Dar inawapotezea watu muda

Dar inawapotezea watu muda

Nilikaa miaka miwili na nusu mikoani lakini sikuwahi ona jambo la maana hela zenyewe hakuna, yani watu hawanywi hata soda aisee na wakinywa soda ni kwenye sherehe aisee, tangu nirudi Daslama nateleza tu kama maji...
 
Mkoani kama huna pesa ni vigumu mno kupata pesa, tofauti na dar.

Kuipta 10000 tu mkoa ni kazi mno tofauti ukiwa hapa mjini aiseeh.

Yote kwa yote kila mtu ana jinsi yake aaminiavyo atatoboa. Mjini si kila mtu katoboa kuna wanaokwama na wanaofanikiwa ni bongo yako tu jinsi gni unaichemsha.
Hiyo elfu kumi dar unaipataje kirahisi?
 
Hio ni wewe na mipangilio yako. Mimi naondoka saa mbili asubuhi saa tatu kasoro niko kibaruani. Kurudi hivyo hivyo 45mins tu.
inategemea na mahali unapokaa kuna watu wanachukua masaa hata matatu kwenye foleni... Dar kero tupu
 
Nani kakudanganya wewe hivi ulishafika kwanza Mwanza au unasikiliza story za vijiweni wewe , halafu unajifanya mjanja na swali langu hujajibu nimwkwambia nionyeshe maeneo ya jiji la mwanza yaliyo ovyo kama ya Dar umeshindwa


Na kwa taarifa yako Mwanza hayo mapanki unayoyasema hayaliwi na binadamu acha ushamba vitu vingine uwe unauliza ,hayo mapanki ni chakula cha mifugo
Mwanza inasifika kwa kitoweo safi cha samaki wa Sato na Sangara sisi hatuli takataka kama mnazokula nyie wa Dar , mnakula vibua na vitu vya ajabu ajabu halafu mnaita samaki

Mwanza life ni cheap sana kwa kila kitu kuanzia malazi , usafiri na chakula

Karibu sana mkuu hutajutia kuishi Rock City , ukiwa mchapa kazi tu probability ya kutoboa ni kubwa sana
Katika utafito wa NBS Mwanza ni moja ya mikoa yenye maisha ya dhiki kwa wakazi wake hapa nchini.
 
Jibu langu lilianza na 'hio ni wewe' maana yangu yeye ndio anaamka saa kumi alfajiri sio wote
inategemea na mahali unapokaa kuna watu wanachukua masaa hata matatu kwenye foleni... Dar kero tupu
 
Penye watu wengi kuna fursa,pesa na matumizi mengi ya pesa. Katika maeneo haya watu wengi hishindana kuona na kuanzisha fursa ili kuendana mtindo wa maisha wa eneo hilo. Wengi wanaotoka nje ya dar hushangaa jinsi vijana wa dar wanaopanga kweny nyumba nzuri ambazo mkoani ni za viongozi na taasisi. Huishia kushangaa acces ya nguo nzuri kwa bei nzuri na vitu vingine vizuri. Kuishi dar unapaswa kuwa mbunifu, mchapakazi na jasiri. Wanaokimbia dar lazima watatunga vijisababu ili kujifariji kwa kushindwa kwao. Kuishi dar tu ukawa na uwezo wa kulipia bills za maisha sio kazi rahisi. Ndo maana tukirudi mikoani tunaheshimika kuliko nyinyi mliorudi na kunyoosha mikono mmeshindwa.
siku hizi heshima pesa.... we rudi mkoani huna pesa uone kama kuna mtu atakuwa na time na wewe
 
U
Nimeishi Dar kwa takribani miaka 13,hakuna cha maana nilichokifanya,ila niliporudi mkoani ndani ya mwaka mmoja maisha yalikuwa tofauti kabisa. Niliacha kufikiria mawazo ya muda mfupi mfano nitakula nini kesho,kodi itakuaje na mengineyo ya kipuuzi..

