Clouds TV acheni kuwadhalilisha bibi, mama zetu!

Clouds TV acheni kuwadhalilisha bibi, mama zetu!

Mimi nashangaa hao wabibi walioenda kwenye hili shindano hawana ndugu wala watoto. Yani ni aibu siwezi kumruhusu mama yangu akashiriki upuuzi kama huo. Mengi yameandikwa na members waliochangia mwanzo kipindi kifutwe ni udhalilishaji na huyo mtangazaji akapimwe akili siyo mzima nadhani.
 
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyo--havina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha 'BIBI BOMBA' kinachorushwa na TV hiyo. Nimehudunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.

Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa 'Biology', akajibu 'ndiyo'. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.

Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.

Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu--tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki.

cc: RRONDO
 
Last edited by a moderator:
Yaani yule mtangazaji anayeendesha kile kipindi ni mbumbumbu kuliko maelezo. Eti alimuuliza bibi aseme bhang magazine ni kitu gani. Bibi akaWa amemsikia vibaya--akadhani amtetamka BAN MAGAZINE. Basi bibi akajibu "ban magazine ni gazeti lililopigwa marufuku (banned)--yaani ambalo halitakiwi kuwepo". Na lile litangazaji, likiwa kama MODERATOR wa kipindi, halikumsahihisha bibi--likamuacha bibi apuyange hivyo hivyo! Sasa bhang magazine na wabibi wapi na wapi? Litangazaji linauliza maswali ya kibangebange na ambayo hayana mwelekeo wowote! Hivi hawa watangazaji wa TV mbumbumbu kama huyu huokotwa wapi?
kama Ruge unafika JF hili ni somo tosha ! Huyo Abuu wa Kitaa ni kijana Mzinzi hakuna mfano ! Tabia zake nje ya kipindi si za kuigwa ! Ruge hicho kipindi kilipaswa kiwe cha kuelimisha jamii ,kiyakemee mabaya kulaani Bangi,uzinzi,udokozi na mitabia mibaya kama ya kuvaa nguo chini ya makalio na viheleni kwa vijana wa kiume ,Ruge najua wewe ni bingwa wa kuziba masikio ! Lakini kwa hili usizibe sikio funguka rekebisha hiyo kasoro.
 
Hicho kipindi kikilaani uvaaji wa hovyo,hovyo, yaani (mlegezo) kuvaa nguo chini ya makalio, vijinguo vya kubana,fupi kwa wadada na uvaaji usiofuata Maadili kitaleta maana ! Kumbuka Hao ni wazee wanatakiwa wasaidue Taifa kurejesha maadili yake ambayo yamebomoka kwa kiasi kikubwa.
 
kama Ruge unafika JF hili ni somo tosha ! Huyo Abuu wa Kitaa ni kijana Mzinzi hakuna mfano !

Hivi unapomuita mtu mzinzi unakuwa na ushahidi gani maana uzinzi unafanyiwa faragha. Hapa kwa kuongea kwa uhakika hivi ni huenda Babuu kakuzini wewe au mtu wako wa jaribu.
 
Hivi kumbe hizo clouds tv na redio bado zinasikilizwa/kutazamwa!!!!!!!!
Poleni kwa yaliyowakuta kwa kutizama hizo media
 
Hivi unapomuita mtu mzinzi unakuwa na ushahidi gani maana uzinzi unafanyiwa faragha. Hapa kwa kuongea kwa uhakika hivi ni huenda Babuu kakuzini wewe au mtu wako wa jaribu.
mchawi na mwanga wanaloga usiku huku wakijitahidi wasijulikane ,lakini watu huwajua,Sembuse Uzinzi ambao mara nyingi harakati za awali huwa hadhalani huko faraga ni fainal,tambua mashalo huwa hawana siri kila wakimega mdada huanika live.
 
Swali tu...commercial break...

Hivi kila kipindi cha TV au redio au anything that goes public ni sharti kwamba kielimishe jamii? Seriously?

Na hizo educative programmes zina viewer base kubwa kiasi gani compared to the others?
 
I never knew kuna such program, but inategemea kuna soko lake, kila program in target viewers au listerners(sp) tofauti, nadhani ukichoshwa change channel,

I subscribe to 102.5 ni jamii ya clouds in the morning na jioni ni any radio that has DW dunia yetu !

TV on weekdays naangalia kwa nadra sana, I record all my favourite shows na kuzirudia weekend especially soapies omnibus, mengine yote nasoma magazetini
We huna akili wewe so kukiwa na viewers ndo waoneshe?,kwani porno movies hazina viewers mbona hawazioneshi..
 
