Dada yake MBOWE aikacha CHADEMA ajiunga na CCM!!

Dada yake MBOWE aikacha CHADEMA ajiunga na CCM!!

Kwa hiyo hii nayo inageukaje kua habari? who is she anyway
 
huyu kafuata maslahi binafsi kwani CDM alikuwa kiongozi au mwanachama tu?pia ikumbukwe kuhama ndio demokrasia kama makongoro Nyerere alivyohamia NCCR hahivyo chunguzeni kwanza inawezekana kapata buzi na masharti lazima aingie ccm.teh teh
 
Mbona ilo jambo ni la kawaida sana Makongoro Nyerere alikuwa Mbunge wa upinzani wakati baba yake akiwa CCM na nguvu zote, sasa ukoo wa Nyerere kuna wabunge wawili wa Upinzani mbona hamsemi. Haya mtoto wa Wasira yuko Chadema mbona hapo hamsemi, mke wake wa zamani wa Dr Slaa alikuwa diwani wa CCM japo sasa kafunguka ni mbunge wa Chadema, Mzee Masha kule mwanza aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema lakini mtoto wake Laurence Masha mnamjua wote. Mifano ni mingi na si kitu cha kushanganza au mke kuwa chama fulani na mme kuwa na chama fulani. Ni sawa kuwa Yanga na mke kuwa Simba au kuwa Man U na watoto wakawa Arsenal

Jamani mbona ni haki yake kikatiba? MMesahau Makongoro aliwahi kuwa upinzani wakati Mwl. Nyerere (Baba mzazi akiwa CCM), tunalikuza saana hili jambo, ila inaleta picha kuwa kweli CCM mnaigopa CHADEMA. Hivi mnataka kutuaminisha kuwa ukoo woote wa Dr. Slaa wako CHADEMA? au ukoo wa Mh. Nyerere wote wako CCM? suala la kuingia chama chochote ni utashi wa mtu, hivyo Grace ameamua tumtakie mema huko alikoenda
 
Grace ugomvi binafsi kaleta hadi nje toka kwenye familia ? Lakini sawa maana hata Makongoro alikuwa NCCR , Wassira , Guninita , hapa la kushangaa ni kitu gani ? Uhuru huo .Na labda kasha vuta mwache tu
 
Tetesi za Huyu dada si nasikia kuwa naye ni miongoni mwa wauza unga na alionywa mara kadhaa kujishughulisha na hiyo biashara ya kuuza unga ila akakataa ushauri ndipo mtafaruku na yeye kuijbaragua kuondoka!!!!!!!
 
Hao magavana ndo walioiba pesa zetu kwa manufaa yao bnafsi,wamesahau nn Tz wanataka tena warudi kuchota mali zetu,wafie mbele hawatoiona ikulu mikonon mwa cDM kamwe.

Mbona hamkuwafikisha mahakamani, Kama serikali yenu ni makini?
 
Huyu dada/mama amegusia pale pale wengi wetu tunapopaona kua katika sera CCM bado ni safi na CDM ni wanaharakati tu wasio na uzoefu wowote wa kuongoza dola huku wakipita huku na huko kudanganya tui watz...

CDM imekua ghafla na bila ya kujitayarisha kisawa sawa kwenye demokrasia ya ndani na maslahi binafsi ya kiuongozi.. ni chama kidogo lakini kutokana na kukua kwa umaarufu wake maradufu ndani ya miaka kama mi5 hivi kimejikuta overwhelmed with its own success na kuonyesha nyufa zote za chama kikongwe...

katika uchambuzi yakinifu, CDM ina hatari ya kuzorota na kufa kabisa kama itashindwa uchaguzi wa 2015 kwa % nyingi na CCM. kama nilivyoonyesha hapo juu licha ya umaarufu kushindwa kwa kishindo kutaifanya CDM na safu yake ya uongozi "kuangalia wapi walikosea na nani anahusika na makosa hayo" yaliyosababisha kushindwa vibaya wakati wakiwa na imani ya kua umma mkubwa wa watz upo nao (nikimaanisha umma mkubwa not necessarily wapiga kura), kutokana na hulka ya ubinafsi ya wanasiasa waliopata mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi "wafanya makosa watakataa kuwajibika" na hapo mgogoro mkubwa wa kiuongozi utauikumba CDM na kutishia uhai wake.

ukitilia maanani kua umoja miongoni mwa viongozi muhimu wa kitaifa wa CDM umeshikiliwa na imani 2 ya kua 2015 kuna uwezekano mkubwa wa kushika dola. kushindwa kwa CDM kutakua mwisho wa umoja na mshikamano baridi huu wa hawa viongozi na wengi wao kuanza kujiuliza maswali ya kubadilisha dira yote, mipango na taswira ya chama kupata nguvu mpya ya kisiasa. Mabadiliko mara nyingi hutishia watu wenye maslahi yao na hapo hali haitokua shwari kwa CDM.

CDM lazima washinde uchaguzi wa 2015 ili iendelee kuwepo, au watone down ambitions zao na waelekeze nguvu kwenye kujenga sustainable opposition kwa kuongeza namba ya wabunge, wavutie zaidi viongozi na vijana toka vyama vingine hususan toka CCM, otherwise mwisho wa CDM kama chama kikubwa cha upinzani ni 2015.
 
Mkuu, hayo ni maandalizi ya ukoo wa akina Mbowe kuhamia CCM. Kuelekea 2015 tutashuhudia mambo mengi na wengi watabaki midomo wazi

ni Kweli mtashudia mengi, Kama CCM kuachia nchi, chaddema kwenda ikulu, CCM ikizikwa rasmi, KIKWETE kuhamia kambi ya upinzani ambayo itakua NCCR au vngn baada ya Chaddema kushika dola na baada ya CCM kufa. Jiandae kushuhudia mengi mkuu.
 
wapo walokua wanamfata YESU kwa sababu ya mikate kwa hiyo sishangai pia mana hata Huyu Grace alikuja chaddema kufuata mikate.
 
Dada yake Mbowe kajitambua, ameona haiwezekani akili ndogo iongoze akili kubwa.

Hongera sana Grace Mbowe.

Kama nyumbani wanamkataa Mbowe, kulikoni.
Kwanza ni haki ya kila mtanzania kujiunga/kutojiunga na chama chochote!
Vilevile ni kudhihirisha kwamba CHADEMA si chama cha UKOO kama mlivyokuwa mkijinasibu hapa jukwaani...!
 
Angehama Mbowe, ningesikitika sana. Kumbe dada kaenda kufanya espionage!
 
Kimsingi Chadema ni chama cha kifamilia hilo lipo wazi wala haliitaji PhD kulitambua.

Mmiliki wa Chadema ni Mtei, na Mwenyikiti wa Chadema ni Mbowe, ambaye ni mkwe wa Mtei,

Kuna uwezekano mkubwa wa kimaslahi ndani ya familia ndiyo maana Grace Mbowe, kuamua kuondoka Chadema na kwenda CCM.

Tutasikia mengi pindi Grace Mbowe, atakapofunguka zaidi.
Ritz,
Kama Chadema ni chama cha kifamilia iweje sasa Grace aondoke kwenye familia? Na vipi ule mjadala wa Ridhiwani na madawa ya kulevya umeishia wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom