Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Ikiwa ni siku 4 tangu Afisa Programu na Elimu kwa Umma wa LHRC, Tito Magoti ‘atekwe’ na wasiojulikana, kuna taarifa kuwa mwandishi Bollen Ngeti naye ametekwa na wasiojulikana leo maeneo ya Msasani, Dar
POLISI: HATUNA TAARIFA UTEKWAJI WA MWANDISHI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kupitia kamanda Mussa Taibu limesema halina taarifa za kutekwa kwa mwandishi wa habari nchini Tanzania, Bollen Ngeti, ambaye inadaiwa kuwa ametekwa leo na watu wasiojulikana eneo la Msasani, DSM.
=======
UPDATES
Kwa mujibu wa mke wa Bollen Ngeti, mumewe alimfahamisha kuwa amekamatwa akiwa maeneo ya Banana jijini Dar na alikuwa anahofia usalama wake
> Bollen alimtaka mkewe awafahamishe watu haraka na alihisi ni katika sakata la Tito Magoti
#JFLeo #FreeBollenNgeti #FreeTitoMagoti
Zaidi soma:
Dar: Mwandishi wa habari Bollen Ngetti akamatwa na Polisi, apelekwa Sitakishari
Mwandishi wa Habari za Uchunguzi Bollen Ngetti, Bollen Ngetti, amekamatwa jioni hii na askari 3, na kupelekwa kituo cha Polisi Stakshari. Ijumaa, Bollen Ngeti alihamishiwa katika kituo cha Polisi Buguruni, Dar es Salaam akituhumiwa kumtukana mke wake. Bollen anasemekana kuwa na Diploma ya...
www.jamiiforums.com
Bollen Ngetti: Utawala wa Rais Magufuli na hatima ya CCM
TUMEFIKA mahali ambapo tuweke kando itikadi ya vyama, dini na ubaguzi mwingine wowote tujadili na kutafakari kwa pamoja hatima ya nchi yetu na watu wake! Jamii inayojadiliana masuala ya Taifa ndiyo inaitwa jamii hai. Kinyume na hapo hiyo ni jamii mfu! Tunahitaji watu wa kada zote kujitokeza...
www.jamiiforums.com
Bollen Ngetti CCM maarufu kwa kuikosoa Serikali na chama chake mitandaoni anusurika kifo baada ya gari lake kugongwa na gari lililokuwa likiwafuatilia
Bollen Ngetti ambaye Ni mwana CCM maarufu kwa kuikosoa serikali na chama chake mitandaoni amenusulika kifo baada ya gari lake kugongwa na gari iliyokuwa ikiwafatilia na kutokomea kusikojulikana!
www.jamiiforums.com
Bollen Ngetti: Dk. Bashiru, Membe si size yako, kaa kimya
SHIKAMOO Mwalimu Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM. Nina hakika una afya njema hapa Lumumba ukiwa juu ya kiti chako cheusi cha kuzunguka zunguka ukipitia mafaeli mbalimbali ya kiutendaji. Naomba umuagize Esther akuletee juisi baridi sana kama haujafunga ukae kwa utulivu mkubwa kusoma waraka huu...
www.jamiiforums.com