GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,638
- 108,993
Mlizoea GENTAMYCINE naleta tu Taarifa Nyeti za Ndani ya Yanga SC ila Usiku huu nawaletea moja Kabambe kutoka ndani ya Simba SC ( Timu ambayo naishabikia ) mno na Naipenda.
Taarifa ikufikie ya kwamba kumbe Kocha Juma Mgunda ( ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi Simba SC na Boss wa Kocha Mkuu wa Simba SC Roberto Oliveira ) ndiyo alipanga Kikosi cha Juzi kilichocheza na Al Ahly FC huku akiwa hakumpanga Beki Shomary Kapombe ( ambaye kwa mujibu wa Kocha Mgunda ) alisema kuwa hakuwa Fiti na Kiwango chake kwa sasa Kimeshuka.
Cha Kushangaza Kocha Mgunda ( Mkurugenzi wa Ufundi Simba SC na Boss wa Kocha Kiutendaji ) akijua ameshakubaliana na Kocha Mkuu Roberto kuwa Beki Shomary Kapombe asianze na apangwe Beki Israel Mwenda au David Kameta 'Duchu' ghafla akaona Kapombe anaanza Kitendo ambacho Kilimkwaza sana Kocha Mgunda kwani alishajua Kapombe hakuwa Fiti na kweli hata katika Mechi ile Alipwaya, akawa Uchochoro hadi Kutolewa na kuonyesha kuwa kumbe kwa 100% Kocha Mgunda alikuwa sahihi ila Kocha Roberto alimpuuza.
Hivyo basi kwa sasa Sakata hili linafichwa / linapoozwa lakini kama Simba SC itatolewa rasmi na Al Ahly FC Jumanne kule Misri basi Timu ikirejea Kocha Mkuu Roberto Oliveira atakuwa Kikaangoni kwa Mahojiano na huenda akifanya Mzaha akafurumushwa rasmi japo uhakika nilionao ni kwamba ametegwa Kufukuzwa katika Mechi za CAFCL huku ana Kocha Nabi au Ibenge wakiambiwa Wajiandae ambapo atakayechukua Usukani wa Ukocha Simba SC atasaidiwa na Kocha Mzawa Juma Mgunda.
Haya akina Ricardo Momo, Edo Kumwembe, Bloggers, Watangazaji na Wachambuzi wa Michezo wa Redio na Television tayari GENTAMYCINE nimeshawapeni hii Inside Info huko Simba SC hivyo mkiichukua na kuitumia tafadhali toeni Credits Kwangu na kwa huu Mtandao wangu pendwa wa JamiiForums na msidanganye kuwa mmeitafuta nyie wakati Uwezo huo hamna na ninao Mfalme na Bingwa Mwenyewe.
Taarifa ikufikie ya kwamba kumbe Kocha Juma Mgunda ( ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi Simba SC na Boss wa Kocha Mkuu wa Simba SC Roberto Oliveira ) ndiyo alipanga Kikosi cha Juzi kilichocheza na Al Ahly FC huku akiwa hakumpanga Beki Shomary Kapombe ( ambaye kwa mujibu wa Kocha Mgunda ) alisema kuwa hakuwa Fiti na Kiwango chake kwa sasa Kimeshuka.
Cha Kushangaza Kocha Mgunda ( Mkurugenzi wa Ufundi Simba SC na Boss wa Kocha Kiutendaji ) akijua ameshakubaliana na Kocha Mkuu Roberto kuwa Beki Shomary Kapombe asianze na apangwe Beki Israel Mwenda au David Kameta 'Duchu' ghafla akaona Kapombe anaanza Kitendo ambacho Kilimkwaza sana Kocha Mgunda kwani alishajua Kapombe hakuwa Fiti na kweli hata katika Mechi ile Alipwaya, akawa Uchochoro hadi Kutolewa na kuonyesha kuwa kumbe kwa 100% Kocha Mgunda alikuwa sahihi ila Kocha Roberto alimpuuza.
Hivyo basi kwa sasa Sakata hili linafichwa / linapoozwa lakini kama Simba SC itatolewa rasmi na Al Ahly FC Jumanne kule Misri basi Timu ikirejea Kocha Mkuu Roberto Oliveira atakuwa Kikaangoni kwa Mahojiano na huenda akifanya Mzaha akafurumushwa rasmi japo uhakika nilionao ni kwamba ametegwa Kufukuzwa katika Mechi za CAFCL huku ana Kocha Nabi au Ibenge wakiambiwa Wajiandae ambapo atakayechukua Usukani wa Ukocha Simba SC atasaidiwa na Kocha Mzawa Juma Mgunda.
Haya akina Ricardo Momo, Edo Kumwembe, Bloggers, Watangazaji na Wachambuzi wa Michezo wa Redio na Television tayari GENTAMYCINE nimeshawapeni hii Inside Info huko Simba SC hivyo mkiichukua na kuitumia tafadhali toeni Credits Kwangu na kwa huu Mtandao wangu pendwa wa JamiiForums na msidanganye kuwa mmeitafuta nyie wakati Uwezo huo hamna na ninao Mfalme na Bingwa Mwenyewe.