Dakika za mwisho Al-Bashir amebaki peke yake

Dakika za mwisho Al-Bashir amebaki peke yake

The golden

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2018
Posts
1,381
Reaction score
2,586
Kweli dunia hadaa ulimwengu shujaa.

Nimemuona aliyekuwa akiabudiwa kama Mungu hana tena la kufanya zaidi tu ya kuwa mpole kama hua.

Wapambe wake wote hawapo tena. Wapiga vigelegele na mapambio wote wametimua mbio. Al-bashir yuko peke yake hana tena Yale madaraka . Leo anaweza kuwa mfungwa kama wafungwa wengine.

Tunaposherekea sikukuu hii ya pasaka naomba tukio hili la Al-bashir liwe funzo kwetu. Tuishi maisha ya kutenda haki. Madaraka hutoweka kama kivuli ndipo nyakati za aibu na mateso hutamalaki.
 
Nilikua nasoma aljazeera kwamba speaker wa Bunge,mwenyekiti na katibu mkuu wa chama chake,aliyekua naibu raisi,mkuu wa shirika la upelelezi,mkuu wa polisi wote wamewekwa ndani. Wadogo zake wawili ndani, account za fedha bank zote zimekua frozen pia mzee elbashir wako mbioni kumfungulia kesi ya money laundering. Basi nikakumbuka ya nyumbani kwetu Tanzania nikajiambia moyoni ipo siku yaja,,,.
 
Hiyo mbaya sana kila samuel doe ryberia iliwakuta hiyo kitu hatari sana
 
Albashir hayuko pekeyake, ni swala la muda tu, Makamanda wakisha idhibiti hali atakwenda kupumzika uhamishoni.Wengine wata tolewa kafala ila Albashir ataendelea kupeta.
Kwa nini unasema hivyo?
 
Nilikua nasoma aljazeera kwamba speaker wa Bunge,mwenyekiti na katibu mkuu wa chama chake,aliyekua naibu raisi,mkuu wa shirika la upelelezi,mkuu wa polisi wote wamewekwa ndani. Wadogo zake wawili ndani, account za fedha bank zote zimekua frozen pia mzee elbashir wako mbioni kumfungulia kesi ya money laundering. Basi nikakumbuka ya nyumbani kwetu Tanzania nikajiambia moyoni ipo siku yaja,,,.
Tena hapo kwa spika kutupwa gerezani ndiyo patamu haswaa
 
Na hiyo siku sidhani kama iko mbali ingawa vipofu wamejiaminisha tofauti, wanaamini wanaweza kuzuia tsunami kwa mikono.
Kipindi pekee chenye msukumo mkubwa wa hayo kutokea ni nyakati hizi. Mambo hayo hutokea wakati ule utesaji, dhuluma, ubaguzi na upendeleo, ubabe na uvunjifu wa sheria na katiba, sheria mbaya zinapotungwa kwa nia ya kuwaumiza wanaodhaniwa ni wapinzani, vyote vinapotamalaki.

Nadhani hatujawahi kuyashuhudia hayo katika kipindi chochote cha uhai wa taifa letu, isipokuwa wakati huu.
 
Umenikumbusha riwaya pendwa ya KULI 'lakini yana mwisho'
Kweli dunia hadaa ulimwengu shujaa.

Nimemuona aliyekuwa akiabudiwa kama Mungu hana tena la kufanya zaidi tu ya kuwa mpole kama hua.

Wapambe wake wote hawapo tena. Wapiga vigelele na mapambio wote wametimua mbio. Al-bashir yuko peke yake hana tena Yale madaraka . Leo anaweza kuwa mfungwa kama wafungwa wengine.

Tunaposherekea sikukuu hii ya pasaka naomba tukio hili la Al-bashir liwe funzo kwetu. Tuishi maisha ya kutenda haki. Madaraka hutoweka kama kivuli ndipo nyakati za aibu na mateso hutamalaki.
 
Back
Top Bottom