mbongo_halisi
JF-Expert Member
- Apr 16, 2010
- 6,607
- 4,902
Kuwa mwana wa Mungu,kunahitaji maelezo,kwa kuwa Yesu alizaliwa Na Maria,Mwanadamu, Lakini Mungu alipulizia Pumzi yake ili apate Mimba yule Mariam. Sasa tunasemaje kuhusu Adam ,Babu yetu yeye hakuwa na baba wala mama ,si yeye angelistahiki zaidi kuwa mwana kamili wa Mungu?battawi koran yenu ni matokeo ya kitu kinachoitwa UPINGAJI.
Koran inapinga mafundisho ya Biblia karibu ya agano jipya karibu yote yani imefanya kinyume chake.
Mfano Nabii aliye mkuu kuliko manabii wote ulimwenguni Yohana mbatizaji anasema Yesu ni mwana wa Mungu na alikuja kuukomboa ulimwengu kwa kufa kwake tumepata ondoleo la dhambi (kiroho) Koran inasema Yesu si mwana wa Mungu ila inakubali ni Masihi seriously?
Biblia inatuambia Yesu alizaliwa horini koran inasema alizaliwa chini ya mtende seriously?
Poleni na majukumu ya hapa na pale sasa na kale yanayowafanya msilale, niende moja kwa moja kwenye mada husika.
Kama kweli maombi yanafanya kazi kwa namna ambayo tunaaminishwa, kwanini viongozi wa dini wameungana kutekeleza agizo la kuvunja mirundamano ikiwemo mijumuiko ya kiibada ili kuikwepa korona?
Kama walifanya maombi kwa lengo la kuizuia corona isiingie nchini, lakini tunaona corona imeingia, nini kinachokufanya uwaamini kua maombi ya sasa wanayojipanga kuyafanya yataitokomeza corona mazima?
Haya mambo probably si magumu ila ugumu tunauweka sisi kwa kuweka mizaha kwa kutumia kivuli cha dini.
Hivi mfano hawa madaktari wetu na sekta ya afya kiujumla wangejumuika kwenye maombi kwa kuamini kwamba maombi ni njia madhubuti ya kutatua matatizo kama haya katika kila janga la ugonjwa. Kama ambavyo watu wa dini wamekua wakituhimiza kufanya, je tungefanikisha kutibu gonjwa lipi kwa maombi?
Ngoma inaingia tanzania wabongo tulijitia wachamungu sana kua tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na n'ge hivyo ukimwi kwetu sio tishio.
Lakini tunachokiona mpaka saizi mapasta na masheikh wanachukua vidonge kwa siri sana. Lakini pamoja na hayo hatuwaoni wakijisalimisha kua wameshindwa kudhibiti ukimwi kwa maombi yao.
Mungu ambaye tunamtolea sadaka kila siku halafu katika matatizo kama haya kajichimbia tu wala hatuoni juhudi zake, huyu si mungu wakuabudiwa. Ni sawa na rafiki mnafki ambaye kwenye matanuzi mkiwa viwanja mnakua naye karibu sana halafu ikatokea siku umeishiwa anakukimbia.
Wahubiri wanahubiri huku wamevaa face mask at the same time wanasema damu ya yesu ni tiba ya kila kitu. What a joke but i ain't laughing?
Tunaambiwa ukiwa na imani waweza kuamisha hadi milima lakini sikutegemea kuona vatican, mekka ziwe kipaumbele kukataza watu wasiende kwao kwa hofu ya korona.
Mungu muweza wa yote yuko wapi mbona kawasusia msala madaktari wetu halafu yeye amesizi tu eti mpaka aamshwe kwa maombi?
Kwanini mungu mjuzi wa yote na muweza wa yote ahitaji maombi?
Mbona kwenye zile hadithi za gharika na sodoma na gomora huyu mungu ali-respond haraka sana kwanini asifanye hivyo kwenye janga hili linalomaliza ndugu zetu na kudhoofisha hali ya uchumi wetu?
Hivi kweli mungu huyu yupo kweli? Maana viongozi wetu wa dini nao wanaathirika mpaka inafikia hatua italy makanisa yameshehena maiti inamaana yeye haoni?
Kwanini Mungu ahitaji maombi yetu ili aweze ku-solve matatizo yetu, ilihali anaelewa hitaji la moyo wetu hata kabla hatujasema?
====
Chukua tahadhari kwa kufuata angalizo lililotolewa na mamlaka ya afya Corona haidhibitiwi kwa maombi bali kwa kuepuka makatazo ambayo yameainishwa na shirika la afya
Hakuna popote ndani ya biblia ilipokataa kuoa zaidi ya mke mmoja. bali Kuna pendekezo tuu lilopendekeza kuwa kuto kuoa ni bors kwa kiongozi wa dini,na atakae owa aowe 1 tena hiyo ni kwenye agano jipya.
Lile la kale Unaowa upendao.
Kwa hiyo Qur-an na Biblia kwa hili viko sambamba.
