Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

Nguruvi3 Hii hoja ajabu ya mwaka kwanza Mzee Mwanakijiji anaipindisha ama pia hataki kuijibu. Swali la Lissu ambalo halijajibiwa na huyo "mtoa darsa" wao na hata na Mzee mwanakijiji mwenyewe ni kwamba kuna sababu gani ya msingi mhimili kama Mahakama kuwa na kiongozi anayekaimu nafasi yake kwa miezi mitano sasa?

Yeye Mwanakijiji anawashutumu wenzake kuwa na dhana (assumption) dhaifu na mbaya dhidi ya jambo hili, lakini na yeye pia ana dhana kwamba hakuna tatizo wakati kiuhalisia tatizo lipo. Kinadharia ni kama vile mhimili wa utawala umeutunishia misuli mhimili wa mahakama kwamba hatuteui Jaji Mkuu na nyie hamna la kutufanya.

Mosi nakubaliana na hoja ya Mwanakijiji kwamba hakuna sheria iliyovunjwa, lakini kwa tukio hili lazima tugutushwe kwamba kama hakuna sheria ilivyovunjwa, basi tuweke sheria ambayo mbele ya safari itazuia jambo hili kutokea. Njia anayotaka Mwanakijiji itumike si sahihi!

Bunge hili lililojaa wabunge wa CCM haiwezekani kupeleka hoja inayopingana na mtazamo na utashi wa Rais ikakubalika ama ikapitishwa. Tumeona ni kwa jinsi gani wabunge hao wanapoungana dhidi ya hoja yoyote ile inayopingwa na Serikali. Jibu ni rahisi, wabunge wanaujua ukuu wa chama (Party Supremacy) kwenye nafasi zao walizonazo za ubunge!

Suluhisho la haya yote ni marekebisho ya Katiba ambayo yatakifutilia mbali kifungu kinachovipa vyama vya siasa mamlaka ya kuuvua ubunge wa Mbunge kwa kumvua uanachama wake. Wabunge wa CCM wakiwa hawana hofu ya kufukuzwa chama na kupoteza ubunge wao, ndiyo wanaweza kufanya hayo marekebisho anayoyapendekeza Mwanakijiji!
 
Tundu Lisu haeleweki kwa sababu ni retarded!
Dah usidhani Tundu Lissu ni GSM wanaokulisha wewe,mkeo na familia yako you are the retarded unatumika kaa tambala bovu na yeyote anayedhani anataka kutupia kwenye hilo shimo lako na kila mtu anayetaka kujifunza kutumia kwa waliobinuka no wonder you dont have marinda
 
Msimamo wangu ni huu na haujabadilika.

..Lowassa ni fisadi ( Richmond).

..Dikteta uchwara ni fisadi ( kuuza nyumba za serikali na kununua meli mkweche).

..Chenge ni fisadi ( ununuzi wa rada).

..
Sasa unapingana na chama chako kuhusu ufisadi wa Lowassa
 
Mawazo ya hovyo hovyo ambayo badala ya kujikita kwenye hoja, hukimbilia kwenye viroja!!!

"...mlivyomkaribisha...!" Hao waliomkaribisha ambao mimi ni mmoja wao ni akina nani?!
Hapo tunaizungumzia chadema na ukawa. Wewe ni ccm?
 
Hapo tunaizungumzia chadema na ukawa. Wewe ni ccm?
Ninachokiona kwenye mada hii ni darasa la Profesa Kabudi in relation to nafasi ya Kaimu Jaji Mkuu!! I am so surprised kusikia kumbe kilichopo hapa ni CHADEMA na CCM!!!!

Kwenye mfano wangu nimemwelezea Kitila Mkumbo... ni CCM au CHADEMA yule?!
 
Nimesikiliza kwa makini kile kinachoitwa "darasa" la Prof. Kabudi jana Bungeni kuhusiana na suala la Kaimu Jaji Mkuu na hasa hoja nzima ya kukaimiwa kwa nafasi ya Jaji Mkuu. Inasikitisha kwanza kwamba kuna watu wanasifia kuwa ametoa "darasa" na kwamba watu walikuwa wanamsikiliza kama wanafunzi katika Shule ya Msingi Mtakuja!

Je, ni kweli kile alichokisema watu walikuwa hawakijui? Ni kweli wabunge na wanasheria walioko Bungeni walikuwa hawajui yale yaliyokuwa yanasemwa?

Kuna hoja ya kuuliza swali; kwamba - kwanini Rais amemteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu kwa muda wote huu. Swali ambalo halipaswi kuulizwa na tulilikataa wakati ule ni kuhusu mamlaka ya Rais kumteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu. Hili liko ndani ya mamlaka ya Rais (Presidential prerogative). Lakini pia swali hili kwa ukubwa wake halipaswi kuulizwa isipokuwa kisiasa (political question) ili watu kupata hoja za kisiasa au ujiko wa kisiasa. Kwamba, mtu anataka kuonesha kuwa Magufuli amekosa mtu wa kuwa jaji mkuu, au kwamba Magufuli ana tatizo na mahakama n.k. Hili si jambo sahihi; wabunge kama wanaona Rais anatumia muda mrefu kujaza nafasi ya jaji mkuu wana uwezo wa kubadilisha sharia na hata Katiba chini ya Ibara ya 100 ya Katiba yetu.

Kama wanataka nafasi ya Jaji Mkuu isikaimiwe indefinitely (kama hoja ya Lissu ilivyoashiria) namna pekee ni kubadilisha Katiba au sheria ili kuweka kikomo kama ilivyo katika baadhi ya nafasi za utumishi wa umma ambapo sheria inasema mtu atakaimu nafasi kwa muda fulani na baada ya hapo basi mtu wa kudumu ateuliwe au aliyekaimu athibitishwe. Wao wabunge (watunga sheria na wanaoweza kufanya mabadiliko ya Katiba) wanaweza kuweka kikomo labda kwa ajili ya mustakabali)

Kama kwa mfano Rais angejaza cheo cha Ujaji siku moja tu baada ya Jaji Othman kustaafu wapo ambao labda wangeweza kuja na hoja ya kwanini amejaza nafasi haraka bila kuonesha tafakari sana au klutumia muda kufanya utafiti wa kutosha! Lakini pia kuna swali ambalo inabidi liulizwe kwa wale wanaolalamikia - kwa Rais kuweka Kaimu Jaji Mkuu ni shughuli gani ya Mahakama Kuu ambayo haiwezi kufanyika sasa hivi kwa vile kuna kaimu Jaji Mkuu au ni kitu gani hakifanyiki katika mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ambacho kinapaswa kufanywa na jaji mkuu peke yake. Hili ndilo linaweza kuwa hoja ya kwanini inahitajika Jaji Mkuu na siyo Kaimu Jaji Mkuu?

Lakini kung'ang'ania kitu ambacho wote wanajua hakipo - kwamba Rais hajavunja sheria wala Katiba, na kuwa hakuna kikomo cha muda kilichowekwa kwa hoja ya kuwa ni mazoea mapya haitoshi kuwa hoja.

Lakini wapo ambao wanasema kuwa kwa kutomthibitisha Kaimu Jaji basi Kaimu Jaji anaweza asifanye anayotakiwa kufanya kwa kuhofia kuiudhi mamlaka ya uteuzi. hilo si wazo sahihi katika utawala. Unapokaimu nafasi unakuwa na madara yote ambayo unayo kwa mujibu wa kukaimu kwako. Hakuna hoja ya kumridhisha mtu au la. Makamu wa Rais anapokaimu nafasi ya Urais wakati Rais hayupo kwa mujibu wa sharia ana madara yote ambayo ameruhusiwa kuwa nayo kwa mujibu wa Katiba. Na hili ni kweli kwa mtu mwingine yeyote ambaye Rais anaweza kumpa nafasi ya kukaimu jambo lolote kwa niaba yake. Mtu yeyote professional hajali sana kama atamfurahisha mtu au la atafanya kwa mujibu wa madaraka aliyopewa. Mtu ambaye atajali kuwa akifanya jambo Fulani atamuudhi aliyemteua au chombo cha juu hafasi kushika nafasi hiyo.

Somo ambalo Kabudi angepaswa kulitoa na labda wengi wanalihitaji kulielewa ni hili la Presidential prerogatives..
Amekaa nao miaka kibao darasani anawafundisha hawakuelewa hawawezi kumuelewa kwa nusu saa, wanafunzi wake hao wakina TL ni Vi..laza tu!Anapoteza muda wake
 
Ninachokiona kwenye mada hii ni darasa la Profesa Kabudi in relation to nafasi ya Kaimu Jaji Mkuu!! I am so surprised kusikia kumbe kilichopo hapa ni CHADEMA na CCM!!!!

