Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

Darasa la Prof. Kabudi Halikuwa la Lazima!

Hili la Jaji mkuu kukaimu lina jambo, halina uetetezi, Kabudi na darsa ilikuwa aibu
Sijaona mahali pengine panaposhawishi vinginevyo

By the way nakubaliana nawe , next time Kabudi aangalie darsa lisiwe lile tena

Haya mkuu wangu, nakupa neno la mwisho. Binafsi sina cha kuongeza kwa kweli hoja yangu bado inasimama.
 
Professor hukosea pia,tuna professor mwingine mchumi ana make headlines Sana,naye yu sawa?
 
Jamani, haya ndio matokeo ya demokrasia! Ukitaka wasiwe na nguvu hiyo unakuwa na wabunge wengi! Sasa kama wana wabunge wengi na wanatumia wingi wao kwa ajili ya maslahi yaona Rais au chama chao; ndio demokrasia uzuri na ubaya wake. Na tusipoangalia tutaendelea kuwa wkenye hali hii hadi tuamue kujenga upinzani wa kweli ambao unaweza kushinda angalau kuwa na Bunge! Hili huwezi kuwalalamikia CCM wasipounga mkono.
Hapo ndio kwenye safari ndefu,kwa tume hii hii ya uchaguzi?inatakiwa mkazo sana kwenye elimu ya uraia ili wananchi wajitambue wakati kunawatu wanatamani wawe na uwezo wa kuvifuta vyama vya upinzani.
 
Ninachokiamini si kweli wote Walikuwa wanajua alichokisema prof. Kabudi, kwahiyo kama unayajua alivyosema ni vema akawapa fursa wasiojua wajifunze, unachokijua wewe si wote wanajua, sioni kwanini iwe hoja, mbona wabunge walimsikiliza tena kwa makini?
 
Nadhani hapa tunamdhania sana Prof. Ibrahim; kwamba kwa namna fulani si mtu mwadilifu na kuwa hawezi kutekeleza wajibu wake kwa sababu ana hofu ya kupoteza hiyo nafasi kwa msingi wa hii 'security of tenure'. Kudhania huku msingi wake ni nini?

Mzee Mwanakijiji, naomba nirudie nukuu niliyoitoa awali...

Without security of tenure, an office-holder may find his or her ability to carry out their powers, functions and duties restricted by the fear that whoever disapprove of any of their decisions may be able to easily remove them from office in revenge.

Ni wapi hapa nimemdhania Prof. Ibrahim kwamba si mtu mwadilifu na kuwa hawezi kutekeleza wajibu wake kwa sababu ana hofu ya kupoteza nafasi hiyo? Hiyo ni nukuu inayoweza kutumika kwa mtu yeyote duniani ambaye nafasi aliyopewa si ya kudumu kwa maana kwamba ni kwa hiari tu ya mteuzi wakati ama anaendelea kumtafuta mwenye sifa anazozitaka au anaye mtu wake anayemtayarisha. Hivyo mteuzi anajipa kinga, sababu na urahisi wa kutengua uteuzi huo bila kutoa maelezo.

Lakini la muhimu zaidi Mzee Mwanakijiji, hebu jiweke upande wa huyo Prof. Ibrahim halafu ujiulize, hivi kwa kuendelea kukaimu nafasi hiyo kwa muda wote huu anajisikiaje? Je unadhani anapata usingizi bila kujiuliza ni kitu gani kimemfanya mteuzi wake kutomthibitisha kama Jaji Mkuu wakati wote huo? Je yawezekana mteuzi anamuona hatoshi kuvaa hivyo viatu na kwa maana hiyo cheo hicho kinamzidi kimo.? Je yawezekana mteuzi wake haridhishwi na utendaji wake na hivyo kusita kumthibitisha?

Naendelea kunukuu...

Security of tenure offers protection, by ensuring that an office-holder cannot be victimised for exercising their powers, functions and duties. It enables the democratic or constitutional methodology through which an office-holder comes to office not to be overturned except in the strictest and most extreme cases.

Narudia kusema kuwa nukuu hiyo haikuandikwa mahsusi kwa Prof. Ibrahim ila kwa wote wale ambao wamejikuta katika hali kama hiyo popote pale walipo ndani na nje ya Tanzania. Kwa kuendelea kukaimu, atawezaje kutekeleza majukumu lake kwa amani bila kujua hatma yake kama atadumu kwenye hiyo nafasi kwa muda gani na bila kinga yoyote? Mathalani kama ana makakati wa kuanzisha mchakato endelevu kiuwajibikaji, kweli atajituma huku kafunikwa na hilo wingu kubwa la mashaka ndani ya nafsi yake?

