Chikawe awakemea Mwakyembe na Sitta: Waache kuzungumzia DOWANS

eeeuii eeeeuiii, sijawahi kuona serikali iliyoparangatuka namna hii Sitta,Mwakyembe kama muna makende kweli katikati ya miguu yenu ondokeni kwenye serikali hii haiwafai hamuwezi kugombezwa na waziri tena mdogo,umeona dharau zake anaposema Mwakyembe waziri mdogo maana yake nini akiwa waziri mdogo hastahili kuona uchungu kama Mtanzania,KIKWETE KIKWETE baraza lako limekushinda kabisa kila mtu anaropoka kivyake mbona chikawe hakumuonya Selina Kombani Warema walivyotoa maoni yao kuhusu Katiba walisema yalikuwa maoni yao binafsi kwa nini mawaziri hawa wakizungumzia ya dowans wonekana wanampuuza Raisi eeeeuiii nchi yangu Tanzania pole
 
Namuwazia sana jk katika muda kama huu sijui kichwani kwake anawaza nini huyu mkwere!!!!!!!!!!!
 
SITA na Mwakyembe hawajavunja sheria yoyote wala kukiuka taratibu yoyote. Suala la Dowans halijapelekwa kwenye baraza la mawaziri kwa hiyo hakuna kuwajibika kwa pamoja! hawajaweka msimamo wa pamoja. Kwa kuogopa kulipeleka suala hili bungeni au kwenye baraza la mawaziri ili lijadiliwe, hawa wezi na vikorogosi wao wasitarajie kuwa na msimamo wa pamoja. Wananchi tutalipinga, na watu wote wenye akili timamamu watalipinga na kuwazomea!

Suala la Dowans haliwezi kuwa siri ya baraza kwa sababu halijawahi kufikishwa huko. Suala litakuwaje siri ya Baraza la mawaziri wakati halijafikishwa huko? Labda huyu kilaza atwambie kuwa dowans ni siri ya Kikwete, Lowasa, Rostam, Ngeleja, Chikawe,AG na baadhi ya wapuuzi ambao anadhani ni lazima wote togope kujadili????!!!!!!

Hivi akijitokea Waziri akasema kuwa Tanzania haiwezi kuwa nchi ya kiislam au ya kikristu kwa kuwa suala hilo halijawahi kujadiliwa na Baraza la Mawaziri, ataonekana mpuuzi mwenye chuki binafsi na kukemewa na Chikawe kwamba ameshindwa kutunza siri za baraza?????????
 
Kwa bahati mbaya hawakulazimishwa na walikuwa na bado wanahaki ya kukataa nafasi zile. Hizi kauli zao zinatofauti gani na wafanyakazi wanaomwibia mwajiri wao? Au marketing officer anayachafua bidhaa za kampuni aliyoajiriwa. Upuuzi wa namna hii haupo. Hapa ninasisitiza aidha watoke serikalini au wafunge midomo yao.
Mimi naona wasitoke labda wawatoe lakini waendelea kutujuza kinachoendelea halafu sisi wananchi tutachukua maamzi na mfano wako si dhani kama ni sahihi kwenye swala hili anacho kifanya sita na Mwakyembe ni kutuambia wananchi kilichofanyika kuwa jamaa hawakufata taratibu zilizotakiwa yaani kupelea kwenye baraza la mawaziri lakini kama lingepelekwa kwenye baraza likapitishwa na wao wakapinga hapo ndipo tungewataka waajiuzuru...yaani kinacho fanyika kwa sasa ni uwizi wa wazi wazi kama umesikiliza Mdaharo wa jana ITV utakubaliana na mimi na kama hukusikiliza hebu gonga hapa
 
Tanzania imeoza ingawa ina rasilmali nyingi. Tatizo liko kule juu; ni Kama ambavyo Zaire ilivyoharibika kutokana na yule aliyekuwa juu wakati huo, yaani Mobutu. Tanzania is next!!!
 
SAKATA la malipo ya kampuni ya kufua umeme ya Dowans, limeingia hatua mpya baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utawala Bora, Mathias Chikawe, kusema mawaziri wawili waliompinga Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kutangaza serikali kuilipa
kampuni hiyo, walikiuka utaratibu wa serikali.