Kwenye mfano wangu nimemwelezea Kitila Mkumbo... ni CCM au CHADEMA yule?!
Kitila Mkumbo is an outlier in this context
 
Kitila Mkumbo is an outlier in this context
Na wewe unadhani upo within a context perimeter?

Soma mada kuu, soma posts zangu kwa kituo then judge yourself if you believe you're within a proposed perimeter based on my posts and your argument!
 
Siku JPM alipomteua Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu; watu tulimtarajia angeikana nafasi hiyo kwa sababu ilikuwa inapunguza nguvu kazi ya watoa taaluma lakini kinyume chake, Mkumbo nae alifurahia kweli kweli uteuzi huo!!!
Mkuu,hapo ndipo unapojua nguvu ya tumbo kuliko akili,huyo nae ni profesa wala usingedhani angekubali huo uteuzi.
 
Sijasikiliza hayo ya bungeni na sidhani kama bado nina interest ya siasa za bunge hivi sasa ambazo kwangu naona ni kama zimekosa mvuto!!

Tuje kwenye hiyo hja ya kwamba, kukaimu kwa muda mrefu hakuwezi kumfanya Kaimu Jaji kushindwa kufanya kazi zake sawa sawa!!!

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Rais hana mamlaka ya kumtumbua Jaji wa Mahakama Kuu kirahisi rahisi tu!

Inapotokea sababu ambazo rais anaona Jaji huyu hafai tena kuwa jaji, hata kama ni suala la ukosefu wa maadili, bado Rais anatakiwa kwanza kuunda Tume ambayo itakuwa na Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume, na miongoni mwao angalau nusu wanatakiwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu kutoka nchi za Jumuiya ya Madola!

Tume hii itachunguza tuhuma dhidi ya Jaji kuona kama ni kweli au hapana!

NOTE: Nitapitia katiba ili nione kifungu hicho kinasemaje kwa yakini!!

Kutokana na kifungu hicho cha Katiba, Jaji Mkuu na in fact, Jaji yeyote wa Mahakama Kuu hawezi kuwa na hofu ya kutekeleza wajibu wake kwa kuhofia mamlaka ya uteuzi kwa sababu, anafahamu, hawezi kuondolewa hovyo hovyo au hata kwa makosa ya kubambikiwa!!!

Kaimu Jaji Mkuu kwa nafasi yake hiyo sio Jaji wa kawaida na wala sio Jaji Mkuu ambao wanaweza kulindwa na kifungu hicho hapo juu! Kwahiyo, Rais anaweza kumtoa muda wowote bila maswali kwa sababu, atakachomvua sio Ujaji wala Ujaji Mkuu bali Ukaimu Jaji Mkuu ambao sidhani kama Katiba inatoa ulinzi niliotaja hapo juu!!!

Hoja ndiyo hiyo hapo juuu!!

Na kwa staili hiyo, unaweza kuteua Kaimu Jaji Mkuu kama ilivyo sasa; na ukiona anazingua unamtoa unamweka mwingine nae anakuwa Kaimu Jaji Mkuu!! Sasa hofu isije kwamba, kwa kuhofia kutokuwa na ulinzi wa katiba, basi huenda wengine wanaweza kufanya mambo kwa kuyaridhisha mamlaka ya uteuzi!!

Isitoshe, huyu Kaimu Jaji Mkuu kila wakati atakuwa anaota kuwa Jaji Mkuu na sio kaimu tena!! Kwa namna ya kawaida kabisa; lazima ndoto zake zitaenda sambamba na kuhakikisha hazikeri mamlaka ya uteuzi!!
umesomeka mkuu in summary ni kuwa jaji akishateuliwa analindwa kikatiba.

pia jaji mkuu akisha kuteuliwa analindwa kikatiba isipokuwa kaimu jaji hana utaratibu maalumu unaomweka pale kisheria,

aksante kwa ufafanuzi mzuri prof. Kabudi akipitia hapa atapata shule ya kutosha.

nasikia huyo bwana anajiona yeye ndo anajua kuliko wanasheria wote ingawa alifeli bar exams
 
Babu unazeeka vibaya ... sikuhizi huna hoja zaidi ya kufagilia waumini wenzio ...
Nimesikiliza kwa makini kile kinachoitwa "darasa" la Prof. Kabudi jana Bungeni kuhusiana na suala la Kaimu Jaji Mkuu na hasa hoja nzima ya kukaimiwa kwa nafasi ya Jaji Mkuu. Inasikitisha kwanza kwamba kuna watu wanasifia kuwa ametoa "darasa" na kwamba watu walikuwa wanamsikiliza kama wanafunzi katika Shule ya Msingi Mtakuja!

