Kyatile
JF-Expert Member
- Feb 5, 2017
- 1,739
- 1,585
Na wewe huwa haumuelewi?Tundu Lisu haeleweki kwa sababu ni retarded!
Na wewe huwa haumuelewi?Tundu Lisu haeleweki kwa sababu ni retarded!
Prof Kabudi amejibu kuwa Rais Nyerere alifanya hivyo pia! Niliposikia hilo jibu nikajua siasa si mchezo, na sikuamini nilichosikia
Lakini, hata kama Nyerere atatumika kama 'template' bado kuna hoja. Mwl alieleza kwanini alichukua muda kumteua Jaji mkuu. Mwl alikuwa na presidential prerogative ya kumwacha Jaji mzungu. Kwa busara za wakati hakutumia prerogative hiyo kiholela
Aliitumia kwenda kutafuta Jaji kutoka Commonwealth kwa spirit ya matumizi sahihi ya prerogative. Leo Prof na MM hawana jibu kwanini nafasi hiyo nyeti ikaimiwe miezi 5 Nimekubaliana naye kwa sheria kutovunjwa, nimekubaliana naye kwa ''prerogative power''.
Nisichokubaliana naye ni matumizi ya prerogative.
Prerogative iliwekwa makusudi ili kumpa uwezo wa kutenda ndani ya Busara
Rais ana prerogative ya kuteua wabunge 10. Kwa kutambua anaweza ku misuse prerogative, sheria ikasema wawepo makundi kadhaa.
Hapa busara zimetumika kuhakikisha Rais kwa jinsia yoyote hatatimiza masharti bila busara
Niliwahi kujadili, katika wabunge 10 Rais anaweza kuteua wote kutoka kwa familia yake na bado hajavunja sheria. Atakuwa ametumia prerogative, lakini je, busara za hilo zina impact gani na ni kwa national interest?
Prerogative ya kuteua kaimu Jaji mkuu ipo, lakini kama zingine imewekewa uzio na sababu zake. Haipo wazi tu kama MM anavyodhani, na asivyoweza kueleza jamvi kama alivyofeli Prof Kabudi
Ikitokea sababu muhimu nje ya zilizoanishwa kama ya Mwl, umma una haki ya kujua.
Hapo ndipo hoja ya Lissu si kuwa inapata miguu bali inatembea bila kupingwa.
Kabudi hakuweza, MM hadi sasa hajaweza. Pengine anajipanga tumpe muda
Wapinzani walitoa hoja ya kujadili hali ya usalama wa Taifa.
CCM-wabunge kwa kuelewa mhimili huo nao 'unakaimiwa' wakakataa
Siku tatu baadaye, CCM hao hao wakataka ijadiliwe baada ya matatizo Kibiti
Juzi wakati Prof Kabudi anajikanyaga kanyaga walikuwa wanapiga makofi.
Leo ukiwauliza kwanini nafasi hiyo ikaimiwe kwa muda mrefu hakuna anayeweza kueleza, afadhali ya Prof Kabudi alijihifadhi kwa Nyerere, MM anatumia prerogative
Kuna kiongozi aliteuliwa kwa prerogative, akapitishwa na chama kwa prerogative, na akachaguliwa katika taasisi nyeti kwa prerogative.
Matatizo ya taasisi ni kutokana na kiongozi kufanya kazi kwa 'fadhila' za prerogative
Masuala ya kitaifa yanajadiliwa akitazama 'prerogative' iliyomfikisha hapo. Tunafeli sote
Watu wengi wasichokiona ni umuhimu wa mhimili wa sheria.
Mhimili huo unapopoteza nguvu zake za asili ni hatari
Uchaguzi wa TLS uliingiliwa na serikali, tukasikia kauli zenye mwelekeo wa 'kisiasa'
Pengine hii ni katika kuonyesha misuli ya ''mhimili uliozama zaidi kwenda chini''
Swali, je, hayo ni kwa public interest au ni kwa interest ya mtu au watu?
Kama haya ni malalamiko ya Jaji Ibrahim; na kama anaona hawezi kufanya kazi kwa weledi kwa vile anachelewa kuthibitishwa au uwezekano wa kuteuliwa mtu mwingine unaweza kumvuruga mbona si lazima awe Kaimu Jaji Mkuu; anaweza kabisa kumuomba Rais ajiuzulu ili Rais ateue mtu mwingine. Hivi, kwanini unafikiria Jaji Ibrahim na weledi wake wote ni mtu petty sana kuhusu hivi vyeo?
