Dar es salaam inachanganya sana

Dar es salaam inachanganya sana

Hivi BAMAGA ni Mwenge Au Sinza!?

HONGERA BAR ni Sinza Au Kijitonyama?

Chuo Cha Ustawi Ni Sinza Au K'ijitoNyama?

ITV Iko Mikocheni Au Mwenge?

COCO BEACH Iko Masaki Au Osterbay?

MLIMANI CITY Iko Ubungo Au?

SAYANSI Iko Kijitonyama Sasa Kwanini ROSE GARDEN Ni Mikocheni?

Clouds FM Ni Mikocheni Aaaf Kwanini EFM Ni Kawe !?

Hii Mipaka Ikoje Ikoje!?
1. Bamaga ipo Mtaa wa Mwenge, Kata ya Kijitonyama, Wilaya ya Kinondoni
2. Hongera Bar ipo Mtaa wa Mpakani 'A' Kata ya Kijitonyama
3. Chuo cha Ustawi wa Jamii kipo Mtaa wa Mpakani 'A' Kata ya Kijitonyama
4. ITV ipo Kata ya Mikocheni
5. Kituo cha Sayansi kipo pande zote, Kijitonyama na Mikocheni, ule upande wa Rose Garden ndio Mikocheni
6. Ufukwe wa Coco Beach upo Mtaa wa OysterBay Kata ya Msasani
 
😀😁😄 kuwa mtu wa system haifanyi nijue mitaa yote ya kariakoo me sio winga
Basi utakuwa upo ofisini tu .yule mwamba sio posta sio kariakoo.vichochoro gani havijui.
Huko mansese,mabibo,tandale ndio usiseme.pale difenda linasubiri.
 
Msasani maandazi load Ndio njia gani hiyo mkuu
Basi wewe siyo mwenyeji zamani kulikuwa na mtaa unaitwa mandazi road ulikuwa ni uswahilini unakuta mandazi yanauzwa mtaa wote
 
Hivi BAMAGA ni Mwenge Au Sinza!?

HONGERA BAR ni Sinza Au Kijitonyama?

Chuo Cha Ustawi Ni Sinza Au K'ijitoNyama?

ITV Iko Mikocheni Au Mwenge?

COCO BEACH Iko Masaki Au Osterbay?

MLIMANI CITY Iko Ubungo Au?

SAYANSI Iko Kijitonyama Sasa Kwanini ROSE GARDEN Ni Mikocheni?

Clouds FM Ni Mikocheni Aaaf Kwanini EFM Ni Kawe !?

Hii Mipaka Ikoje Ikoje!?
Oysterbay Police ipo Oysterbay lakini Namanga ipo Msasani 😂😂😂
 
Masaki ipo Kinondoni, Oysterbay ipo Kinondoni, ila utasikia mtu anakwambia siwezi kaa kinondoni nakaa oysterbay upepo unqpovuma 🤣
Na we pia ndo wale wale, tofautisha Kinondoni wilaya na Kinondoni kata.
 
Back
Top Bottom