Hivi mnavyosema serikali ndio ilipe mnamaanisha nini?.....ninavyofahamu mimi serikali inatoa hela zake kutoka katika kodi zetu.....kwa hiyo ukisema serikali ilipe, inachomaanisha ni kwamba wananchi walipe.
Hii ya nani alipe ni kupoteza dira tu.....sisi msimamo wetu uwe HAKUNA KULIPA......sio tunabidsha nani alipe.
Mkuu kwanza ninakushukuru kwamba umeonyesha kilichojificha ndani ya kauli hizi za TANESCO au SERIKALI kulipa. Mimi binafsi sikumwelewa sawasawa mwenyekiti wa POAC aliposema serikali ndiyo ibebe mzigo wa kuilipa DOWANS. Maana yake ni kwamba, Mh Zitto na kamati yake walikuwa wanahalalisha malipo kwa DOWANS yafanyike. Kimsingi walikuwa wanasema watanzania wailipe DOWANS.
Kuna vitu vya kuviangalia tunapotazama utendaji wa Bunge na serikali. Ukichukua taifa kama kampuni ambayo inamilikiwa na wana hisa utaona kwamba:
(i) Taifa la Tanzania linakaliwa na Watanzania wenyewe ambao kimsingi ndiyo kama wanahisa wa Rasirimali zilizopo Tanzania.
(ii) Serikali ni Utawala- Management katika taifa letu. Hapa ni sawa na kuwa na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni pamoja na wasaidizi wake, ambao ni wakuu wa Idara mbalimbali katika kampuni. Rais wa tanzania ni kama Mkurugenzi mtendaji wa kampuni na mawaziri wake ni kama wakuu wa idara wa kampuni.
(iii) Bunge ni kama Bodi ya Wakurugenzi iliyopewa dhamana ya kuhakikisha (a) Serikali yaani management inatimiza wajibu wake wa kuhakikisha rasirimali (Amana) za nchi zinatumika ipasavyo na kuongeza tija. (b) Bunge linakuwa ni kama vile NOn- Executive Directors wa kampuni. Sasa basi, Bunge haliwezi lote kuwalinafanya kila kitu, ndipo zikawepo kamati mbalimbali kama za akina Zitto na wengine kwa lengo la kurahisisha wajibu wa Bunge katika kuwatumikia wanahisa wa nchi ya Tanzania.
Sasa basi, Mh Zitto na wenzake wanaposimama kwa niaba ya Bunge kusema Serikali ndiyo iwalipe Dowans, inamaanisha kwamba Utawala utumie amana za taifa kuwalipa DOWANS jambo ambalo TUNALIPINGA NA CHADEMA kikiandamana kupinga hilo. Hapo ndipo ninajiuliza maswali kwamba hivi Mh Zitto na wenzake hawakupata kuona kwamba wanajichanganya na kwamba hawaelewi vizuri majukumu yao???
Zitto na wenzake watoe hoja zinazoeleweka badala ya kuanza kujikanganya!! Tunahitaji utendaji wa Bunge wenye tija siyo kuzungumza zungumza vitu ili mradi kupata media coverage!!