CWT yapinga walimu kusafiri bure

CWT yapinga walimu kusafiri bure

Huku ni kutafuta sifa pasipotakiwa. Huyu dogo hajui aina ya watu anaodeal nao yaani walimu. Anasema tupewe vitambulisho vya kuwaonyesha mako dakta tutabeba vitambulisho vingapi ukizingatia ninacho cha benki, cha kazi na bima ya afya?
Anatusemea kwa tafiti ipi aliyoifanya juu ya walimu kuwahi au kuchelewa kazini? Nimuonye tu, aache kutuchimba kwani tumezivumilia hizi serikali na aina ya viongozi wa aina yake na tupo karibu kupasuka. Aache kutuletea siasa kwani siyo mahali pake.
 
Yeye Mkoba hajui shida za walimu badala ya kushukuru yeye anaanza kulaumu ,nia apate ujiko kuwa alishiriki kufanikisha hilo jambo,huo ni wivu wa kike,jeyeye na chama chake ni kipi wamefanya kusaidia waalimu kuondokana adha ya maisha duni na tabuwanazopata kila siku
Mpuuzi mmoja hivi,
Kwanini mnataka kuwachukulia walimu kama special group?
Huyo DC angekuwa na akili angewapa transport allowance, sio huu upuuzi, wanawageuza walimu ombaomba..
 
Ni discrimination kwa watumishi wa kada moja kutofautishwa ktk unafuu wa gharama za maisha,ninachoona ni walimu kuacha kwenda vijijin na kubaki mijini ili kupata unafuu wa gharama za maisha
 
Na nitoe rai kwa walimu msisubutu kupokea ofa hii maana mtadhalilishwa na makonda mpaka basi, kwanza makonda wakishawashika sura utasikia usisimame hapo hao ndiyo wale wale na mtapewa majina fake ambayo mkiyajua mtakereka mno...Kama ni kuwasaidia wangewatafutia usafiri wenu sema kuanzia saa fulani gari litaanzia ruti sehemu fulani kwenda sehemu fulani na liwe linawapakia ninyi tu...Unless otherwise makonda watawanyanyapaa mno...Siwashauri walimu..
 
HIVI HUYU ALIYELETE HOJA YA WALIMU KUSAFIRI BURE ALIKUA ANAWAZA NN MAANA, KAMA NI MSAADA KWA WALIMU NAONA KAMA SERIKALI ITAKUA HAIJATOA MSAADA, KAMA WANAHITAJI KUWASAIDIA BASI WAWALIPE STAHIKI ZAO ZOTE NA MADENI YOTE HALAFU KILA MWALIMU ALIPE NAULI KAMA KAWAIDA ILI KUONGEZA KIPATO CHA TAIFA, LAKIN HII DANGANYA TOTO HAIFAI, MAANA HATA MANUFAA YAKE BADO CJAYAONA KAMA NI KUTAKA WAWAHI KAZINI ILIBIDI WATAFUTIE USAFIRI MAALUM, KAMA NI KUPUNGUZA GHARAMA ZA MAISHA ILITAKIWA WAPEWE MISHAHARA MIZURI, NA WALIPWE MADENI YOYE, KAMA NI MOTIVATION ILI BIDII KUWE NA UTARATIBU MAALUM WA KUTUMI USAFIRI MMOJA KWA WALIMU WOTE........HIVI NI NINI HASA MANTIKI YA HOJA HII NAFIKIRI HII NDIYO KAZI TUU, ILA SI KAZI BORA


Kwa siku Mwalimu analipa shilingi 1200 kwenda na kurudi kazini, kwa wiki analipa 1,200 X 5 = 6,000, kwa mwezi analipa shilingi 6,000 X 4 = 24,000 (usafiri wa daladala)

Kama Mwalimu huyo anatoka mbali na kilipo kituo cha daladala basi atalipia bodaboda si chini ya shilingi 2,000 kwa siku (kwenda na kurudi) = shilingi 10,000 kwa wiki, = shilingi 40,000 kwa mwezi

Ukijumlisha na nauli ya daladala kwa mwezi unakuta mwalimu huyo analipa nauli ya shilingi (24,000 + 40,000) = shilingi 64,000

