomaji wa hizo mita mpya. Utakuta unit 9.5 wanakwambia 95! Hivi waweza kutumia unit 95 za maji ndani ya mwezi mmoja na maji yanatoka mara mbili tu kwa wiki kwa familia moja?
Imafika kipindi tunaamini kuwa wanalazimisha kutengeneza mazingira ya kukatia watu maji ili magari yao ya mitaani waweze kuuza maji.
Mita imebadilishwa bila hata taarifa kwa wahusika, hivi kama mita imetolewa kwingine ikiwa na unit nikawekewa mimi kwa visa au fundi kahongwa huko aihamishie kwangu nitaelewaje? wasiwasi mwingine mkubwa ni kulipishwa mara mbili kwa kwa sababu inaonekana mita imefungwa zamani na wakaendelea kutoa bili kwa kukadiria kwa mita ya zamani.
Na inaonyesha kama kwamba hawana uelewa na usomaji wa hizo mita mpya. Utakuta unit 9.5 wanakwambia 95! Hivi waweza kutumia unit 95 za maji ndani ya mwezi mmoja na maji yanatoka mara mbili tu kwa wiki kwa familia moja?
Imafika kipindi tunaamini kuwa wanalazimisha kutengeneza mazingira ya kukatia watu maji ili magari yao ya mitaani waweze kuuza maji.