VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kwanza, tunamshukuru Mungu kwa kuzuia hujuma zisizo na huruma kwa CCM yetu baada ya kuepusha kupokwa kwa nafasi ya Katibu Mkuu jana. Shukrani zetu, kama makada waandamizi na wazee wa chama, ni kwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa Mama Samia S. Hassan kwa kutusikiliza tulipomshauri cha kufanya.
Hatimaye, Katibu Mkuu wa CCM atapatikana kiutaratibu wa kiustaarabu na adabu. Si majungu ambayo hata Mungu anayapiga rungu. Mwenyekiti wetu, kwakuwa aliomba na kupokea ushauri mashuhuri, amefanikiwa kuukwepa mtego wa kupokwa Ukatibu Mkuu wa CCM.
Uchunguzi umeagizwa ufanyike wakati nafasi hiyo ikikaimiwa na Komredi Anamringi Macha. Uchunguzi wa kina utafanyika kwenye tuhuma zilizoelekezwa kwa Katibu Mkuu Mjiuzulu Daniel Chongolo. Uchunguzi pia utazingatia maelezo yake aliyoyatoa na atakayoyatoa chamani.
Komredi Chongolo, just relax uwe na amani. Kwakuwa Kamati Ndogo ya Uchunguzi imeshaundwa na leo inaanza kazi yake, haki itatendeka. Katika sakata hili la Chongolo, CCM itaonesha ukubwa wake. Haitavumilia chama 'kutekwa' na waroho wa madaraka wenye haraka isiyo na baraka.
Walioratibu mpango dhidi ya Chongolo wanapaswa kujua jambo moja. Chongolo ni mwana wa Serikali na chama. Amefanya kazi ya kutukuka na kusifika Serikalini na chamani. Hawezi kuondoka bila kishindo kikubwa chamani. Ripoti itaanika kila kitu. Ukweli na usio ukweli. Heri au shari.
Katibu Mkuu hatapatikana hadi uchunguzi ukamilike. Wa kusafishwa atasafishwa na wakuwajibishwa atawajibishwa. Hakuna upendeleo wala video kwenye jambo hili. Narudi zangu Kilosa nikifurahi kuilinda nafasi ya Katibu Mkuu kwa ajaye au atakaporejeshwa huyu.
Gekul, yalikuwa ndiyo madaraka ya kulevya?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kuelekea Kilosa, Morogoro)
Hatimaye, Katibu Mkuu wa CCM atapatikana kiutaratibu wa kiustaarabu na adabu. Si majungu ambayo hata Mungu anayapiga rungu. Mwenyekiti wetu, kwakuwa aliomba na kupokea ushauri mashuhuri, amefanikiwa kuukwepa mtego wa kupokwa Ukatibu Mkuu wa CCM.
Uchunguzi umeagizwa ufanyike wakati nafasi hiyo ikikaimiwa na Komredi Anamringi Macha. Uchunguzi wa kina utafanyika kwenye tuhuma zilizoelekezwa kwa Katibu Mkuu Mjiuzulu Daniel Chongolo. Uchunguzi pia utazingatia maelezo yake aliyoyatoa na atakayoyatoa chamani.
Komredi Chongolo, just relax uwe na amani. Kwakuwa Kamati Ndogo ya Uchunguzi imeshaundwa na leo inaanza kazi yake, haki itatendeka. Katika sakata hili la Chongolo, CCM itaonesha ukubwa wake. Haitavumilia chama 'kutekwa' na waroho wa madaraka wenye haraka isiyo na baraka.
Walioratibu mpango dhidi ya Chongolo wanapaswa kujua jambo moja. Chongolo ni mwana wa Serikali na chama. Amefanya kazi ya kutukuka na kusifika Serikalini na chamani. Hawezi kuondoka bila kishindo kikubwa chamani. Ripoti itaanika kila kitu. Ukweli na usio ukweli. Heri au shari.
Katibu Mkuu hatapatikana hadi uchunguzi ukamilike. Wa kusafishwa atasafishwa na wakuwajibishwa atawajibishwa. Hakuna upendeleo wala video kwenye jambo hili. Narudi zangu Kilosa nikifurahi kuilinda nafasi ya Katibu Mkuu kwa ajaye au atakaporejeshwa huyu.
Gekul, yalikuwa ndiyo madaraka ya kulevya?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kuelekea Kilosa, Morogoro)