Nyogeza
Hata lile la Mungu mmoja na Utatu mtakatifu, Qur-an imewakataza wakristo juu ya imani hiyo kwa kuwa ni ya kupangwa na wanadamu si ya Mungu.
Simply juu ni kule Nywele zako zilikoelekea.
Scientifically juu ni 'out of earth's surface' both directions' as you like' tunakuita juu.
Kwa upande wa Mungu anaposema juu ni kwa sababu yeye yupo nje ya hii dunia na nje ya space.
Yeye ni mkuu na ana kiti cha enzi hukko aliko.
Ukubwa wa kistuli cha hicho kiti kina enea mbingu na nchi, sikuambii ukubwa wa hicho kiti chenyewe.
Mungu katika kuumba kwake ,Kiti chake cha enzi ndio kiumbe kikubwa kuliko vyote, nacho kiko nje ya space, nje ya Galaxy
UNATAKIWA KULINGANISHA NA KUBAINI HITILAFU, MAFUNDISHO YA MSINGIKwanza kabisa ukiikubali biblia kua ni kitabu cha kweli hupaswi kutoa dosari ambazo ziko ndani yake
Kutoa dosari katika biblia kwa kuilinganisha na kuran kunaonesha kua hukubaliani na biblia, bali unaangalia maneno gani ambayo kwenye biblia yana match na maneno ya kuran
Mkristo anaweza kusema kwa kutumia akili yake anakubaliana kua biblia ni kitabu cha kweli kilicholetwa na mungu, nawewe ukisema kitabu hicho cha kuran ni cha kweli kutoka kwa mungu halafu wote mkakubaliana kua mungu ni mmoja, hiyo ni "contradiction"
Mungu wa biblia ambaye kawasetia pepo ya kuimba na kuabudu milele na mungu wa kuran ambaye kawasetia pepo ya mabikra 72 wanaume. Mungu hao hawawezi kua mmoja
Mpaka hapo tunaona kua akili ya mtu kukubaliana na jambo fulani sio kipimo thabiti kujua ukweli wa hilo jambo ambalo yeye kalikubali
It's Scars
Jiongeze kujisomea, Najuwa wewe akili yakoiko kwenye makalio tuu,unafikiria kujisaidia ,lakini hayo ni Muhali Kwa Mungu,wala hahitaji hayo."Kiti cha enzi"
Huyo mungu anakaa kwenye hicho kiti inamaana ana makalio kama sisi?
Habari hii umeipatia wapi?
It's Scars
Sasa inaonesha unaanza Kuamini Uwepo wa Mungu, lakini unaelekea kwenye Ukiristo,Mkristo anaweza kusema kwa kutumia akili yake anakubaliana kua biblia ni kitabu cha kweli kilicholetwa na mungu, nawewe ukisema kitabu hicho cha kuran ni cha kweli kutoka kwa mungu halafu wote mkakubaliana kua mungu ni mmoja, hiyo ni "contradiction"
We jamaa vina vyako vimekaa pouwa Ila Napingana kwa hoja zako zilizojaa tafiti changa
Twende
Scars nakufananisha na slay queen/... Hoja zako ziko weak.. Zama za Covid19/ Unapinga uwepo Wa Mungu/ unaendelea na drama za wazungu/ na majungu/ hauko smart nime prove/ we zuzu/
Nigga u better stay cool/ Am a graduate from school.....
Note:
Corona virus is real ,we need to take extra cares,
One love
Tatizo lako unaandika maneno mengi sana alafu haujibu maswali yangu.Kuwa mwana wa Mungu,kunahitaji maelezo,kwa kuwa Yesu alizaliwa Na Maria,Mwanadamu, Lakini Mungu alipulizia Pumzi yake ili apate Mimba yule Mariam. Sasa tunasemaje kuhusu Adam ,Babu yetu yeye hakuwa na baba wala mama ,si yeye angelistahiki zaidi kuwa mwana kamili wa Mungu?
Eva yeye kaumbwa bila ya Mama ,hata yeye angelistahiki kuitwa mwana wa mungu.
Kuwa Mwana wa mungu hapa umsikilize yesu mwenyewe ,amejiitaje?
Mbona yeye alijiita 'MWANA WA ADAM''?
Hakuwezi na mimi nimeshafika Bethlehem alipozaliwa Yesu tumeelezwa yote.ama kuhusu kule Horini hakuwezi kuwa na Mtende?.
Kama haikuwemo wewe umeitoa wapi? Yani Koran iisemee Biblia like seriously?Qur-an haijakataa ,kuzaliwa yesu bila ya baba,ila imekuongezea information ambayo kwenye biblia haikuwemo.
Uwiii nasekaga!Huo mtende ulitajwa hapa kwa malengo mahususi,aliutikisa na kumletea tende kama chakula baada ya kujifungua.