Ukiangalia mshahara wake kwa mwezi ni shilingi 400,000

Ukitoa kodi na makato mengine anabaki na take home ya kama shilingi 336,000

akilipa kodi ya nyumba, umeme, maji chakula nk Mwalimu huyo anakuwa na negative income, ndiyo maana wameamua kumpunguzia maumivu kwa ku subsidize nauli
 
Yeye Mkoba hajui shida za walimu badala ya kushukuru yeye anaanza kulaumu ,nia apate ujiko kuwa alishiriki kufanikisha hilo jambo,huo ni wivu wa kike,jeyeye na chama chake ni kipi wamefanya kusaidia waalimu kuondokana adha ya maisha duni na tabuwanazopata kila siku

Hivi walimu waliolengwa kusafiri bure ni wa Kinondoni tu? Je wale wa wilaya zingine za mkoa wa Dar es salaam na hata wa wilaya zingine kwa Tanzania nzima ingekaa vipi? Namuunga mkono Moba, hili lilitamkwa na Makonda kisiasa siasa lakini utekelezaji ungekua mgumu. Jambo ambalo angetakiwa kulifanya ni kukaa na chama cha waaalimu CWT ambao wangeliweka likawa la kitaifa na siyo Kinondoni tu, walimu hawako Kinondoni tu. Hapo Mkonda alikua anajaribu kupanda kupitia migongo ya walimu wa Kinondoni.
 
mm nashindwa kuelewa watu bado wapo na siasa,siasa imekwisha tunataka mabadiliko tuliokuwa tunaimba kwenye kampeni.Mabadilko ndio hayo yanaanza mkuu wa kinondoni kuamuru walimu kupanda daladala bure ni jambo bora linapaswa kuungwa mkono na kufurahiwa na walimu kwani huo ndio mwanzo tu wa mabadiliko kwa walimu hapa Tanzania,tuache tabia ya kubeza hata kama kitu kinamanufaa kwetu.ndio maana nasema bado tupo na siasa zaidi baada ya kufanya kazi na kupongezwa yanayofanwa na serikali ya awamu 5.
 
Mwenyekiti wa chama cha walimu Tanzania G. Mkoba amesema haoni kama ni sahihi kwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni kuingia kwenye makubaliano na wenye mabasi ya daladala ya kuwasafirisha walimu bure bila kuwashirikisha walimu wenyewe, hivyo ameshauri kuwa ni vizuri mambo yanayowahusu waalimu yakawa yanawashirikisha walimu.

Chanzo: Clouds tv

Mkoba wewe umefanya nini kuwasaidia walimu kwa miaka yote ukiwa kiongozi, ukimwona nduguyo anateseka ukamsaidia, atakushukuru, na kama wewe huna huna msaada usimwonee wivu mwenzako aliyetoa msaada anapo pongezwa

Ningekuona Mkoba unabusara kama ungetazama jambo jingine nawe ukafanya kuwapunguzia walimu hao ukali wa maisha badala ya kuwa unaneemeka kwa michango yao miaka nenda rudi
 
Huyo atakayesafiri bure unadhan Konda ataelewana nae mdau???

Nadhani konda ataelewana nao walimu kwakuwa idhini imetoka kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri, labda moja ya mambo ya kuongeza ni kuwa namba za simu za wamiliki wa hayo mabasi ziwe bayana ili kupunguza manyanyaso ya hao makonda
 
Yeye Mkoba hajui shida za walimu badala ya kushukuru yeye anaanza kulaumu ,nia apate ujiko kuwa alishiriki kufanikisha hilo jambo,huo ni wivu wa kike,jeyeye na chama chake ni kipi wamefanya kusaidia waalimu kuondokana adha ya maisha duni na tabuwanazopata kila siku

Kwa nini hii issue ya waalimu inaangaliwa kwa jicho la kipekee as if waalimu ndiyo wafanyakazi pekee wanaopata shida ya usafiri Dar es Salaam.tukiendelea na namna hii hawa waalimu watatusumbua sana huku mbele ya safari. Kama shida ya usafiri ipo kwa wafanyakazi wote tatizo liangaliwe kwa upana wake no matter how long it might take.... i a m afraid to say hizi ni hatua za zima moto tu, mpango huu hautatekelezeka
 
Weye NgoniDema na Watu wengi wenye fikra Kama zako .Mnaonyesha Chuki na WIVU mliokuwanao dhidi ya DC Makonda. Huyu DC Makonda ni mzalendo ambaye anajali watu wa Kinondoni. Kaangalieni alivyo ibadilisha Kinondoni.kuhusu Ardhi,Ajira kwa vijana na kujenga shule kwa misaada ya wananchi.

