CWT yapinga walimu kusafiri bure

CWT yapinga walimu kusafiri bure

Hivi walimu waliolengwa kusafiri bure ni wa Kinondoni tu? Je wale wa wilaya zingine za mkoa wa Dar es salaam na hata wa wilaya zingine kwa Tanzania nzima ingekaa vipi? Namuunga mkono Moba, hili lilitamkwa na Makonda kisiasa siasa lakini utekelezaji ungekua mgumu. Jambo ambalo angetakiwa kulifanya ni kukaa na chama cha waaalimu CWT ambao wangeliweka likawa la kitaifa na siyo Kinondoni tu, walimu hawako Kinondoni tu. Hapo Mkonda alikua anajaribu kupanda kupitia migongo ya walimu wa Kinondoni.
Shida ya usafiri wa kwenda na kurudi kwa waalimu wa hapa Dar huwezi kulinganisha na wa mikoa mingine,usafiri wa Dar wa kila siku ni mgumu kulinganisha na sehemu nyingine,pia mikoani waalimu wengi wana nyumba maeneo ya shule au jirani na shule ni tofauti na Dar ,kwa ujumla adha ya usafiri wa Dar huwezi kulinganisha na sehemu yoyote hapa Tanzania,.pia badala ya kuloloma kwenye vyombo vya habari Mkoba angetafuta nafasi ya kuongea na Makonda mwenyewe ,narudia tena kupinga kwa Mkoba hakusaidii kama wenyewe akina Mkoba wamekaa tu sasa na wengine wakae kimya tu kwa kuwa hakuna Mkoba na timu yake hawajashirikishwa,ni wakati sasa akina Mkoba waamuke na waache kufanya kazi kwa mazoea,waalimu wanatabika miaka yote na wao wapo tu maofisini,nakumbuka mwaka jana walitumika kisiasa wao wenyewe si tuliona wakijinadi kumuunga mkono mwanasiasa mmoja,sijui nani aliwatuma.
 
Hapa sasa ndoo nauona uwezo wa watz ni mdogo sana wa kufikiri.Dc makonda kafanya kuliangana na uwezo wake wa kuomba wenye magali.kama mwalim yuko na nauli alipe.tena ameomba kwenye eneo lake . sasa wengine wanataka wapewe na hela walim.kumbe wachangiaji wengine akili yao sawa na watoto.
 
Ni udhalilishaji.

Kwa mini bus zima wajue Fulani mwalimu?

Kwanini hizo fedha za kulipa wamiliki was daladala siswekwe katika a/c za walimu.

Wapewe allowance ya 2000 per day times 20 working days. Ni Kama 40,000 tu.
Ni nani aliyekwambia kuwa wamiliki wa daladala watalipwa pesa ili kuwabeba walimu bure??

Upo kijiji gani mkuu?
 
Mkuu umehoji vema sana kwakweli huu kwanza ni uzalilishaji juu ya kitengu cha walimu Walimu wamevulia mengi sana wana dai stahiki nyingi sana .Lakini niwapi Makonda alifika kwenyeshule akaambiwa walimu hajafika Leo kazini kwa sababu hawana nauli .Nisawa kutafuta sifa husausani ukishasifiwa kwa hili makonda awaombe radhi waalimu .waalimu pamoja na matatizo yote waliyonayo hakuna hata siku moja wameshindwa kuhudhuria kazini kisa nauli.
Akuombe radhi kwani amekulazimisha kupanda bure? Kama hutaki si ulipe nauli tu ticha!!
 

Kwa siku Mwalimu analipa shilingi 1200 kwenda na kurudi kazini, kwa wiki analipa 1,200 X 5 = 6,000, kwa mwezi analipa shilingi 6,000 X 4 = 24,000 (usafiri wa daladala)

Kama Mwalimu huyo anatoka mbali na kilipo kituo cha daladala basi atalipia bodaboda si chini ya shilingi 2,000 kwa siku (kwenda na kurudi) = shilingi 10,000 kwa wiki, = shilingi 40,000 kwa mwezi

Ukijumlisha na nauli ya daladala kwa mwezi unakuta mwalimu huyo analipa nauli ya shilingi (24,000 + 40,000) = shilingi 64,000

Ukiangalia mshahara wake kwa mwezi ni shilingi 400,000

Ukitoa kodi na makato mengine anabaki na take home ya kama shilingi 336,000

akilipa kodi ya nyumba, umeme, maji chakula nk Mwalimu huyo anakuwa na negative income, ndiyo maana wameamua kumpunguzia maumivu kwa ku subsidize nauli
Ni walimu wa levo zote wanalipwa hiyo 400,000?
 
