Dar inawapotezea watu muda

Dar inawapotezea watu muda

Ushasema kilimo alafu unauliza biashara gani tena...sasa huyo anayelima kisasa ndani ya miezi sita ana uwezo wa kununua gari au kujenga nyumba na ikaisha...je biashara gan kwa wew apo dar unayoweza kuifanya ndani ya miez sita na ukanunua gari la maana na kuanzisha ujenz. Dar ni sawa na mtu mfupi anaetembea hatua fupi fupi nyingi alafu anakuja kupitwa na mtu mrefu anaetembea hatua moja ambayo ni sawa na mbili au zaid za mtu mfupi
Hawa watu huku huku mkoani ukiwaambia kuna watu kila mwezi wanaingiza hadi milioni100 na zaid watabisha,halafu kwa formula ya kawaida kabisa,tena elimu ya kawaida tu...sasa niambie dar unapiga deal gani ambayo unaingiza zaidi ya hela hiyo...
 
Kulima kisasa.?

Usiingie huko manake najua vilimo vyote nchi nzima nje ndani.

Wanaofaidika na kilimo sio mkulima.

Na wakulima wa kisasa wakubwa wengi hawaishi mikoani.
We muongo labda kama ni kigoma huko ambako sikujui
 
Hapana mengine ni ya kwako. Nikipita tandika , kigogo na mwansnyamala
Dar
Dar is complecated. Sii rahisi kama unavoandika hapa.
Dar kulala tajiri na kuamka maskini ni rahisi sana.
Kwa deal...maana sio uhakika
 
Mjini chuo kikuu, hata kama huna elimu changamoto zitakuelimisha tu
 
Wala Dar haijawapotezea muda,hapa mlikuja kusoma mlipofaulu mkarudi mkoani kupambana.Kama mlifikiri mikoani kuna maendeleo Kwa nn hamkufanikiwa kabla hamjaja Dar????
 
Mkoani kama huna pesa ni vigumu mno kupata pesa, tofauti na dar.

Kuipta 10000 tu mkoa ni kazi mno tofauti ukiwa hapa mjini aiseeh.

Yote kwa yote kila mtu ana jinsi yake aaminiavyo atatoboa. Mjini si kila mtu katoboa kuna wanaokwama na wanaofanikiwa ni bongo yako tu jinsi gni unaichemsha.
na ukiipata hiyo 10,000 inafanya kitu kikubwa kuliko Dar...
 
Ukiegemea kwenye hesabu za probability, uwezekano wa kutoboa ukiwa Dar ni mkubwa kuliko mkoani. Magari na majumba mazuri yako Dar. Mkoani mtu anayetembelea shangingi ni mkuu wa mkoa pekee, whats ur chance of getting one?
We unamiliki hata kimoja wapo
 
Dar ndo makao makuu ya mashirika mengi ya serikali
Makao makuu ya mashirika ya binafsi
Makao makuu ya balozi mbalimbali
Mji mkuu wa kibiashara
Ukitumia fursa za hapa utafanikiwa kirahisi sana
 
Hahah ila mi naona Dar nzuri kwa biashara kuliko ajira ila uwe umeinvest pesa ndefu. Sio biashara za kuchonga miwa na kuuza pipi.
Kwa ajira ukipata unayokunja at least 2 to 3m kama take home ndio utainjoy life la mjini. Ila kinyume na hapo ni shida tu mzee baba!
Hizo ajira za take home 2 au 3m kuzipata mkoani ngumu so lazma ukomae hapa Dar
 
Sijui mnaongelea mafanikio gani ,BTW ukitembelea maeneo mengi ya makazi Dar nyumba nyingi nzuri za kisasa zinajengwa/zimejengwa/zinamilikiwa na watu ambao wengi wao hawana hata miaka 5 toka waingie Dar. Nadhani ni kujipanga na kuzingatia plan yako tu.
 
Huu uzi ushapoteza maana kwasababu watu WANATAMBIANA tu!hakuna mtu anakubali kuelewa kua KILICHOKUSHINDA WEWE KWA MWENZIO KINAWEZA KUA NDANI YA UWEZO WAKE.mliopo mkoa kama hujaona umaana wa kukaa dar bhas kuwa muelewa kwa sababu tofauti na mwenzio hajaona umaana wa kukaa mkoa.Kila sehemu kuna fursa zake na kukazania kua sehemu fulani tu ndo kunamafanikio ni mawazo mgando.
 
Acha zako mkuu usitufanye mazuzu humu mimi nimekaa Dar miaka mingi , Tandale zile ni nyumba au slums we jamaa muongo sana , mitaa michafu , plan ya ovyo kabisa na kwa taarifa yako Dar es Salaam maeneo yaliyo staarabika ni machache mno mengi yapo nje ya mji asilimia 70 ya wakazi wa Dar wanaishi kwenye slums halafu nao wanatunisha mabega eti mi wa Dar , nonsense kabisa mwambie akuoneshe anapokaa sasa .......ptuuu

Nyie watu ni arrogant sana ila wengi wenu mnaishi maisha ya taabu sana
Mkuu huo mkoa uliopo watu wote wanaishi kwenye "apatimenti" au nyumba za kisasa pekee??kwa ujuzi mdogo nilionao hakuna mkoa ambao hauna hzo slums unazosema.....na mtu akiwa anaishi slums za dar akitunisha mabega aseme yuko??hahaah
 
Wauza mayai hao , we unaishi kwa mfuga mbwa halafu unajifananisha na wa mkoani , shenzi sana hawa
Mjomba awamu hii ukija kufunga mzigo tena utafikia gesti mana ukijaga dar unanisifu kua nimejiongeza mpaka ukiwa na shida mjini unapata kwa kufikia alafu jf unanichana makavu hivi kweli
 
Inategemea vip na shughuli zako sasa kama utashindwa kutafuta ridhiki kwenye watu milioni5 utaweza kutafuta pesa kwenye watu laki 5? Shughuli nyingi inategemeana na watu na uku ukiwa umejipanga vipi kimaisha.....kama income yako ndogo na matumizi makubwa sana lazima itakukost na hii ipo kwa wengi hasa wapend starehe a.k.a BATA
 
Back
Top Bottom