Weye NgonoDema na wafuasi wako au(The HATERS) mmefanya nini ktk jamii zetu???????????
Nimefanya makubwa na nitaendelea kufanya, Mkuu tofautisha Maneno na vitendo, hata ww unaonekana ni mtu wa bra bra nying vitendo ovyo kama makonda a.k.a Misifa, wilaya yake ndo chimbuko la kipindpindu Tanzania, lakin kwasababu akil zenu ziko sawa Ndo mana unamsifia
 
Maoni yangu ni kwamba suluhisho la kudumu ni kuwajengea nyumba kwenye maeneo ya shule wanazofundisha ili waishi karibu na shule. Ikiwa walimu wa Dar es Salaam wanapewa incentive hiyo hali ni vipi kwa walimu wa mikoa mingine? hii haiwezi kuleta dhana ya kibaguzi?
 
Shida ya walimu siyo kupanda daladala bure bali ni kuboreshewa maslahi yao. Hakuna hata siku moja wal;imu waliomba kupanda daladala bure. Hata hivyo kutokana na uwingi wa walimu hawawezi kupanda bure, watakaopanda labda ni wachache sana. Lakini kingine ni kutaka kuwadhalilisha kwa makonda ili wapate stress na kushindwa kufundisha siku hiyo (siku ambayo umegombana na konda tena mbele ya mwanafunzi wako)
 
Kusafiri bure sio tatizo,tatizo linakuja pale:-

1.Ubure huo kuegemea walimu wa Dar pekee.(ubaguzi kwa walimu wa sehemu nyingine).
2.Ujenzi wa nyumba za walimu unapokuwa sio suala muhimu la kujadili.
3.Namna ya kuwabaini walimu halisi na wale bandia watakaotumia bure hiyo.(hakuna sare za walimu).
4.Bure inapokuwa ni ya kutangaza hadharani,badala ya kutumia angalau faragha fulani
miongoni mwa wadau,(wafanye kama walivyofanya kwa wengine wasiolipa nauli).
5.Utafiti wa kuwabaini ni walimu wangapi wanaishi wapi? na kwanini hawaishi karibu na shule
wanazofundisha?
6.Utakapoongeza walimu kuzurura zurura,kwani tayari watakuwa na nauli za ziada.
register book pekee haitoshi kuzuia uzururaji kwa walimu wazembe.

My take:-
Si busara sana kudhani bure ndio suluhisho la matatizo yetu,suluhisho la matatizo ni
kufahamu nini chanzo chake.Aliyeleta suala hilo hayumkini hakuwasiliana na wakubwa
zake,hususani Waziri mkuu kwani sio walimu wa Dar pekee bali ni Nchi nzima.
Masuala kama haya na mengine ambayo angependa kuyaibua ni bora yajadiliwe
kwanza na wakubwa zake badala ya kwenda moja kwa moja kwenye media na
kutangaza vile anavyofiki.
Sawa anaweza akawa ni very intelligent kwenye decision making,lakini akateleza
kwenye implementation na follow up.
 
Hivi tatizo la walimu ni sh 800 kwa siku? Serikali ifikiri upya juu ya watumishi wake.Manurse nao wakitaka bure itakuwaje? watafutieni usafiri wao mbona wakati wa teachet kila sector walikuwa na usafiri wao?.Eee banae mi wife nisha mmnunulia usafiri wake.Wawalipe stahiki zao vzr itakuwa bora kuliko kupewa majina bandia na makondakta rafiki yao na makonda
 
Back
Top Bottom