Nadhani hapa tunamdhania sana Prof. Ibrahim; kwamba kwa namna fulani si mtu mwadilifu na kuwa hawezi kutekeleza wajibu wake kwa sababu ana hofu ya kupoteza hiyo nafasi kwa msingi wa hii 'security of tenure'. Kudhania huku msingi wake ni nini?
Prof Ibrahim hana tatizo katika mjadala huu kabisa. Yeye ni mteuliwa
Prof kateuliwa na Rais baada ya kupewa majina. Kumteua Prof ni prerogative ya Rais , hakuna tatizo katika hilo na anatumia vigezo gani ni privilege ambayo kama prerogative haina tatizo
Ni makosa makubwa kwa yoyote kumtuhumu Prof iwe kwa uteuzi au uwezo wake
Ni makosa kudhania au kutilia shaka uadilifu wa Prof Ibrahim kuhusu uwezo wa majukumu yake
Msingi wa wa dhana yoyote inayoonyesha Prof kukwazwa inajengwa na 'Teuzi'
Nafasi ya kukaimu ina makusudi talaa linatokea lisilotarajiwa na mhimili lazima usimame
Prof Kabudi anaposimama na kutupa historia ya Nyerere bila kutueleza nini kinatokea leo
Kwamba jibu la kwanini kuna kukaimu kwa muda mrefu ni 'Nyerere alifanya hivyo pia'
''That was too low!'' Prof Kabudi alitakiwa asimame na kujibu hoja ya Lissu kwanini kuna kukaimu kwa muda mrefu. Tungepewa jibu rahisi kama la Nyerere! hakuna
Tena Lissu alisema kuna mambo mawili. Prof Ibrahim athibitishwe au achaguliwe mwingine
Hilo linatuacha na hoja kuwa, Prof amewekwa njia panda kwa kazi ya 'probation'
Uteuzi wa Jaji mkuu unapowekewa probation lipo tatizo!
Mhimili wa sheria unapoteza nguvu kwasababu Jaji mkuu ni alama ya mhimili
Kazi ya kwanza ya Bunge ni kumpata Spika, si kumpata kaimu Spika
Kazi ya kwanza ya Serikali ni kumpata Rais si Kaimu Rais
Teuzi ya kwanza ya Rais ni Mwanasheria mkuu si kaimu mwanasheria mkuu
Leo tuna Kaimu Jaji mkuu ambaye akiwa na Rais na Spika, yeye yupo katika 'probation'
Swali ambalo Prof Kabudi na MM wanaweza kutusaidia ni moja, kuna sababu gani za nafasi ya Jaji mkuu kwa mwaka 2017 kukiwa na wastaafu, wazoefu, vijana n.k. katika fani ya sheria kuwekewa kaimu Jaji katika mtindo wa 'probabtion'
Kabudi hakuwa na majibu, alizunguka zunguka na hakika 'darsa' alilosimama ilikuwa aibu
Labda MM anajibu, so far hatujaona katika aliyoandika