Na mwisho Mzee Mwanakijiji, je wewe binafsi unahisi ni sababu zipi zinazofanya Magufuli apate kigugumizi katika kumteua Jaji Mkuu? Kama Prof. Kabudi angekuwa mkweli kwa nafsi yake angetumia muda wake kuzijibu hoja za Mh. Tundu Lissu badala ya kutoa mipasho kama vile anaongea na watoto wa chekechea. Kwa maelezo aliyoyatoa amezidi tu kupigilia msumari hatma ya Kaimu Jaji Mkuu na kuonesha asivyo makini na matamshi yake...kwa lugha nyingine kazidi tu kamdhalilisha profesa mwenzanke.
 
Vitu ambavyo kaimu hawezi kuvifanya ni vile vinavyoelekezwa kwenye katiba kuwa vitafanywa na Jaji Mkuu kama Jaji Mkuu. Hivyo Kaimu Jaji Mkuu anaweza kufanya kila kinachofanywa na Jaji Mkuu isipokuwa kwenye kukaimu urais kwa sababu kukaimu ni delegated powers hivyo kwenye status ya delegated powers hawezi ku delegete wakati yeye sio mwenyewe kama ilivyo kwa kaimu rais anaweza kufanya kila kinachofanywa na rais ila hawezi kutia saini pale green inapotakiwa saini ya rais.

Paskali
Mkuu Paskali, chuoni tulifundishwa "delegatus non delegale" ... nisahihishwe kama nitakosea maandishi japo nina uhakika na mantiki. Uko sahihi kabisa.

Kaka ...
 
Mzee Mwanakijiji,

Na mwisho Mzee Mwanakijiji, je wewe binafsi unahisi ni sababu zipi zinazofanya Magufuli apate kigugumizi katika kumteua Jaji Mkuu? Kama Prof. Kabudi angekuwa mkweli kwa nafsi yake angetumia muda wake kuzijibu hoja za Mh. Tundu Lissu badala ya kutoa mipasho kama vile anaongea na watoto wa chekechea. Kwa maelezo aliyoyatoa amezidi tu kupigilia msumari hatma ya Kaimu Jaji Mkuu na kuonesha asivyo makini na matamshi yake...kwa lugha nyingine kazidi tu kamdhalilisha profesa mwenzanke.

Mimi na wewe sote tutakuwa tunafanya makosa ya kudhania sababu zilizomo kichwani mwa Rais. Ningependa tuweze kuzungumza kwa uhakika kwa kile tunachokijua. Nimesema hapo juu kama kweli Prof. Ibrahim anakosa hata usingizi kwa sababu hana uhakika wa usalama wa kibarua chake, hafai kuwa Jaji Mkuu. Binafsi naamini yeye anatekekelza wajibu wake kwa kadiri ya uwezo wake na kiapo chake. Alipoapishwa hakuambiwa atakuwa na "security of tenure"; na hakuambiwa itakuwa kwa muda gani. Aliiitikia wito wa taifa kutumika kwa wakati huu. Magufuli peke yake ndio anajua kwa uhakika sana kwanini hajamthibitisha au hajateua mwingine. Nje ya hapo we will be playing a guessing game.
 
Mkuu niwie radhi kidogo, kwanini nilipoandika 'probation' umepatwa na taharuki kidogo

Hapana, hata kidogo sijataharuki ila nashangaa kwanini inaletwa hilo badala ya kukubali tu anakaimu at the pleasure of the President. Nimesoma na wengine wanaitwa hii ni probation. Sidhani kama tunamtendea haki Kaimu Jaji.
 
Alaf jamaa wengine wanaandika kama wehu hata hawaeleweki simfupishe ? 🙁 unaaandikaaaaa alaf maana kiduchu
 
Hapana, hata kidogo sijataharuki ila nashangaa kwanini inaletwa hilo badala ya kukubali tu anakaimu at the pleasure of the President. Nimesoma na wengine wanaitwa hii ni probation. Sidhani kama tunamtendea haki Kaimu Jaji.
Sasa mkubwa mwenzangu, utendaji wa kazi kama unaoshauri hapa chini tuiite vipi? On Job training (OJT), Apprenticeship au Probation (ambayo umesema si nzuri).
... Rais yupo ndani ya uwezo na madaraka yake na hajafanya lolote lile la kuweza ku sema ama amevunja sheria au ametenda nje ya maslahi ya Taifa.