Umejuaje kama Prof. Ibrahim ni mtu wa namna hiyo? kwamba siyo professional enough kuweza kusimamia kiapo chake kwa muda wote ambao anakaimu cheo hicho?
Kwanini amteue moja kwa moja?Hivi kama mmojawapo wa majaji waliopo wanatosha kuwa Jaji Mkuu, kwa nini Rais asimteue moja kwa moja?
MM kuna mambo matatu, sheria, prerogative na privilege Rais amepewa kisheria. Kama Rais hajavunja sheria, hajavunja Katiba, hatumia madaraka vibaya ni kwanini watu wanataka afanye jambo ambalo anapanga kulifanya anyway?
Ni matumaini yangu kwa mchango wako huu, hata wale wanaotumwa na vyama vyao kushabikia wamekuelewa na watabadiri mtazamo.Sijasikiliza hayo ya bungeni na sidhani kama bado nina interest ya siasa za bunge hivi sasa ambazo kwangu naona ni kama zimekosa mvuto!!
Tuje kwenye hiyo hja ya kwamba, kukaimu kwa muda mrefu hakuwezi kumfanya Kaimu Jaji kushindwa kufanya kazi zake sawa sawa!!!
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Rais hana mamlaka ya kumtumbua Jaji wa Mahakama Kuu kirahisi rahisi tu!
Inapotokea sababu ambazo rais anaona Jaji huyu hafai tena kuwa jaji, hata kama ni suala la ukosefu wa maadili, bado Rais anatakiwa kwanza kuunda Tume ambayo itakuwa na Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume, na miongoni mwao angalau nusu wanatakiwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu kutoka nchi za Jumuiya ya Madola!
Tume hii itachunguza tuhuma dhidi ya Jaji kuona kama ni kweli au hapana!
NOTE: Nitapitia katiba ili nione kifungu hicho kinasemaje kwa yakini!!
Kutokana na kifungu hicho cha Katiba, Jaji Mkuu na in fact, Jaji yeyote wa Mahakama Kuu hawezi kuwa na hofu ya kutekeleza wajibu wake kwa kuhofia mamlaka ya uteuzi kwa sababu, anafahamu, hawezi kuondolewa hovyo hovyo au hata kwa makosa ya kubambikiwa!!!
Kaimu Jaji Mkuu kwa nafasi yake hiyo sio Jaji wa kawaida na wala sio Jaji Mkuu ambao wanaweza kulindwa na kifungu hicho hapo juu! Kwahiyo, Rais anaweza kumtoa muda wowote bila maswali kwa sababu, atakachomvua sio Ujaji wala Ujaji Mkuu bali Ukaimu Jaji Mkuu ambao sidhani kama Katiba inatoa ulinzi niliotaja hapo juu!!!
Hoja ndiyo hiyo hapo juuu!!
Na kwa staili hiyo, unaweza kuteua Kaimu Jaji Mkuu kama ilivyo sasa; na ukiona anazingua unamtoa unamweka mwingine nae anakuwa Kaimu Jaji Mkuu!! Sasa hofu isije kwamba, kwa kuhofia kutokuwa na ulinzi wa katiba, basi huenda wengine wanaweza kufanya mambo kwa kuyaridhisha mamlaka ya uteuzi!!
Isitoshe, huyu Kaimu Jaji Mkuu kila wakati atakuwa anaota kuwa Jaji Mkuu na sio kaimu tena!! Kwa namna ya kawaida kabisa; lazima ndoto zake zitaenda sambamba na kuhakikisha hazikeri mamlaka ya uteuzi!!
Kila prerogative imejengewa uzio. Presidential prerogative ina Trust.
Kwamba, mkuu wa nchi amepewa jukumu zito na hiyo tu ni trust.
Prerogative pamoja na conditions inategemea Trust kwasababu ya public interest
Mambo yanayohusu prerogative hayapo kisheria moja kwa moja, yamejengewa uzio tu kwamba asivuke eneo fulani au acheze katika eneo fulani.
Ikitokea nje ya hapo prerogative inageuka kuwa abuse of power na mistrust
Kwa suala la Jaji, sheria imetamka uwepo wa Jaji mkuu na Kaimu jaji mkuu
Kaimu Jaji mkuu imewekwa ili kutoa prerogative kwa public interest si kwa personal interest. Hapa ndipo unapochanganya
Hakuna sheria iliyovunjwa, hakuna katiba iliyokiukwa, kuna kila dalili za matumizi mabaya ya prerogative. Hizo zinabaki kuwa hisia, lakini je, ni za kunyamazia?
