Clouds TV (Ruge na team yake) mlipoanzisha shindano hili la BIBI BOMBA nilifikiri wanataka kuwatumia bibi hawa kwa ajili ya kutukuza uTanzania wetu, utamaduni wetu na mchango wao ili kufanya vijana wafahamu utamaduni wetu ambao unaanza kusahaulika katika jamii. Lakini tunachokishuhudia hivi sasa ni kinyume chake. Ni udhalilishaji usiovumilika wanaofanyiwa bibi na mama zetu. Haingii akilini kumuimbisha bibi wa miaka 65- 70 nyimbo za muziki wa kizazi kipya au kumvalisha suruali wakati tunazo nyimbo zetu za kabila mbalimbali na pia tunafahamu kabisa katika maisha ya kawaida bibi hao hawavai hivyo!
Ruge umekosea sana(wewe ndiye msimamizi wa TV yako kufanya marekebisho. Jipe muda fuaitili shindano hilo uone kama kuna lolote la maana jamiiinajifunza. Badili maramoja; itapendeza na kuleta maana zaidi kama bibi hawa watashidanishwa kwa mambo yenye maadili na kudumisha utamaduni wetu Watanzania
EJL
Eti bibi anaulizwa, unamjua facebook? Sasa bibi fb inamsaidia nini kama c upuuzi?
zambada,kaiza sosa,mtumbaya,babuu wakitaa,mfalme mswati....mume wenu....majina kibao
we mkuda umepima?...au nimmoja kat yao alio wapitia tupe ushahidi wa uyanenayo...
ukimwi ni kitu cha kawaida sana mshikaji anakula arv mbona hata watu kibao wanao halafu mbona umeshtuka utadhani umetiwa kidole
hii laana ya kuwadhalilisha bibi na mama zetu itawaandama clouz hadi mtapoomba msamaha hawa mabi wakubwa hawakustahili kufanyiwa hivi hata kama economic base yao poor😕😕😱😱
...dah mkuu,yaani kama ulikuwepo eneo ambalo tulikuwa nasi tunasikiliza hicho kipindi(nilikuwa kwa kinyozi),kiukweli nasi tulijisikia fedheha kubwa sana kuona bibi na mama zetu,kuulizwa maswali ya kijinga namna ile,
Labda nami niwaombe Viongozi wa Clouds TV kwanza wakiangalie vizuri hiki kipindi kwani kina makosa mengi ya kiitaaluma na ikiwezekana watafute mtangazaji mwingine wa kuendesha hiki kipindi,huyo Babuu wa Kitaa hafai,kwanza umarekani mwingi,maneno ya mtaani mengi na maswali ya kijinga.
Kumbe wengi tunaokerwa na huu ujinga
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyo--havina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha 'BIBI BOMBA' kinachorushwa na TV hiyo. Nimehudunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.
Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa 'Biology', akajibu 'ndiyo'. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.
Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.
Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu--tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki.
Bibi wa miaka 70 anapofundishwa apozi kama Black American thug na kuambiwa aseme "whatsup ma nigger" na kufanya ndio tangazo la mara kwa mara, huu ni udhalilishaji na ushenzi!!