Je, ni kweli kile alichokisema watu walikuwa hawakijui? Ni kweli wabunge na wanasheria walioko Bungeni walikuwa hawajui yale yaliyokuwa yanasemwa?

Kuna hoja ya kuuliza swali; kwamba - kwanini Rais amemteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu kwa muda wote huu. Swali ambalo halipaswi kuulizwa na tulilikataa wakati ule ni kuhusu mamlaka ya Rais kumteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu. Hili liko ndani ya mamlaka ya Rais (Presidential prerogative). Lakini pia swali hili kwa ukubwa wake halipaswi kuulizwa isipokuwa kisiasa (political question) ili watu kupata hoja za kisiasa au ujiko wa kisiasa. Kwamba, mtu anataka kuonesha kuwa Magufuli amekosa mtu wa kuwa jaji mkuu, au kwamba Magufuli ana tatizo na mahakama n.k. Hili si jambo sahihi; wabunge kama wanaona Rais anatumia muda mrefu kujaza nafasi ya jaji mkuu wana uwezo wa kubadilisha sharia na hata Katiba chini ya Ibara ya 100 ya Katiba yetu.

Kama wanataka nafasi ya Jaji Mkuu isikaimiwe indefinitely (kama hoja ya Lissu ilivyoashiria) namna pekee ni kubadilisha Katiba au sheria ili kuweka kikomo kama ilivyo katika baadhi ya nafasi za utumishi wa umma ambapo sheria inasema mtu atakaimu nafasi kwa muda fulani na baada ya hapo basi mtu wa kudumu ateuliwe au aliyekaimu athibitishwe. Wao wabunge (watunga sheria na wanaoweza kufanya mabadiliko ya Katiba) wanaweza kuweka kikomo labda kwa ajili ya mustakabali)

Kama kwa mfano Rais angejaza cheo cha Ujaji siku moja tu baada ya Jaji Othman kustaafu wapo ambao labda wangeweza kuja na hoja ya kwanini amejaza nafasi haraka bila kuonesha tafakari sana au klutumia muda kufanya utafiti wa kutosha! Lakini pia kuna swali ambalo inabidi liulizwe kwa wale wanaolalamikia - kwa Rais kuweka Kaimu Jaji Mkuu ni shughuli gani ya Mahakama Kuu ambayo haiwezi kufanyika sasa hivi kwa vile kuna kaimu Jaji Mkuu au ni kitu gani hakifanyiki katika mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ambacho kinapaswa kufanywa na jaji mkuu peke yake. Hili ndilo linaweza kuwa hoja ya kwanini inahitajika Jaji Mkuu na siyo Kaimu Jaji Mkuu?

Lakini kung'ang'ania kitu ambacho wote wanajua hakipo - kwamba Rais hajavunja sheria wala Katiba, na kuwa hakuna kikomo cha muda kilichowekwa kwa hoja ya kuwa ni mazoea mapya haitoshi kuwa hoja.

Lakini wapo ambao wanasema kuwa kwa kutomthibitisha Kaimu Jaji basi Kaimu Jaji anaweza asifanye anayotakiwa kufanya kwa kuhofia kuiudhi mamlaka ya uteuzi. hilo si wazo sahihi katika utawala. Unapokaimu nafasi unakuwa na madara yote ambayo unayo kwa mujibu wa kukaimu kwako. Hakuna hoja ya kumridhisha mtu au la. Makamu wa Rais anapokaimu nafasi ya Urais wakati Rais hayupo kwa mujibu wa sharia ana madara yote ambayo ameruhusiwa kuwa nayo kwa mujibu wa Katiba. Na hili ni kweli kwa mtu mwingine yeyote ambaye Rais anaweza kumpa nafasi ya kukaimu jambo lolote kwa niaba yake. Mtu yeyote professional hajali sana kama atamfurahisha mtu au la atafanya kwa mujibu wa madaraka aliyopewa. Mtu ambaye atajali kuwa akifanya jambo Fulani atamuudhi aliyemteua au chombo cha juu hafasi kushika nafasi hiyo.

Somo ambalo Kabudi angepaswa kulitoa na labda wengi wanalihitaji kulielewa ni hili la Presidential prerogatives..
 
Back
Top Bottom