Atamteua Jaji Mkuu mwingine wakati muafaka au atamthibitisha aliyepo..
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hoja ya lissu mbona iko wazi kabisa...hajasema kuwa rais amekosea..anachosema lissu ni kuwa sheria zetu/katiba hazijaweka limit ya kuwa na acting chief Justice

Kitu ambacho kinaweza kuwa na madhara...hivi hebu chukulia kwa mfano rais aendelee kuwa na kaimu jaji hadi mwaka 2020.....hili jambo lin athari katika utendaji wa jaji

Kwa bahati mbaya Watu wengi huwa hamumuelewi Lisu kwa kipindi hicho anaongea...mnakuja kumuelewa baada ya miezi kadhaa au miaka kadhaa kupita
Lissu sasa ni Rais kama anavyojitanabai....abadilishe mambo...aache story
 
Kama haya ni malalamiko ya Jaji Ibrahim; na kama anaona hawezi kufanya kazi kwa weledi kwa vile anachelewa kuthibitishwa au uwezekano wa kuteuliwa mtu mwingine unaweza kumvuruga mbona si lazima awe Kaimu Jaji Mkuu; anaweza kabisa kumuomba Rais ajiuzulu ili Rais ateue mtu mwingine. Hivi, kwanini unafikiria Jaji Ibrahim na weledi wake wote ni mtu petty sana kuhusu hivi vyeo?
Umepewa hoja zote za kwa sababu gani haipendezi mtu kuwa Kaimu Jaji Mkuu kwa muda wote huo na mtu kama Pascal Mayalla amekutajia hadi sababu za msingi zinazoweza kumfanya Rais kuteua Kaimu Jaji Mkuu!!

Yote hayo huyataki!!!

Now your turn: Toa sababu moja tu ya msingi yenye busara ndani yake kwanini mtu awe Kaimu Jaji Mkuu muda wote huo!!! Sababu inaweza kuwa na uhalali wa kisiasa au hata kijamii... JUST ONE!

Usituambaie masuala ya kuvunja au kutovunja katiba kwa sababu JPM hana moral authority linapokuja suala la ulindaji wa katiba!!!

Isitoshe, hakuna anayesema JPM amevunja katiba kwenye hilo... sana sana watu wanailaumu katiba kutoa loophole ya Rais kuweza kukaa hata miaka 5 madarakani huku Mahakama ikiongozwa na Kaimu Jaji Mkuu kwa miaka yote hiyo!

Na hivyo, kwa sababu nilizotaja mwanzoni... Rais anaweza kubadilisha Kaimu Jaji Mkuu mara nyingi apendavyo bila kuwapo kwa legal argument kwamba Rais anavunja sheria!!!

Or else, labda ukiri kwamba Rais anatumia ana-take advantage ya mapungufu ya katiba kufanya vile anavyotaka yeye na hivyo kuthibitisha ile kauli ya Hayati Baba wa Taifa kwamba "Katiba hii inampa rais nguvu ya kuwa dikteta!"

Btw, mwanzoni nilikutajia watu walioyakana yale waliyokuwa wanayasimamia hapo mwanzoni kwa sababu tu ya madaraka na nikahitimisha kwamba, unless huyo Ibrahim ni very exceptional lakini nae hana tofaauti yoyote na akina Polepole, Mwakyembe, Kitila Mkumbo na wengine kahaa!!!

Kwavile umehoji kwanini watu waamini Ibrahimu anaweza kuwa cheap guy!! Jibu ni kwamba we make judgement basing on past experience or else, tuambie hapa ni nini kinachomfanya Profesa Ibrahimu awe so exceptional!

I hope post hii utaijibu kwa sababu una kawaida ya kuzikimbia baadhi ya post(hoja) though unaweza kuwa na sababu inayokubalika kwamba "...huwezi kujibu kila post!" hata kama utakuwa unafanya hivyo kwa kusukumwa na jambo lingine!!!
 