Prof Kabudi alieleza Nyerere kwa kuelewa kilichotokea ili kupata public trust na kwamba matumizi ya prerogative yapo salama. Alikuwa na prerogative, haikutosha bila trust
Swali, tunasababu gani za kutumia prerogative kwa miezi 5 ya kukaimu nafasi?
Hatusemi ni makosa, tunauliza kwasababu 'mamlaka inatoka kwa wananchi' kama alivyofanya Mwl. kwa kuujulisha umma kwanini ilitokea vile
Kama ni suala la kuwa mtu anaamini kuwa prerogative imekuwa abused; lakini hana namna ya kuthibitisha kuwa imekuwa abused siwezi kutolea maoni maana masuala ya imani kwa kweli ni ya mtu mwenyewe. Kuna watu wanaamini vitu vya ajabu sana duniani na wengine wako tayari kujitoa mhanga kwa ajli yake au hata kuapa kwa mbingu na na nchi.Kama hakuna sababu au majibu, kuna kila sababu ya kuamini kuwa prerogative imekuwa ''abused''. Ikiwa hilo si kweli, tupeni sababu zenye mashiko
Kwa sababu amekidhi vigezo na nafasi ipo wazi.Kwanini amteue moja kwa moja?
Mkuu, hatuwezi ku ignore hoja ya kwamba kuna abuse hata kama ni kwa 'imani'Kama ni suala la kuwa mtu anaamini kuwa prerogative imekuwa abused; lakini hana namna ya kuthibitisha kuwa imekuwa abused siwezi kutolea maoni maana masuala ya imani kwa kweli ni ya mtu mwenyewe. Kuna watu wanaamini vitu vya ajabu sana duniani na wengine wako tayari kujitoa mhanga kwa ajli yake au hata kuapa kwa mbingu na na nchi.
Mkuu, hatuwezi ku ignore hoja ya kwamba kuna abuse hata kama ni kwa 'imani'
Rais kwa mujibu wa katiba ana prerogative ya kuteua wabunge 10.
Anaweza kuteua watoto wake na mkewe na shemeji yake mdogo wakafika 10.
Hatakuwa amevunja sheria, au katiba
Tuta amini amefanya hivyo kwa imani tu kwamba ana prerogative ambayo ni sahihi
Kwa jicho lingine linalohitaji fikra, atakuwa ame abuse prerogative aliyopewa
Utathibitishaje kuwa haku abuse ikiwa kila kitu kipo sawa?
Utathibitisha kwa kutumia trust and public interest, hivi ni vitu vya 'imani' vyenye impact katika society.
Pili, mtu anaweza kuhukumiwa 'kuua kwa kudhamiria au kutodhamiria'
Dhamira ni kitu tuischoweza kukijua kwani kipo ndani ya mtu
Tunaweza kuthibitisha 'kudhamiria au kutodhamiria' kwa kuangalia mazingira ya tukio
Hili la Jaji kukaimu lina mazingira mzuri tu, kwa kuangalia utaratibu, muda, na ''utangamano wa mihimili'' kauli na mengi tu.
Public interest ni pale inapokuwa na hofu kuhusu 'probabtion' ya Jaji mkuu. Utaratibu wa kumuondoa Jaji mkuu na kumuondoa Kaimu ni tofauti"Mzee Mwanakijiji, post: 20890882, member: 118"] hadi hivi sasa hakuna kwa kiwango cha kutosha public interests ukiondoa zile zinazoonekaa ni za kisiasa.
Hapa nakubaliana nawe kwasababu hata alipowaambia Wanasheria wamalize kesi atawapa robo ya mapato, wao hawakuona ni jambo la hatariKwa mfano, chama cha wanasheria (TLS), Chama cha Majaji wastaafu n.k vikitoa tamko kuonesha kuwa kuna tatizo basi tunaweza tukasema kweli lipo; kwa sababu inaonekana ni kweli suala hili ni kubwa kivile. So far hakuna
Kama sikosei ''wainglishi'' wanasema unapokuwa public figure unaoteza baadhi ya mambo na hifadhi yako inakuwa haipo tenaMagufuli anaweza akakohoa hadharani na watu wakafanya ni hoja ya kisiasa. Anaweza akajikwaa na watu wakaona ni kwa nini amejikwaa wakati yeye ni Rais!.