Biblia inazungumza habari za kupelekewa zawadi tu na mama jusi haisemi alikula tende wala kuzaliwa chini ya mtende.Hatukuona kwenye biblia habari ya kunywa maziwa eti kwa vile kajifungukia Horini(zizi la ngombe) labda hii nayo ingelifanana
Hii ni misingi yako tu hakuna Mkristo mwenye hii misingi.Misingi ya Kikristo ni hiyi hapa kwa mujibu wa Yesu mwenyewe.
1.Uzima wa milele ni kumjuwa Mungu kuwa Ni mmoja wa kweli na wa pekee.( One God)
2. Yesu Ametumwa na Mungu ,na kwa hiyo ni mtumishi wake.
3.Yesu kaleta Ujumbe ,na wanafunzi waliupokea.
4.Wanafunzi wa Yesu wao wamejuwa kuwa Yesu katoka kwa Mungu ,na ujumbe umetoka kwa Huyo Mungu.
5.Wakati Yeu anaondoka ,anawasisitiza watu wake kushika Mafundisho na kuyafanyia kazi.
Soma Injili ya
Yohana 17:-
1 Yesu alipokwisha sema hayo, alitazama juu mbinguni, akasema, “Baba, saa imefika! Mtukuze Mwanao ili naye Mwana apate kukutukuza. 2 Maana ulimpa Mwanao mamlaka juu ya watu wote ili awape uzima wa milele wote hao uliompa. 3 Na uzima wa milele ndio huu: kukujua wewe uliye peke yako Mungu wa kweli, na kumjua Yesu Kristo uliyemtuma. 4 Mimi nimekutukuza hapa duniani; nimeikamilisha ile kazi uliyonipa nifanye. 5 Sasa, Baba, nitukuze mbele yako kwa ule utukufu niliokuwa nao kabla ya kuumbwa ulimwengu. 6 “Nimekufanya ujulikane kwa watu wale ulionipa kutoka duniani. Walikuwa watu wako, nawe ukanipa wawe wangu; nao wamelishika neno lako. 7 Sasa wanajua kwamba kila ulichonipa kimetoka kwako. 8 Mimi nimewapa ule ujumbe ulionipa nao wameupokea; wanajua kwamba kweli nimetoka kwako, na wanaamini kwamba wewe ulinituma.
I don't believe them do you got anything else?The Jehovah’s Witnesses in their “AWAKE” Magazine dated 8th September 1957 published the following headline:
“50,000 Errors in the Bible” wherein they say “..there are probably 50,000 errors in the Bible...errors which have crept into the Bible text...50,000 such serious errors...” After all of this, however, they go on to say: “...as a whole the Bible is accurate.”
Nikienda kanisan nikasikia maubiri ya padri huwa nacheka kimoyomoyo na kusema hapa niwe na kuja ilimradi tuu nisitengwe na wanajamii.Wote wako chaka wanaskilizia madaktari watoe jibu la hitimisho maana wao tayari wamejipanga na majibu yao mfukoni mwao
Ikitokea madaktari wametoa dawa, tutawaskia wakisema maombi yao ndio yamewezesha wanasayansi kupata dawa.
Na ikitokea hakuna dawa iliyotengenezwa na wanasayansi watasema kua mungu katupa corona ili kutujaribu na kutupima imani au watasema mungu hujibu maombi kwa wakati wake
Hiyo paragraph ya mwisho sio kweli, mwenyezi Mungu mnambebesha misalaba ambayo sio. Hii haina tofauti kama unavyowaona wananchi kwa kilakitu kumlaumu Rais wa nchi.Wewe jamaa bhana
Kama hii ndio hoja yako basi unaweza kusema kila jambo limekuja kuumbua uongo wa dini.
Kwa nini hukusema kutafuta riziki kumekuja kuumbua uongo wa dini,maana ingetosha tu mtu kukaandani na kuomba dua halafu chakula kikamshukia.
Au kwanini hukusema kusoma kumekuja kuumbua uongo wa dini,maana ingetosha tu mtu kwenda msikitini kuomba dua kisha tayari akawa professor. Na hivyo hivyo mambo mengine.
We jamaa mwenyezimungu aliweka nidhamu/kanuni katika ulimwengu na mambo hayaendi vile unavyo fikiri wewe.
Kila mtu kazaliwa na wazazi wake, sasa ukisema ameumbwa unatakiwa uthibitishe kaumbwa na nini?
It's Scars
Chain hiyo ukiifata bila kuipindisha itakuletea swali kua hata mungu naye atahitaji chanzoNenda na chain hii nani alimza mzazi wako nk nk nk nk mpaka ukomo wake
Sent using Jamii Forums mobile app
Sikiliza ,Uzi huu ulikuwa ni wa Mtu asiyeamini dini ,wala Mungu,Hii ni misingi yako tu hakuna Mkristo mwenye hii misingi.
Msingi wa Ukristo ulio mkuu ni UPENDO na msingi wa pili ni kufuata mafundisho ya Kristo OVER!
Hii verse uliyoiweka hapa unaiamini?