WAHESHIMIWA WOTE WA CHELSEA FC.
KWA HESHIMA 'MLIYONIPA' ACHENI TUANZE UCHAMBUZI WETU KUELEKEA MECHI YETU YA JUMAMOSI.
CHELSEA FC vs EVERTON...
SEHEMU YA KWANZA - UIMARA WA EVERTON FC.
Katika idadi ya mechi za chelsea vs everton...chelsea fc imeshinda mara nyingi zaidi.
hata hivyo katika miaka ya hivi karibuni vijana hawa wa mjini Liverpool; na ambao ndo walioizaa Liverpool fc wamekuwa wagumu sana kufungika. Kama mjuavyo tumekuwa tukishinda kwa tofauti ndogo sana ya magoli kwenye mechi zetu vs Everton fc.
mfano: msimu ulopita walitunga kwao na sisi tukawafunga kwetu. Ikumbukwe kwamba katika msimu ulopita CHELSEA FC haikufungwa na timu yoyote ya top 5 isipokuwa Everton.
Everton hii ya Roberto Martinez ni tofauti sana na Everton ya d.Moyes..
Huyu kocha Martinez ni kocha mjanja, anajua jinsi ya kudhibiti timu kubwa tofauti sana na Moyes.
Mfano 2. r.Martinez alipokuwa kocha wa Wigan Athletic alichukua ubingwa wa kombe la FA. timu yake ilishuka daraja na kombe lao la FA.
Everton fC, inacheza mpira mzuri wa haraka na wanatumia sana mashambulizi ya pembeni. Kinachowasaidia sana ni wepesi wa wachezaji wao wa mbele hasa Kevin Mirallas na Steven Naismith..bila kusahau 'mwili nyumba' Romelu Lukaku, jamaa ana zaidi ya kilo 100. 'the big # 9.'
Everton Fc, wanacheza mfumo wa 4-3-3..kule mbele wanakuwa Lukaku,Naismith na Mirallas..
Katikati wanasimamaa; Gareth Barry, James Mc Cathy, na Steven Pienaar..
mabeki: Baines{kushoto}, Coleman{kulia}, kati Jagielka na Distin...
kipa wao uwezo wake unajulikana..Tim Howard..
Mechi ya jumamosi itakuwa na ushindani wa kutosha...