Now your turn: Toa sababu moja tu ya msingi yenye busara ndani yake kwanini mtu awe Kaimu Jaji Mkuu muda wote huo!!! Sababu inaweza kuwa na uhalali wa kisiasa au hata kijamii... JUST ONE!!!!
Yes, just one! Tumeuliza sana hili so far hakuna jibu.
Of course hatutegemei kutoka kwa Prof Kabudi baada ya 'syncope in the house ''
 
Mimi na wewe sote tutakuwa tunafanya makosa ya kudhania sababu zilizomo kichwani mwa Rais. Ningependa tuweze kuzungumza kwa uhakika kwa kile tunachokijua. Nimesema hapo juu kama kweli Prof. Ibrahim anakosa hata usingizi kwa sababu hana uhakika wa usalama wa kibarua chake, hafai kuwa Jaji Mkuu. Binafsi naamini yeye anatekekelza wajibu wake kwa kadiri ya uwezo wake na kiapo chake. Alipoapishwa hakuambiwa atakuwa na "security of tenure"; na hakuambiwa itakuwa kwa muda gani. Aliiitikia wito wa taifa kutumika kwa wakati huu. Magufuli peke yake ndio anajua kwa uhakika sana kwanini hajamthibitisha au hajateua mwingine. Nje ya hapo we will be playing a guessing game.
Mkuu Mzee Mwanakijiji, japo ni kweli haturuhusiwi kuhoji anachowaza rais wetu, lakini tunachoangalia ni matokeo ya maamuzi yake. Kila rais anachosema na anachotenda kinapitia public scrutiny ya kuhoji the logic behind.

Wengi wetu hujenga based on kilichofanyika kama hoja yako kuwa tusiingie mawazoni kwa rais. Baadhi yetu sisi hatuangalii kilichotendwa kumteua Kaimu Jaji Mkuu, bali tunajiuliza what is the motive behind uamuzi huu?!".

Katika searching for the motive behind ni kweli tutamuweka rais wetu kwenye mizania za assumptions huku tukiangalia logic katika maamuzi yake na assumptions hizo zikitueleza maamuzi hayo ni illogical, then ni illogical mpaka tupewe the reasons behind kujustfy logic.

Enzi za Nyerere kulikuwa na sheria mbaya sana ya Presidential Preventive Detention Order ambapo rais alikuwa na mamlaka ya kumuweka mtu yoyote kizuizini kwa kipindi chochote bila kuambiwa kosa lake!. Ikitokea mmegombea mwanamke na jamaa wa usalama ukamshinda, jamaa anaweza kuuundia zengwe ukaozea.

Kupitia prerogative order ya Habeas Copus, Prof.Shivij kupitia Kituo cha Msaada wa Kisheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakamshitaki rais (rais anashitakika), ndipo Mahakama Kuu ikamuamuru rais kuwa akimuweka mtu kizuizini kwa amri hiyo, lazima huyo mtu aelezwe makosa yake na kupitiwa haki ya kusikilizwa. Huyo jamaa aliposikilizwa kumbe ni ugomvi wa kugombea bibi!. Hivyo rais analazimishwa kutoa sababu.

Kiukweli katiba yetu imempa rais wetu mamlaka kubwa mno kufanya maamuzi bila kutoa sababu. Kiukweli kabisa, whatever the reasons he has, uamuzi huu wa kuikaimisha nafasi ya mhimili mmoja wa dola for too long ni uamuzi wa ajabu. Yaani unampa probation Prof. Ibrahim Juma!. Naomba nisiseme zaidi kuhusu Prof. Juma, ni kundi la caliber ya kina Shivji, ni watu waadilifu wa ajabu kabisa, wakati wenzao ni makada, hivyo waadilifu kwa chama kwanza ndipo kwenye sheria!.

Tufike mahali lazima rais wetu alazimishwe kutoa sababu za baadhi ya maamuzi yake!.

Paskali
 
Yes, just one! Tumeuliza sana hili so far hakuna jibu.
Of course hatutegemei kutoka kwa Prof Kabudi baada ya 'syncope in the house ''
Hakuna jibu na wakati wote ataendelea kuelezea hoja ile ile ambayo watu wamemtaka ufafanuzi lakini hatoi!! Ni kama mtu anayehubiri Injili ya 1+1=11 kisha watu kadhaa wanakazana kuuliza how come 1+1=11 lakini badala ya kueleza ni kwa vipi 1+1=11 badala ya 2; yeye bado anaendelea kukata mbuga na nyika... nchi na nchi; bara na bara huku akiendelea kuhubiri injili ile ile isiyoeleweka na watu ya kwamba 1+1=11 na sio 2!!!
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji, japo ni kweli haturuhusiwi kuhoji anachowaza rais wetu, lakini tunachoangalia ni matokeo ya maamuzi yake. Kila rais anachosema na anachotenda kinapitia public scrutiny ya kuhoji the logic behind.

