Dar es salaam inachanganya sana

Dar es salaam inachanganya sana

Masaki ipo Kinondoni, Oysterbay ipo Kinondoni, ila utasikia mtu anakwambia siwezi kaa kinondoni nakaa oysterbay upepo unqpovuma 🤣
Kuna Kinondoni wilaya, Kinondoni jimbo la uchaguzi na Kinondoni kitongoji.
 
Lakini zote zipo chini ya kinondoni wilaya
Watu wakisema wanapokaa, hawasemi wilaya, wanasema kitongoji.

Kwa hivyo naweza kutenganisha kwetu Oysterbay na Kinondoni kwa kusema nakaa Oysterbay, si Kinondoni.

Kwa maana ya kwamba nakaa kitongoji cha Oysterbay, si kitongoji cha Kinondoni.

Hata kama Oysterbay ipo wilaya ya Kinondoni.
 
Ile mitaa ya kariakoo me ndo inaniacha hoi sijui mtaa wa agrey mara msimbazi mara uhuru jangwan mtaa wa kongo mtaa wa swahili yaan iyo mitaa sijuinmipaka yake ni ipi
Utasikia tupo mataa wa sikuku na Agrey hapo ndio utajua kariakooo ina vuruga kichwa
 
Hivi BAMAGA ni Mwenge Au Sinza!?

HONGERA BAR ni Sinza Au Kijitonyama?

Chuo Cha Ustawi Ni Sinza Au K'ijitoNyama?

ITV Iko Mikocheni Au Mwenge?

COCO BEACH Iko Masaki Au Osterbay?

MLIMANI CITY Iko Ubungo Au?

SAYANSI Iko Kijitonyama Sasa Kwanini ROSE GARDEN Ni Mikocheni?

Clouds FM Ni Mikocheni Aaaf Kwanini EFM Ni Kawe !?

Hii Mipaka Ikoje Ikoje!?
Halafu pale TAZARA ni Buguruni...Mandela rd...Nyerere rd...Pugu rd...Tmk....au Vingweta?
 
Ile mitaa ya kariakoo me ndo inaniacha hoi sijui mtaa wa agrey mara msimbazi mara uhuru jangwan mtaa wa kongo mtaa wa swahili yaan iyo mitaa sijuinmipaka yake ni ipi
Ukiielewa mitaa ya kariakoo hakuna kitu utashindwa kuelewa
 
Mipaka ya hapa inatenganishwa na barabara. Ukiwa unatokea Lugalo barabara ya Coca kuja mpaka Morocco hiyo yote ni Mikocheni, upande wa pili Mwenge inaishia Bamaga ukivuka road unaingia K'nyama mpaka Victoria kama sijakosea. Ukifika junction ya Morocco hapa panaanzia Oysterbay mpaka Redcross upande huu wa kwenda mjini, upande wa pili ni Kinondoni mpaka Selander bridge. Mwai Kibaki road huwa kuna Msaani na Mikocheni pia.

Studio sio Mwananyamala, ni Kino pale mpaka Komakoma, ndiko inakoanzia M'nyamala.
 
Watu wanauliza vitu serious wajuaji wanajiona wao ndo wa mjini wanaleta ngebe...
Mm na kuishi kote huko kuna mitaa siijui na kuna maeneo sijawahi fika...
 
Back
Top Bottom