"Allen Kilewella, post: 20880835, member: 55849"]
Nguruvi3 Hii hoja ajabu ya mwaka kwanza
Mzee Mwanakijiji anaipindisha ama pia hataki kuijibu. Swali la Lissu ambalo halijajibiwa na huyo "mtoa darsa" wao na hata na Mzee mwanakijiji mwenyewe ni kwamba kuna sababu gani ya msingi mhimili kama Mahakama kuwa na kiongozi anayekaimu nafasi yake kwa miezi mitano sasa?
Prof Kabudi amejibu kuwa Rais Nyerere alifanya hivyo pia! Niliposikia hilo jibu nikajua siasa si mchezo, na sikuamini nilichosikia
Lakini, hata kama Nyerere atatumika kama 'template' bado kuna hoja. Mwl alieleza kwanini alichukua muda kumteua Jaji mkuu. Mwl alikuwa na presidential prerogative ya kumwacha Jaji mzungu. Kwa busara za wakati hakutumia prerogative hiyo kiholela
Aliitumia kwenda kutafuta Jaji kutoka Commonwealth kwa spirit ya matumizi sahihi ya prerogative. Leo Prof na MM hawana jibu kwanini nafasi hiyo nyeti ikaimiwe miezi 5
Mosi nakubaliana na hoja ya Mwanakijiji kwamba hakuna sheria iliyovunjwa, lakini kwa tukio hili lazima tugutushwe kwamba kama hakuna sheria ilivyovunjwa
Nimekubaliana naye kwa sheria kutovunjwa, nimekubaliana naye kwa ''prerogative power''.
Nisichokubaliana naye ni matumizi ya prerogative.
Prerogative iliwekwa makusudi ili kumpa uwezo wa kutenda ndani ya Busara
Rais ana prerogative ya kuteua wabunge 10. Kwa kutambua anaweza ku misuse prerogative, sheria ikasema wawepo makundi kadhaa.
Hapa busara zimetumika kuhakikisha Rais kwa jinsia yoyote hatatimiza masharti bila busara
Niliwahi kujadili, katika wabunge 10 Rais anaweza kuteua wote kutoka kwa familia yake na bado hajavunja sheria. Atakuwa ametumia prerogative, lakini je, busara za hilo zina impact gani na ni kwa national interest?
Prerogative ya kuteua kaimu Jaji mkuu ipo, lakini kama zingine imewekewa uzio na sababu zake. Haipo wazi tu kama MM anavyodhani, na asivyoweza kueleza jamvi kama alivyofeli Prof Kabudi
Ikitokea sababu muhimu nje ya zilizoanishwa kama ya Mwl, umma una haki ya kujua.
Hapo ndipo hoja ya Lissu si kuwa inapata miguu bali inatembea bila kupingwa.
Kabudi hakuweza, MM hadi sasa hajaweza. Pengine anajipanga tumpe muda
Bunge hili lililojaa wabunge wa CCM haiwezekani kupeleka hoja inayopingana na mtazamo na utashi wa Rais ikakubalika ama ikapitishwa. Tumeona ni kwa jinsi gani wabunge hao wanapoungana dhidi ya hoja yoyote ile inayopingwa na Serikali. Jibu ni rahisi, wabunge wanaujua ukuu wa chama (Party Supremacy) kwenye nafasi zao walizonazo za ubunge!
Wapinzani walitoa hoja ya kujadili hali ya usalama wa Taifa.
CCM-wabunge kwa kuelewa mhimili huo nao 'unakaimiwa' wakakataa
Siku tatu baadaye, CCM hao hao wakataka ijadiliwe baada ya matatizo Kibiti
Juzi wakati Prof Kabudi anajikanyaga kanyaga walikuwa wanapiga makofi.
Leo ukiwauliza kwanini nafasi hiyo ikaimiwe kwa muda mrefu hakuna anayeweza kueleza, afadhali ya Prof Kabudi alijihifadhi kwa Nyerere, MM anatumia prerogative
Kuna kiongozi aliteuliwa kwa prerogative, akapitishwa na chama kwa prerogative, na akachaguliwa katika taasisi nyeti kwa prerogative.
Matatizo ya taasisi ni kutokana na kiongozi kufanya kazi kwa 'fadhila' za prerogative
Masuala ya kitaifa yanajadiliwa akitazama 'prerogative' iliyomfikisha hapo. Tunafeli sote
Watu wengi wasichokiona ni umuhimu wa mhimili wa sheria.
Mhimili huo unapopoteza nguvu zake za asili ni hatari
Uchaguzi wa TLS uliingiliwa na serikali, tukasikia kauli zenye mwelekeo wa 'kisiasa'
Pengine hii ni katika kuonyesha misuli ya ''mhimili uliozama zaidi kwenda chini''
Swali, je, hayo ni kwa public interest au ni kwa interest ya mtu au watu?