Wengi wetu hujenga based on kilichofanyika kama hoja yako kuwa tusiingie mawazoni kwa rais. Baadhi yetu sisi hatuangalii kilichotendwa kumteua Kaimu Jaji Mkuu, bali tunajiuliza what is the motive behind uamuzi huu?!".

Katika searching for the motive behind ni kweli tutamuweka rais wetu kwenye mizania za assumptions huku tukiangalia logic katika maamuzi yake na assumptions hizo zikitueleza maamuzi hayo ni illogical, then ni illogical mpaka tupewe the reasons behind kujustfy logic.

Mpewe kama nani na kwanini? Rais halazimiki kutoa maelezo yake ya maamuzi yake. Tunaweza kudai ni vizuri tuambiwe lakini kama hakuna tatizo hadi hivi sasa tunachodai tunakidai kwa ajili gani hasa? Na vipi tutaridhika tukiambiwa sababu?


Enzi za Nyerere kulikuwa na sheria mbaya sana ya Presidential Preventive Detention Order ambapo rais alikuwa na mamlaka ya kumuweka mtu yoyote kizuizini kwa kipindi chochote bila kuambiwa kosa lake!. Ikitokea mmegombea mwanamke na jamaa wa usalama ukamshinda, jamaa anaweza kuuundia zengwe ukaozea.

Kupitia prerogative order ya Habeas Copus, Prof.Shivij kupitia Kituo cha Msaada wa Kisheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakamshitaki rais (rais anashitakika), ndipo Mahakama Kuu ikamuamuru rais kuwa akimuweka mtu kizuizini kwa amri hiyo, lazima huyo mtu aelezwe makosa yake na kupitiwa haki ya kusikilizwa. Huyo jamaa aliposikilizwa kumbe ni ugomvi wa kugombea bibi!. Hivyo rais analazimishwa kutoa sababu.

Mfano mzuri kwa kiasi ndio maana nimesema kama wanafikiri kuna sheria au sehemu ya Katiba imevunjwa; kuna namna moja tu ya kuresolve that; go to court! Kwanini kina Lissu au taasisi za wanasheria hawajaenda mahakamani "kudai" waambiwe kwanini Rais hajamthibitisha Ibrahim au hajateua mtu mwingine tusikie reasoning ya Serikali? Inawezekana hawajafanya hivyo kwa sababu wanajua ni kesi ambayo ngumu kushinda.


Kiukweli katiba yetu imempa rais wetu mamlaka kubwa mno kufanya maamuzi bila kutoa sababu. Kiukweli kabisa, whatever the reasons he has, uamuzi huu wa kuikaimisha nafasi ya mhimili mmoja wa dola for too long ni uamuzi wa ajabu. Yaani unampa probation Prof. Ibrahim Juma!. Naomba nisiseme zaidi kuhusu Prof. Juma, ni kundi la caliber ya kina Shivji, ni watu waadilifu wa ajabu kabisa, wakati wenzao ni makada, hivyo waadilifu kwa chama kwanza ndipo kwenye sheria!.

Hili wazo la probation ni fabrication ya fikra za watu tu. Amepewa kukaimu that's it; amekula kiapo cha kukaimu ndio hilo. Kama ni probation hakuna anayejua isipokuwa watu wamejiumbia wenyewe kwenye fikra zao. Tusije kutengeneza utaratibu kuwa kila Rais anapompa mtu nafasi ya kukaimu watu wakaanza kuona ni probation na kama hatothibitishwa basi waje kusema "hafai". Tusidai hilo kwa mtu mwenye weledi na caliber ya Prof. Ibrahim. Hatumtendei haki na kwa kweli hata mahakama yenyewe hatuitendei haki.


Tufike mahali lazima rais wetu alazimishwe kutoa sababu za baadhi ya maamuzi yake!.

Paskali

Hatakuwa tena RAis kama atakuwa analazimishwa. Na ukitaka njia nzuri badili katiba au sheria. Na njia sahihi ni kupata wabunge wengi wanaoweza kuunga mkono hoja hiyo. Haya ni matokeo ya demokrasia. lakini kutaka Rais alazimishwe tu ilimradi watu Fulani wasikie siyo sawa hata kidogo na sidhani kama nchi yeyote inaweza kuruhusu hilo. Si umeona hapa US wanavyohangaika kupata nakala za taarifa za kodi za Trump; kaam hataki kutoa hakuna namna ya kumlazimisha atoe. Ndio demokrasia. Tunapokataa udikteta wa mtu mmoja tusitengeneze na kukubali udikteta wa wengi - tyranny of the majority.
 
Back
Top Bottom