Dar es salaam inachanganya sana

Dar es salaam inachanganya sana

Ni City Centre, sio posta.
Ujuwaji mwingi kumbe hakuna ulijuwalo.

City center ni Posta, kinachofuata ni mtaa gani upo au kata gani, kuna Kivukoni, Kisutu na Mchafukoge, hizi kata tatu ndio kata za mjini kati.

Mfano nimeona Cape town South Africa route za metro bus zao kutoka sehemu zote kwenda City center wanapaita Cape town, hata vimin bus vyao vikitoka mashinani kwenda City center wanatangaza Cape Town.

Kwahiyo mtu akitoka Kimara kwenda Posta akikwambia nakwenda Dar yuko sahihi kwa mtu aliyetembeatembea duniani huo ndio mfumo unaotumika.
 
Nilikuwa LA mwaka jana,ni rahisi kutembea na kukata mitaa kwenye nchi za magharibi kuliko nchi zetu za Africa....prove me wrong
Kuendesha gari ndio rahisi zaidi, otherwise hakuna foreigner angeweza kuendesha gari New York.

Gps inakupeleka mpaka unapotaka kufika.
 
Nyamwezi na kipata

Kibambawe na jangwani

Congo na matumbi,

Upanga Alykhn road

Ila Upanga kumetulia wazee nimefikia kwa shemeji
 
Hivi BAMAGA ni Mwenge Au Sinza!?

HONGERA BAR ni Sinza Au Kijitonyama?

Chuo Cha Ustawi Ni Sinza Au K'ijitoNyama?

ITV Iko Mikocheni Au Mwenge?

COCO BEACH Iko Masaki Au Osterbay?

MLIMANI CITY Iko Ubungo Au?

SAYANSI Iko Kijitonyama Sasa Kwanini ROSE GARDEN Ni Mikocheni?

Clouds FM Ni Mikocheni Aaaf Kwanini EFM Ni Kawe !?

Hii Mipaka Ikoje Ikoje!?
Miaka ya zamani hiyo kitu isingekupa shida,kulikuwa hakuna daladala wala bodaboda na hata gari binafsi zilikuwa za kuhesabika,watu walikuwa wanatembea zaidi,mitaa na mipaka ulikuwa unaijua kichwani lakini kwa sasa sio rahisi sana....
 
Ujuwaji mwingi kumbe hakuna ulijuwalo.

City center ni Posta, kinachofuata ni mtaa gani upo au kata gani, kuna Kivukoni, Kisutu na Mchafukoge, hizi kata tatu ndio kata za mjini kati.

Mfano nimeona Cape town South Africa route za metro bus zao kutoka sehemu zote kwenda City center wanapaita Cape town, hata vimin bus vyao vikitoka mashinani kwenda City center wanatangaza Cape Town.

Kwahiyo mtu akitoka Kimara kwenda Posta akikwambia nakwenda Dar yuko sahihi kwa mtu aliyetembeatembea duniani huo ndio mfumo unaotumika.
Jamaa kapondea wakuja kumbe nae wakuja vile vile 😃
 
Jamaa kapondea wakuja kumbe nae wakuja vile vile 😃
Hajui lolote, kijiwe cha watoto wa mjini kitambo hiyo ni Posta Salamanda corner, Mtaa wa Samora avenue na Mkwepu street kwa sasa ndio GSM HQ.
 
Kuna mtaa Kariakoo unaitwa Magira, yaan Siku naelekezwa nilishangaa sana, " nenda Magira Street" moyoni nikasema hakuna huo mtaa, kumbe upo kweli
 
Ile mitaa ya kariakoo me ndo inaniacha hoi sijui mtaa wa agrey mara msimbazi mara uhuru jangwan mtaa wa kongo mtaa wa swahili yaan iyo mitaa sijuinmipaka yake ni ipi
Mitaa ya Kariakoo ni kizungumkuti kabisa. Ila ndio burudani ya Darsalam.
 
Acha kujidanganya wewe, umeshafika mji Mkongwe Zanzibar?

Vile chochoro vyake vinaitwa msitu wa Zanzibar.

Mtu anayevijuwa vichochoro vile dunia mzima anatobowa.
Sijafika ila kwa experience ya kkoo sidhani kama huo mji mkongwe hivyo vichochoro vyake vinazidi idadi ya mitaa kkoo
 
Mipaka ya hapa inatenganishwa na barabara. Ukiwa unatokea Lugalo barabara ya Coca kuja mpaka Morocco hiyo yote ni Mikocheni, upande wa pili Mwenge inaishia Bamaga ukivuka road unaingia K'nyama mpaka Victoria kama sijakosea. Ukifika junction ya Morocco hapa panaanzia Oysterbay mpaka Redcross upande huu wa kwenda mjini, upande wa pili ni Kinondoni mpaka Selander bridge. Mwai Kibaki road huwa kuna Msaani na Mikocheni pia.

Studio sio Mwananyamala, ni Kino pale mpaka Komakoma, ndiko inakoanzia M'nyamala.
Kituo cha moroko mwendokasi kipo mpakani mwa Mwananyamala na Kinondoni. Vodacom HQ ipo mwananyamala,Tanzanite park ipo mwananyamala,hospitali ya kinondoni dr. Mvungi ipo mwananyamala pia.
 
Back
Top Bottom