Aidha, amewataka mawaziri hao, Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kuacha kutoa maelezo ya sekta zisizowahusu kwani si utaratibu wa utawala bora na ni kuwachanganya wananchi.

Akifafanua kuhusu kauli zilizompinga Waziri Ngeleja, Chikawe alisema mawaziri hao walipaswa kufuata utaratibu wa kufikisha hoja zao kwa Mamlaka husika, au wajiondoe serikalini kabla ya kupingana na waziri mwenzao.

Alisema Waziri Sitta ni mzoefu na wa siku nyingi, hahitaji kufundishwa, kwa kuwa ameshika nyadhifa mbalimbali serikalini na anafahamu namna za kutoa maoni kwa mawaziri bila kuathiri utaratibu.

Kuhusu Mwakyembe, alisema ingawa ni mpya katika uwaziri, lakini ni mwanasheria wa siku nyingi na anajua utaratibu wa sheria ulivyo, hivyo pia hakuhitaji kufundishwa kuhusu namna ya kutoa mawazo yake kuhusu Dowans wakati akiwa serikalini tena Naibu Waziri.

“Umefika wakati Sitta na Mwakyembe waache kuendesha mambo kisiasa, bali waangalie sheria zaidi katika suala la Dowans,” alisema Chikawe.

Alisema kitendo cha mawaziri hao kumkosoa Waziri Ngeleja, kutokana na kutangaza hadharani kuilipa kampuni hiyo Sh bilioni 94, kimetoa picha kuwa kuna mgongano ndani ya Baraza la Mawaziri.

MAONI YANGU. HUO NDO UKWELI NDANI YA BARAZA LA MAWAZIRI MOTO MTUPU.UKWELI HAUKWEPEKI WASINGEKANUSHANA KAMA WAPO KITU KIMOJA.
 
Dowans ‘yawatafuna’ Sitta na Mwakyembe

SAKATA la malipo ya kampuni ya kufua umeme ya Dowans, limeingia hatua mpya baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utawala Bora, Mathias Chikawe, kusema mawaziri wawili waliompinga Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kutangaza serikali kuilipa
kampuni hiyo, walikiuka utaratibu wa serikali.

Aidha, amewataka mawaziri hao, Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kuacha kutoa maelezo ya sekta zisizowahusu kwani si utaratibu wa utawala bora na ni kuwachanganya wananchi.

Akifafanua kuhusu kauli zilizompinga Waziri Ngeleja, Chikawe alisema mawaziri hao walipaswa kufuata utaratibu wa kufikisha hoja zao kwa Mamlaka husika, au wajiondoe serikalini kabla ya kupingana na waziri mwenzao.

Source: HabariLeo | Dowans ‘yawatafuna’ Sitta na Mwakyembe
 
Kama Chikawe ni kiranja Pinda atakuwa nani? Nadhani hajapewa semina elekezi ya wajibu wake.
 
Sitta na Mwakyembe wanajaribu kuficha aibu. Najua hawachomoki katika hili. They were supposed to foresee the repucation of breaching the Dowans contract. Were are paying Dowans b'se of Bunge fail to foresee!!

It's shame to have those kind of people!

Kama tuna watanzania wa aina hii hivi kweli tutafika? Kwanza ndugu ungetumia lugha unayoielewa vizuri.

1. Mwakyembe, Sitta na Bunge lilishiriki vipi katika kuingia kwenye mkataba na kampuni kama Richmond na baadaye Dowans. hapo ndiyo mwanzo wa tatizo.
2. Kama serikali imeona ilikuwa ni makosa kuvunja mkataba hao wanasheria waliomshauri waziri walikuwa wapi kuzuia uvunjaji wa mkataba?
3. Hivi unaweza kuwaleta hapa wakurugenzi wa dowans walipwe mbele ya kadamnas??????
4. Hoja tuliyonayo ni suala la Chikawe kuwakemea Sitta na Mwakyembe - Kwa mamlaka gani aliyonayo????? Angekuwa anajua wajibu wake angemfuata boss wao (Rais) na kumweleza kwamba mawaziri wako wanafanya ndivyo sivyo.
5. Nchi inahitaji ukombozi lakini baadhi ya wananchi kama hawa wanaturudisha nyuma

MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
mm nazidi kushangaa sana tena Nilidhani Chikawe asingeweza kusema haya kwan inaonesha dhahiri kabisa kuwa hana uchungu wowote na analinda kibarua chake. Jambo linajulikana toka mwaka 2007 na ukweli upo wazi kwanini wazidi kuhangaika na kusubiri baraza amabalo halijaitishwa.Chikawe uelew wko ni mdogo huwezi kusoma alama za nyakati? unapozungumza jua unazungumzia pesa zetu kwa hiyo ulitaka wakae kimya na muyamalize kimya kimya siyo?.tuna hasira sana na watu ambao hawana uchungu na nchi hii.Inauma sana kuona watu kama hawa wanafanya ya kwao.
 
Tatizo la kukariri na kusema kama KASUKU.

huyu Chikawe aishie zake ndio wale wale tu DOWANS share holders.

kwanza katokea wapi huyu jamaa? mbona haeleweki eleweki?
 
Sasa Chikawe na wewe si ungewaambia kimyakimya wao wenyewe mbona na wewe umeenda kwenye vyombo vya habari sasa!!!!

Ungewaita na uwape ushauru huo kimyakimya!!!kwa mtazamo wangu na wewe umetereza au umetumwa uwasafishe watu kwa mjadala huo!
chikawe ameongelea mambo ya utawala bora ambayo ndio wizara yake hivyo ana haki ya kuiongelea hadharani.

hao anaowasema wamekiuka taratibu za utawala bora.
 
Yaani huyu chikawe nae yupo upande wao kumbe. kweli mafisadi ni soo, mawaziri wanatetea utadhani ndio kazi iliyowaweka hapo. kila mtu anaongea na hapa tunaweza kuwatambua waliopo kwenye payroll. ukiwa kimya mgao unakupita!!!
 
QUOTE=Jenifa;1495466]chikawe ameongelea mambo ya utawala bora ambayo ndio wizara yake hivyo ana haki ya kuiongelea hadharani.

hao anaowasema wamekiuka taratibu za utawala bora.[/QUOTE]

kuilipa dowans ni utawala bora?? mbona wanaokubali hawaonywi. sitta na mwakyembe wametoa maoni yao kama wahusika wa kamati ya bunge iliyochunguza richdowns.
 
chikawe ameongelea mambo ya utawala bora ambayo ndio wizara yake hivyo ana haki ya kuiongelea hadharani.

hao anaowasema wamekiuka taratibu za utawala bora.

kuilipa dowans ni utawala bora?? mbona wanaokubali hawaonywi. sitta na mwakyembe wametoa maoni yao kama wahusika wa kamati ya bunge iliyochunguza richdowans.
 
kiduku+jk.jpg


Rais Mwizi aende Chalinze kucheza mdundiko atuachie wenyewe tuijenge nchi yetu.
Tuwasafishe mafisadi papa na aiache Tanzania kama ambavyo aliikuta.

Mh. Akacheze KIDUKU
 
Mh. Akacheze KIDUKU

Mimi bado nasimamia palepale kwamba chikawe alitakiwa awaambie kimyakimya sio kuita press conference so naye ana makosa kwa hiyo asiwalaumu wao kuongea kwenye vyombo vya habari tatizo la hili baraza kila mtu ni msemaji na hali hii haitotulia kamwe mpaka mkuu mwenyewe wa nchi awe na msimamo na kwa sababu yupo kimya ndio maana kila mtu anafyatuka na lakwake leo jumamosi mpaka jumamosi ijayo unaweza kuta yametoka matamko 1000 toka kwa mawaziri tofauti mie nilidhani ishu hii ingeitisha kikao cha baraza la mawaziri haraka sana ila cha ajabu bado yupo kimya sasa sijui anawaza nini??
 
wewe si ndio ***** kabisa.mbona unapiga kelele hazarani?Si ungefuata utaratibu unaowashauli? Au unatafuta umaarufu.
 
Back
Top Bottom