Sasa hivi nawaza itakuaje baada ya mwaka au miaka kumi nitakuwa wapi. Hilo Dar linaishia kwenye maneno tu,maisha ya Dar yanamfanya mtu awe mtumwa,wana wengi wanaogopa kurudi mahome kwao kwa kuhisi watadharaulika.

Acha fikra potovu rudi ubadili namna ya kufikiri,huku mambo yanaenda ukitia nia.
Sitake kufanana na wengine mkuu.Wewe umemudu hayo maisha kutokana na aina ya shughuli unayofanya,pia bila shaka huko ulikuwa na vitu vingi ulivyosaidiwa na ndugu au wazazi.Kama ni biashara Dsm inashawishi zaidi kuliko mikoani maana wateja ni wengi zaidi na ongezeko la faida ni la haraka.
 
Dar kinachokera ni foleni na lile joto..Yaani muda wote akili iko juu juu tu huna muda wa kurelax...
Pole mkuu, joto kali ni kuanzia December, ila miezi hii na kurudi hadi wa sita hali sio mbaya. Foleni ni sifa ya jiji lolote kubwa si London,si New York....labda ukae huko huko mikoani na vijijini. Ku-relax ni mipangilio yako tu.
 
Nani kakudanganya wewe hivi ulishafika kwanza Mwanza au unasikiliza story za vijiweni wewe , halafu unajifanya mjanja na swali langu hujajibu nimwkwambia nionyeshe maeneo ya jiji la mwanza yaliyo ovyo kama ya Dar umeshindwa


Na kwa taarifa yako Mwanza hayo mapanki unayoyasema hayaliwi na binadamu acha ushamba vitu vingine uwe unauliza ,hayo mapanki ni chakula cha mifugo
Mwanza inasifika kwa kitoweo safi cha samaki wa Sato na Sangara sisi hatuli takataka kama mnazokula nyie wa Dar , mnakula vibua na vitu vya ajabu ajabu halafu mnaita samaki

Mwanza life ni cheap sana kwa kila kitu kuanzia malazi , usafiri na chakula

Karibu sana mkuu hutajutia kuishi Rock City , ukiwa mchapa kazi tu probability ya kutoboa ni kubwa sana
Mwanza nalo ni jiji kwani? Umeshajibiwa Kwa takwimu za NBS Mwanza wanaishi Kwa maisha ya dhiki hata Pato lake ni dogo ukilinganisha na Dar
 
Man kupanga sio tatizo wala kukaa kwa shem wako sio tatizo....tatizo ni wew kumcheka na kumponda mwenye kajumba kadogo wakati ni ya kwake na amejenga kwa jasho lake. Unaambiwa bachela hutakiwi kuchangia chochote kweny mkutano wa wenye ndoa zao. Ivo ivo pia...mwenye gari la kuazima hana sauti anapokutana na wenzake wanaomiliki pikipik zao
Tatizo ni huyo mwenye kajumba anaposema mwenzie kapanga na maisha ye katoboa.Tena anaanzisha na thread kuwa watu waache kupanga waende kuishi kama yeye anavyoona inafaa. By the way kati ya vipofu mwenye chongo huonekana mfalme
 
Man kupanga sio tatizo wala kukaa kwa shem wako sio tatizo....tatizo ni wew kumcheka na kumponda mwenye kajumba kadogo wakati ni ya kwake na amejenga kwa jasho lake. Unaambiwa bachela hutakiwi kuchangia chochote kweny mkutano wa wenye ndoa zao. Ivo ivo pia...mwenye gari la kuazima hana sauti anapokutana na wenzake wanaomiliki pikipik zao
Tatizo watu mmekariri maisha
 
Kumbe wengi sasa hivi mmeshajua hii kitu...Dsm unaweza ishi miaka mingi lkn usiwe na mafaniko hata kidogo!
Popote pale waweza ishi miaka nenda rudi na usiwe na mafanikio hata kidogo.Kuna sehemu Kijiji kizima wameshindwa kujenga choo cha zahanati.
 
Back
Top Bottom