Invisible, shukran sana mzee,
Kama Bunge lingekuwa na meno, lingeweza kuibua mambo mengi kwenye riport ya mkaguzi mkuu wa mahesabu ya serikali, lakini naogopa, yule dada yangu (Speaker) hawezi kuwa na ujasiri kuivua nguo serikali ya Joka Kuu.
Ukweli ni kwamba, hatuna serikali inayosimamia masirahi ya wananchi (wakulima na wafanyakazi), bali kuna genge la majizi, majambazi na mafisadi, ambalo baada ya miaka mitano nchi itakuwa imefilisika na kuuzwa yote.
Nakumbuka mtu aliyekuwa na kauli ya kuhoji na kusitisha uovu huo alikuwa Mwl Nyerere, sasa hayupo, na hata yule rafiki yake Kingunge, kwa sasa amezeeka sana na hawezi kuzungumza!!!
Wa-Tz wenzangu tupeane pole.
Lakini tunaweza kufanya jambo ili kujiokoa na hali hii, kuunga mkono sauti ya wanaharakati na vyama vyenye upinzani wa kweli. Kama hali ikiendelea kuwa hivi hadi June, yaitishwe maandamano ya nchi nzima kuikataa serikali. Yes, nimesema hivyo. Nipo tayari kuwajibika na kauli yangu kwa ajili ya nchi yangu.