Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,240
- 44,487
- Thread starter
- #241
Umepewa hoja zote za kwa sababu gani haipendezi mtu kuwa Kaimu Jaji Mkuu kwa muda wote huo na mtu kama Pascal Mayalla amekutajia hadi sababu za msingi zinazoweza kumfanya Rais kuteua Kaimu Jaji Mkuu!!
Yote hayo huyataki!!!
Now your turn: Toa sababu moja tu ya msingi yenye busara ndani yake kwanini mtu awe Kaimu Jaji Mkuu muda wote huo!!! Sababu inaweza kuwa na uhalali wa kisiasa au hata kijamii... JUST ONE!
Hili ndilo tatizo; sasa mimi nitajuaje sababu ya uhakika ya kwanini hili limefanyika. Kama unataka nikisie nitakuambia sababu moja ni kuwa Rais bado hajaona sababu ya kumthibitisha aliyepo ama hajapata mtu wa kuchukua nafasi hiyo. Ukiniuliza "kwanini" nitakuambia sijui ni Rais mwenyewe anajua. Na kwa vile hakuna sheria imevunjwa sina tatizo. Nasubiri tu amthibitisha Ibrahim au amteue mwingine. That is his prerogative. Nje ya hapo nitakuwa kwenye klabu ya wadhaniao.
Usituambaie masuala ya kuvunja au kutovunja katiba kwa sababu JPM hana moral authority linapokuja suala la ulindaji wa katiba!!!
Huna sababu ya kupayuka; naweza kusoma vizuri tu.
Isitoshe, hakuna anayesema JPM amevunja katiba kwenye hilo... sana sana watu wanailaumu katiba kutoa loophole ya Rais kuweza kukaa hata miaka 5 madarakani huku Mahakama ikiongozwa na Kaimu Jaji Mkuu kwa miaka yote hiyo!
Na hivyo, kwa sababu nilizotaja mwanzoni... Rais anaweza kubadilisha Kaimu Jaji Mkuu mara nyingi apendavyo bila kuwapo kwa legal argument kwamba Rais anavunja sheria!!!
Sasa kama havunji tatizo liko wapi; kama tatizo ni la kisheria njia ni kufix it kwa kutumia taratibu za kibunge za kushughulikia mapungufu ya kisheria au hata Kikatiba.
Or else, labda ukiri kwamba Rais anatumia ana-take advantage ya mapungufu ya katiba kufanya vile anavyotaka yeye na hivyo kuthibitisha ile kauli ya Hayati Baba wa Taifa kwamba "Katiba hii inampa rais nguvu ya kuwa dikteta!"
Hili linawezekana lakini ndio mazao ya demokrasia na sheria. Kile ambacho sheria haikatazi, sheria inaruhusu. Na mtu hawezi kuadhibiwa kwa kitu ambacho si kosa kisheria.
Btw, mwanzoni nilikutajia watu walioyakana yale waliyokuwa wanayasimamia hapo mwanzoni kwa sababu tu ya madaraka na nikahitimisha kwamba, unless huyo Ibrahim ni very exceptional lakini nae hana tofaauti yoyote na akina Polepole, Mwakyembe, Kitila Mkumbo na wengine kahaa!!!Well, kama kila mtu yuko hivi; na kwamba hakuna tena waadilifu (unless ukimaanisha wale nje ya serikali tu ndio waadilifu) basi hakuna matumaini kwani hakuna yeytoe ambaye ana tofauti. Hii ni namna mbaya sana ya kuubariki uzembe, ufisadi na utendaji mbovu wa kazi. Kama kila mtu ni mbovu basi haijalishi kama mtu anakaimu au anathibitishwa. Wote kama wasemavyo wajomba zangu "zikongwine".
Kwavile umehoji kwanini watu waamini Ibrahimu anaweza kuwa cheap guy!! Jibu ni kwamba we make judgement basing on past experience or else, tuambie hapa ni nini kinachomfanya Profesa Ibrahimu awe so exceptional!
That's is silly; how can you make a judgement on somebody based on someone else's past experience. Unless you are saying that you know something about Prof. Ibrahim compromising incompetency and professional mediocrity. Is that what you are saying?
I hope post hii utaijibu kwa sababu una kawaida ya kuzikimbia baadhi ya post(hoja) though unaweza kuwa na sababu inayokubalika kwamba "...huwezi kujibu kila post!" hata kama utakuwa unafanya hivyo kwa kusukumwa na jambo lingine!!!
Not really, huwa najibu watu ambao najua tunaweza kujadiliana nao kwa staha na heshima. Sijibu mtu yeyote ambaye for whatever reason hawezi kufanya majadiliano bila vijembe vya kitoto au mashindano ya kisiasa. Na wakati mwingine sijibu kwa sababu bado nafikiri jibu vizuri. Sipendi kujibu out of impulse.