Naunga mkono hisia za mleta mada. Hata kama utandawazi unatulazimisha kuiga mambo ya kigeni, si kwa kiwango hiki cha kudhalilisha wazazi wetu kisa tu umasikini wao! Kipindi hiki kinadhalilisha na kinaenda kinyume saana na tamaduni zetu kama Waafrika. Sikiungi mkono na kusema kweli kimenifanya nipate majibu ni kwanini clouds waliwahi kutozwa fine (kupewa adhabu ya pesa) na TCRA kwa kuunga mkono na kurusha vipindi vyenye hisia za ushoga! Kipindi cha bibi bomba kinadhalilisha tamaduni zetu Waafrika kupindukia; hakifai, wote tukipige vita.
 
Ruge hili Darasa natumai utalitumia vyema kuweka mambo sawa hao wazee watumike kurejesha nidhamu ya mavazi kwa vijana hata unyoaji wa nywele siku hizi umejaa staili ya Kiduku ,eti kisingizio cha kwenda na wakati ! Mbona vijana ni wepesi wa kuiga yale ya ajabu ajabu ! Lakini ni wazito wa kushabikia kilimo kwanza na mambo ya maana.
 
Swali tu...commercial break...

Hivi kila kipindi cha TV au redio au anything that goes public ni sharti kwamba kielimishe jamii? Seriously?

Na hizo educative programmes zina viewer base kubwa kiasi gani compared to the others?
Tz tupo nyuma kimaendeleo hivyo vipindi vya kuelimisha Jamii ni muhimu kwa sasa mpaka watu watambue kuwa tamaduni za wengine hazisaidii kurejesha nidhamu ambayo inazidi kumomonyoka kila siku,lazima tuyatambue maadili ya mtanzania kuwa ni bora kuliko ya wageni,tuyapende ya kwetu kwanza pasipo kuwa mtumwa wa mitabia ya kigeni.
 
Kama hali ndio hii ya kila mtu kuona hawa jamaa ni shidah katika jamii, basi kuna umhimu wa TCRA kutazama upya kazi zao na vipindi pia.

Na jiuliza kitu kwanini station nyingi sijawaiona zikilalaimikiwa hapa kwa kazi kuna kitu hapa

cc; Ruge

Nimetimiza wajibu wangu kama raia mwema kwa kutuma malalamiko yafutayo bila shuruti kwenda TCRA ili wamzuie Ruge na timu yake aache kuwadhalilisha bibi zetu. Na attachment ifuatayo inaonesha kwamba fomu ya malalaniko niliyotuma imewafikia TCRA. Mimi kazi yangu nimemaliza, ngoja tuone TCRA watachukua hatua gani kukomesha udhalilishaji huu. Kama itashindikana kabisa, labda tuwahamasishe wananchi waandamane na kususia bidhaa za Clouds TV ili wapigwe njaa wajifunze kuheshimu haki za binadamu wanyonge:
==============================================================================================
Clouds TV wamekuwa wakiwadhalilisha bibi zetu kupitia kipindi chake cha BIBI BOMBA kwa muda mrefu sasa. Nadhani sasa imefika wakati TCRA mchukue hatua ya kusitisha kipindi kile, kuwalipisha faini wahusika au kuwaelekeza namna nzuri ya kutangaza kile kipindi bila kudhalilisha wale watu wazima hadharani. Watu wengi hawapendezwi na udhalilishaji ule lakini hawana namna ya kufanya kuuzuia. Nchi inaendelea kupata laana mbalimbali kwa sababu ya udhalilishwaji wanaofanyiwa watu wazima kama wale, na bahati mbaya ni kwamba udhalilishwaji huu hufanywa na vijana wadogo kabisa kwa kisingizio cha kwamba wanawashindanisha (sijui kwa kitu gani).

Hata kama hawa bibi wanatoka kwenye familia masikini kisiwe kigezo cha kudhalilishwa hivyo. Elewa kwamba nao ni watu wanaostahili kuheshimiwa kama raia wengine katika nchi hii. Sidhani kama TCRA hamuuoni udhalilishaji huu au kama nyie mnaona ni sawa kipindi hiki kiendelee kuruka hewani. Hivi kweli ina maana hamjawahi kuona kipindi hiki? Kama bado hamjawahi kukiona basi nendeni pale Clouds TV muwaambie wawape ile mikanda waliowapiga wale kina bibi halafu muipitie muone kama kweli inakidhi vigezo vya TCRA. Au kama hamhusiki na utoaji wa adhabu kwa makosa kama hayo, naomba suala hili mlipeleke kwenye kitengo kinachohusika ili Clouds TV wachukuliwe hatua zinazofaa kwa kuwadhalilisha mabibi hawa.