Makonda anazingua ndo ubaya wa fisiem wanaendesha mambo kwa mizuka sijui wanakula vindo
 
Ni walimu wa levo zote wanalipwa hiyo 400,000?


Waliowengi wapo kwenye 500,000 na 300,000 hivyo nimechukulia hiyo kama average, japo wapo wanaopata zaidi ya 500,000, lakini kwa mujibu wa utafiti uliofanyika wakati fulani ilionekana scales zao zina-range hapo
 
Kwa siku Mwalimu analipa shilingi 1200 kwenda na kurudi kazini, kwa wiki analipa 1,200 X 5 = 6,000, kwa mwezi analipa shilingi 6,000 X 4 = 24,000 (usafiri wa daladala)

Kama Mwalimu huyo anatoka mbali na kilipo kituo cha daladala basi atalipia bodaboda si chini ya shilingi 2,000 kwa siku (kwenda na kurudi) = shilingi 10,000 kwa wiki, = shilingi 40,000 kwa mwezi

Ukijumlisha na nauli ya daladala kwa mwezi unakuta mwalimu huyo analipa nauli ya shilingi (24,000 + 40,000) = shilingi 64,000

Ukiangalia mshahara wake kwa mwezi ni shilingi 400,000

Ukitoa kodi na makato mengine anabaki na take home ya kama shilingi 336,000

akilipa kodi ya nyumba, umeme, maji chakula nk Mwalimu huyo anakuwa na negative income, ndiyo maana wameamua kumpunguzia maumivu kwa ku subsidize nauli


Wenye akili wanasema kama umeweza kujua hivyo kwa nini usitafute utaratibu wa kuzipata hizo hela uwawekee pamoja na mishahara yao badala ya kuwataka kutumia vitambulisho kama manamba au watumwa katika nchi yao?
 
Wenye akili wanasema kama umeweza kujua hivyo kwa nini usitafute utaratibu wa kuzipata hizo hela uwawekee pamoja na mishahara yao badala ya kuwataka kutumia vitambulisho kama manamba au watumwa katika nchi yao?

Anyway yote ni mema lakini alichofanya huyo DC, ni moja ya vitu ambavyo ameona vinawezekana kama kianzio, mwingine angeweza kuja na wazo la kuwakopesha walimu wote vyombo vya usafiri, mwingine angekuja na wazo la kujenga nyumba ndani ya maeneo yao ya kazi nk, nk, nk, kwa sasa wadau wengine ikiwemo serikali wanapaswa kuja na mawazo mengine kama suluhu ya kudumu, hili alilolifanya Makonda ni kama kianzio tu kwasababu haijawahi kutokea kiongozi yeyote aliyewahi kufikiria namna ya kuwapunguzia walimu wetu makali ya maisha, hivyo basi tuchukue hilo kama msingi so that others can build on top of it
 
Hata mimi siafiki huy utaratibu wa walimu kusafiri bure kwenye daladala. Huu utatatibu nahofu utawadharirisha walimu. Makondakta na madreva watawapa walimu majina ya ajabu na wanaweza kuwalazimisha wasikae ili wapishe wanaolipia. Siwaamini kabisa mskondakta wa bongo land
 
Hapa sasa ndoo nauona uwezo wa watz ni mdogo sana wa kufikiri.Dc makonda kafanya kuliangana na uwezo wake wa kuomba wenye magali.kama mwalim yuko na nauli alipe.tena ameomba kwenye eneo lake . sasa wengine wanataka wapewe na hela walim.kumbe wachangiaji wengine akili yao sawa na watoto.
Mkuu, jambo hili lipo kisiasa zaidi. Huyo DC ana mkubwa wake ambaye ni RC! Jambo hili nadhani lingepelekwa kwa RC lingekwama. Licha ya kuwadhalilisha walimu wa Dar pia litapunguza malipo ya kodi toka kwa wamiliki wa magari. Halafu haiingii akilini kwa mtoto ambae mzazi wake hana uwezo wa michango anamtafutia nauli ya basi huku mwl anaelipwa mshahara eti anasafiri bure!
 