Mazingira ya kukaimu ni kama hakuna wenye sifa ndiyo hutumika lakini hapa mamlaka yametumika vibayaNimesikiliza kwa makini kile kinachoitwa "darasa" la Prof. Kabudi jana Bungeni kuhusiana na suala la Kaimu Jaji Mkuu na hasa hoja nzima ya kukaimiwa kwa nafasi ya Jaji Mkuu. Inasikitisha kwanza kwamba kuna watu wanasifia kuwa ametoa "darasa" na kwamba watu walikuwa wanamsikiliza kama wanafunzi katika Shule ya Msingi Mtakuja!
Je, ni kweli kile alichokisema watu walikuwa hawakijui? Ni kweli wabunge na wanasheria walioko Bungeni walikuwa hawajui yale yaliyokuwa yanasemwa?
Kuna hoja ya kuuliza swali; kwamba - kwanini Rais amemteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu kwa muda wote huu. Swali ambalo halipaswi kuulizwa na tulilikataa wakati ule ni kuhusu mamlaka ya Rais kumteua mtu kukaimu Ujaji Mkuu. Hili liko ndani ya mamlaka ya Rais (Presidential prerogative). Lakini pia swali hili kwa ukubwa wake halipaswi kuulizwa isipokuwa kisiasa (political question) ili watu kupata hoja za kisiasa au ujiko wa kisiasa. Kwamba, mtu anataka kuonesha kuwa Magufuli amekosa mtu wa kuwa jaji mkuu, au kwamba Magufuli ana tatizo na mahakama n.k. Hili si jambo sahihi; wabunge kama wanaona Rais anatumia muda mrefu kujaza nafasi ya jaji mkuu wana uwezo wa kubadilisha sharia na hata Katiba chini ya Ibara ya 100 ya Katiba yetu.
Kama wanataka nafasi ya Jaji Mkuu isikaimiwe indefinitely (kama hoja ya Lissu ilivyoashiria) namna pekee ni kubadilisha Katiba au sheria ili kuweka kikomo kama ilivyo katika baadhi ya nafasi za utumishi wa umma ambapo sheria inasema mtu atakaimu nafasi kwa muda fulani na baada ya hapo basi mtu wa kudumu ateuliwe au aliyekaimu athibitishwe. Wao wabunge (watunga sheria na wanaoweza kufanya mabadiliko ya Katiba) wanaweza kuweka kikomo labda kwa ajili ya mustakabali)
Kama kwa mfano Rais angejaza cheo cha Ujaji siku moja tu baada ya Jaji Othman kustaafu wapo ambao labda wangeweza kuja na hoja ya kwanini amejaza nafasi haraka bila kuonesha tafakari sana au klutumia muda kufanya utafiti wa kutosha! Lakini pia kuna swali ambalo inabidi liulizwe kwa wale wanaolalamikia - kwa Rais kuweka Kaimu Jaji Mkuu ni shughuli gani ya Mahakama Kuu ambayo haiwezi kufanyika sasa hivi kwa vile kuna kaimu Jaji Mkuu au ni kitu gani hakifanyiki katika mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ambacho kinapaswa kufanywa na jaji mkuu peke yake. Hili ndilo linaweza kuwa hoja ya kwanini inahitajika Jaji Mkuu na siyo Kaimu Jaji Mkuu?
Lakini kung'ang'ania kitu ambacho wote wanajua hakipo - kwamba Rais hajavunja sheria wala Katiba, na kuwa hakuna kikomo cha muda kilichowekwa kwa hoja ya kuwa ni mazoea mapya haitoshi kuwa hoja.
Lakini wapo ambao wanasema kuwa kwa kutomthibitisha Kaimu Jaji basi Kaimu Jaji anaweza asifanye anayotakiwa kufanya kwa kuhofia kuiudhi mamlaka ya uteuzi. hilo si wazo sahihi katika utawala. Unapokaimu nafasi unakuwa na madara yote ambayo unayo kwa mujibu wa kukaimu kwako. Hakuna hoja ya kumridhisha mtu au la. Makamu wa Rais anapokaimu nafasi ya Urais wakati Rais hayupo kwa mujibu wa sharia ana madara yote ambayo ameruhusiwa kuwa nayo kwa mujibu wa Katiba. Na hili ni kweli kwa mtu mwingine yeyote ambaye Rais anaweza kumpa nafasi ya kukaimu jambo lolote kwa niaba yake. Mtu yeyote professional hajali sana kama atamfurahisha mtu au la atafanya kwa mujibu wa madaraka aliyopewa. Mtu ambaye atajali kuwa akifanya jambo Fulani atamuudhi aliyemteua au chombo cha juu hafasi kushika nafasi hiyo.
