Dada zetu Tanzania mbona hamuolewi?

Dada zetu Tanzania mbona hamuolewi?

Kuolewa watu wanaolewa sana tu, sema mada haikutakiwa iwe kwa nini wanawake watanzania hawaolewi?? Ilitakiwa aseme kwa nini hawa bongo movie hawaolewi na wabongo flavor?

Kwa sababu ndoa kila leo zipo huku mtaani zinafungwa, kwa hiyo ukisema wanawake watanzania kwa nini hawaolewi inaleta utata kidogo.
Sio kwa wanawake watanzania wote
 
Na suala la kutokuolewa kwa wanawake kunawasumbua wanaume kuliko hata wanawake wenyewe.
Kwa sababu wanaume hata miaka 50 anaoa ila mwanamke miaka 50 nani wakukuoa?
 
Ni kweli ila kwahiyo akisema hatuolewi wote ajue haiwezekani wote tuolewe wengine inatosha kuwa nyumba ndogo za watu
Hapo ndipo naposema mbadirike na wanawake mnapenda sana nyumba ndogo kwa nini?
 
Wacha kututoa kwenye reli sie bwana, ngoja kwanza ACT wamalize kuongea halafu nikujibu, lkn una uhakika wadada hawaolewi?Mbona jumamosi panakuwaga na harusi nyingi hivyo mtaani ama ni wanaume kwa wanaume wanaoana?Sema hivi hao bongo muvi kwann hawaolewa na mabwana zao wanaogiza nao au kuimba nao, tuwache sie
Hahhaa haya mkuu
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. Labda mtaani kwao haoni hizo shamra shamra za ndoa
Mnazoziona ni chache sana wanawake wengi sana wanadanga tunawaona
 
Watanzania acheni unafiki wameoa hao mnaanza bango.. ina maana hao dada zenu wanaolewa nje ya nchi hamuwaoni mmeona hao wanaume wawatatu walioa jirani shame on you.

Kwanini hamuoni hao wote wanaolewa na wazungu, kenya uganda na nchi za mbali? acheni unafiki kabisa mbona mimi nimeolewa na foreigner na naona kawaida tuu
Nyie mpo wengi na umri nao wengi wenu unawatupa mkono hatupendi mkae hivi hivi msubirie kuzeeka
 
Miss Madeko
Simba kula mtu sio habari ila mtu kula Simba ni habari. Walishazoea dada zao ndo wanaolewa na foreigners sasa upepo umebadilika kidogo tu imeshakua habari. Kuna ile story ya kipofu kufunguliwa macho akaona mwezi basi kila kitu kwake yeye kinafanana na mwezi. Ndo hali waliyo nayo kaka zetu sasa hivi.
Ukweli lazima tuuzungumze coz tunawapenda sana
 
Hivi hiyo instergram imeanza lini hadi mtu azeekee huko? Na ni wanawake tu ndio wanaopost upuuzi mitandaoni? Hadi ukawafollow na kugundua wanapost upuuzi mitandaoni na unaendelea kuwafollow wewe inakuweka ktk nafasi ipi?

Acheni kukuz mambo.
Kwa mwanamke kuwa na tabia Mbaya na kujifananisha na mwanaume haijakaa poa kiafrica yani
 
Back
Top Bottom