Asante kwa kunielewa na kwa kuchukua hatua zinazofaa dhidi ya ukiukaji huu mkubwa wa haki za binadamu.


View attachment CLOUDS TV.bmp
 
Last edited by a moderator:
Clouds management team ni wapuuzi sana kuruhusu kipindi kama hiki.Sizungumzii TCRA kwa kuwa najua hawana ubavu wa kuipa ban radio/tv inayotumiwa kufanya kampeni ya nguvu kuwarudisha vijana kwenye chama chao.

Ni kama vile kipindi cha kumtafuta bibi anayevuta bangi sana au aliyechetuka akili kwa sababu ili bibi ayajue maujinga yale yaliyopewa jina la maswali,lazima awe msela mvuta bangi na mwenye akili zilizochetuka.

Idea yao eti ni kumtafuta bibi anayeenda na wakati na anayeweza kujua mambo ya vijana wahuni,wavuta bangi na waliokosa malezi mazuri.Sasa hii ni idea au kadhia?

Hawa jamaa huwa wanajifanya wenyewe wanaweza kila kitu kisa wameiweka mfukoni serikali ya "mshkaj" wao ambaye aliwahi kuwapigia promo dhidi ya redio zingine.

Kuna v2 vingi vya kupima IQ za mabibi hao lakini wenyewe "akina mzee wa king'oko" wamestick kwenye ile "bibi msela ndo mwenye akili"!Yani wanamuona bibi wa mfano ni bibi cheka kwa hiyo wanatamani mabibi wote wawe kama yeye!

Wanawadhalilisha hawa viumbe ambao jamii inapaswa ifaidike na uzoefu wao wa maisha.Badala ya kuwatumia hawa akina bibi kuipa jamii faida wao wanawatumia kuiathiri hasi jamii na kuleta utamaduni mwingine wa ajabu na kudhamiria kwa ari,nguvu na kasi zaidi kuupromote na kumpata mshindi atakayefiti kwenye hiyo definition yao ya "bibi bomba".

Msemaji wa clouds huku kwenye jf yule jamaa anayeishi ng'ambo na mwenye kupenda kuandika kiinglishi kuonesha mkwara mpaka sasa sijaona majibu yake.Kama kayatoa ni kwa kupitia ID nyingine sio ile ya kawaida.Huenda hata yeye kwa hili anashindwa atetee vp ingawa siamini sana kwa sababu jamaa ameshatetea vingi vya ajabu vya hawa wapuuzi.
 
Last edited by a moderator:
Mimi nilikuaga mfuatiliaji mzuri sana wa vipindi vya clouds , lakini kipindi kama kile cha saa kumi cha kina kibonde kilinifanya niachane kabisaa na hiii radio, watu w azima kazi kuongea upuuzi na kucheka ovyo kama mashoga, yani wanaudhi sana, upuuzi ni mwingi sana kwenye vipindi vyao.
Hiki kipindi si kibaya kipo Vizuri na kina wasikilizaji wengi japo Kibonde huchemsha mara moja moja,lakini wengine wapo Vizuri Kwa upande wa Radio clouds wapo Vizuri japo kuna kasoro ndogo big up Sebastian maganga mkuu wa vipindi.
 
TCRA wamesikia

CLOUDS wamesikia

Ila kwa uzembe na ulegelege wa serikali yenu utakuta kipindi kinaendelea
 
Swali tu...commercial break...

Hivi kila kipindi cha TV au redio au anything that goes public ni sharti kwamba kielimishe jamii? Seriously?

Na hizo educative programmes zina viewer base kubwa kiasi gani compared to the others?

Mkuu, unaweza kutuambia kipindi cha BIBI BOMBA kina manufaa gani kwa jamii au kinatoa mafundisho gani kwa watanzania? Kwa hivyo kama sio kila kipindi kinapaswa kuelimisha jamii kwanini video za ngono hazionyeshwi kwenye TV? Usitetee ujinga kwa maneno makavu bila kuujengea hoja huo ujinga unaoutetea. Acha kufikiri kwa kutumia tumbo, tumia kichwa.
 
Back
Top Bottom