Somo ambalo Kabudi angepaswa kulitoa na labda wengi wanalihitaji kulielewa ni hili la Presidential prerogatives..
Lissu SIYO retarded, NI RETARDER!Tundu Lisu haeleweki kwa sababu ni retarded!
Hapana bana; hapa tena unadhania vile vile. Hatujui ni kwanini Rais amechukua muda mrefu kujaza nafasi hiyo. kama wapo watu wenye sifa ya kuteuliwa kuwa majaji wa mahakama kuu basi wapo wenye sifa ya kuweza kuwa jaji mkuu. Bila ya shaka kuna sababu nyingine ambazo hatuzijui za kwanini amechelewa kujaza nafasi hii. Sababu hizo zikiondoka au kushughulikiwa bila ya shaka nafasi hiyo itajazwa na mtu wa kudumu. Nje yapo tutakuwa kama wapiga ramli.Mazingira ya kukaimu ni kama hakuna wenye sifa ndiyo hutumika lakini hapa mamlaka yametumika vibaya
Public interest ni pale inapokuwa na hofu kuhusu 'probabtion' ya Jaji mkuu. Utaratibu wa kumuondoa Jaji mkuu na kumuondoa Kaimu ni tofauti
Hilo linatia shaka na maamuzi ya Kaimu. Inaweza kuwa shaka tu, lakini ni shaka yenye public interestHapa nakubaliana nawe kwasababu hata alipowaambia Wanasheria wamalize kesi atawapa robo ya mapato, wao hawakuona ni jambo la hatari
Alipowaambia mawakili wanaosimama 'wahalifu' nao wawekwe ndani hakuna aliyeona ni jambo lililo kinyume.
Hata alipoingilia uchaguzi kwa mkono wa serikali , walinung'unika tu chini chini.
Chama cha majaji wastaafu kilisema 'kuna nchi zinamatamani ziwe na Rais huyu hata kwa siku' Hii ndiyo kauli tuliosikia. Kama sikosei ''wainglishi'' wanasema unapokuwa public figure unaoteza baadhi ya mambo na hifadhi yako inakuwa haipo tena
Ndivyo ilivyo kwa viongozi wote duniani hata watu maarufu, si kwake pekee
Lakini mkuu hizo sababu nyingine si ndio hasa wanaohoji wanaona wanayo haki ya kizijua?Hapana bana; hapa tena unadhania vile vile. Hatujui ni kwanini Rais amechukua muda mrefu kujaza nafasi hiyo. kama wapo watu wenye sifa ya kuteuliwa kuwa majaji wa mahakama kuu basi wapo wenye sifa ya kuweza kuwa jaji mkuu. Bila ya shaka kuna sababu nyingine ambazo hatuzijui za kwanini amechelewa kujaza nafasi hii. Sababu hizo zikiondoka au kushughulikiwa bila ya shaka nafasi hiyo itajazwa na mtu wa kudumu. Nje yapo tutakuwa kama wapiga ramli.
''Probation''"Mzee Mwanakijiji, post: 20891553, member: 118"]Umepata wapi hili wazo kuwa Kaimu Jaji Mkuu yuko kwenye probabation?
Sina takwimu lakini waziri anapojibu mbele ya wabunge 200+hatuwezi kusema ni watu 2Haiwezekani shaka ya watu wawili au watatu itoshe kuwa shaka ya "umma" mzima.
Mkuu si wewe umezungumzia kuhusu TLS na chama cha majaji, nami kikasema ni kweli hatujasikia kauli zao.Haya ni mambo mengine; irrelevant kwenye hoja hii
Lakini mkuu hizo sababu nyingine si ndio hasa wanaohoji wanaona wanayo haki ya kizijua?
Wanataka kujiridhisha kuwa hizo sababu ni zenye mashiko au maslahi ya umma.
Zisiposemwa, ni wazi watu watajaribu kufikiria za kwako.
Hivi ni sahihi kufikiri kuwa Katiba yetu ilikusudia kumpa Rais discretion ya kutoteua Jaji Mkuu na badala kuteuwa Kaimu Jaji Mkuu bila ukomo wowote?