HIVI HUYU ALIYELETE HOJA YA WALIMU KUSAFIRI BURE ALIKUA ANAWAZA NN MAANA, KAMA NI MSAADA KWA WALIMU NAONA KAMA SERIKALI ITAKUA HAIJATOA MSAADA, KAMA WANAHITAJI KUWASAIDIA BASI WAWALIPE STAHIKI ZAO ZOTE NA MADENI YOTE HALAFU KILA MWALIMU ALIPE NAULI KAMA KAWAIDA ILI KUONGEZA KIPATO CHA TAIFA, LAKIN HII DANGANYA TOTO HAIFAI, MAANA HATA MANUFAA YAKE BADO CJAYAONA KAMA NI KUTAKA WAWAHI KAZINI ILIBIDI WATAFUTIE USAFIRI MAALUM, KAMA NI KUPUNGUZA GHARAMA ZA MAISHA ILITAKIWA WAPEWE MISHAHARA MIZURI, NA WALIPWE MADENI YOYE, KAMA NI MOTIVATION ILI BIDII KUWE NA UTARATIBU MAALUM WA KUTUMI USAFIRI MMOJA KWA WALIMU WOTE........HIVI NI NINI HASA MANTIKI YA HOJA HII NAFIKIRI HII NDIYO KAZI TUU, ILA SI KAZI BORA
Huyu DC anataka sifa. Kama JPM atampromote atatufedhehesha Watz.
 
Nadhani konda ataelewana nao walimu kwakuwa idhini imetoka kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri, labda moja ya mambo ya kuongeza ni kuwa namba za simu za wamiliki wa hayo mabasi ziwe bayana ili kupunguza manyanyaso ya hao makonda
Hivi wamiliki hawakukubali wanafunz kulipa 200/-?Na je hawajui kuwa wanafunz wananyanyaswa na makondakta?
 

Kwa siku Mwalimu analipa shilingi 1200 kwenda na kurudi kazini, kwa wiki analipa 1,200 X 5 = 6,000, kwa mwezi analipa shilingi 6,000 X 4 = 24,000 (usafiri wa daladala)

Kama Mwalimu huyo anatoka mbali na kilipo kituo cha daladala basi atalipia bodaboda si chini ya shilingi 2,000 kwa siku (kwenda na kurudi) = shilingi 10,000 kwa wiki, = shilingi 40,000 kwa mwezi

Ukijumlisha na nauli ya daladala kwa mwezi unakuta mwalimu huyo analipa nauli ya shilingi (24,000 + 40,000) = shilingi 64,000

Ukiangalia mshahara wake kwa mwezi ni shilingi 400,000

Ukitoa kodi na makato mengine anabaki na take home ya kama shilingi 336,000

akilipa kodi ya nyumba, umeme, maji chakula nk Mwalimu huyo anakuwa na negative income, ndiyo maana wameamua kumpunguzia maumivu kwa ku subsidize nauli
Sawa na mtoto je? JPM kaamua kuwapa watoto elimu bure hivo ingekuwa jambo jema kusafiri bure pia!
 
Idara ya Mahakama imeweka mabasi makubwa aina ya TATA,kwa ajili ya watumish,kuna ya route ya Tegeta,Mbezi ya Kimara,Mbagala na kwingineko.Walimu,WAPANDE BURE
 
Sawa na mtoto je? JPM kaamua kuwapa watoto elimu bure hivo ingekuwa jambo jema kusafiri bure pia!


Mwinyi aliasisi mpango wa mabasi ya wanafunzi miaka ya 90 kama sijakosea, nadhani kwa awamu hii lingefufuliwa wazo lile likatekelezwa chini ya udhibiti wa hali ya juu, tungeweza kutatua kabisa shida ya usafiri kwa watoto wetu
 
Labda ubuniwe utaratibu wa kistaarabu kufanikisha hili.
 
Back
Top Bottom