Jana sikuangalia mpira nilikuwa safarini ila kwa maoni ya mashabiki na maeelzo muhimu ya kilichojiri mimi naona makosa makubwa mawili
1) Cucurella kaizamisha mazima Chelsea jana, hakutakiwa kumkamata yule mshambuliaji Wilson, hata angefunga tungekuja kurudisha na inshalla tungefunga la ushindi. Poor decision making kwa mchezaji mzoefu kama Kuku
2) Kosa la pili ni la kocha la team magement, kwenye Line-up ile, Neto hakutakiwa kabisa kucheza kwa sababu alicheza vibaya sana mechi na Man city, badala yake, Estevao alitakiwa kuwepo na Garnacho sub ya second half. Sub ya Hato kwaa kumtoa Andrey Santos ni uamuzi wa kijinga sana, yeye ndiye tegemeo la kuweka balance kuwin mipira pale katikati wakisaidiana na Caicedo. Palmer angetolewa badala yake au hata Delap Chelsea ingekuwa na balance nzuri kama striker ndie angetoswa. Tumsamehe bure kwa sababu ni kocha wa Academy tu
Mambo mazuri kwa mechi ya jana, Palmer anaonyesha kuanza kurudi mdogo mdogo kwenye fitness yake.
Jambo baya: Chelsea ni ya 8 Man U, Newcastle na Brenford wakiwa juu yetu. Hata hivyo muda kama huu msimu uliopita Chelsea ilikuwa napoints 31 katika mechi 21 na kushika nafasi ya 8. Hii ni duplicate ya msimu uliopita. Msimu uliopita tulifanya vibaya December na Jan kwa sababu Nicolaous Jacson na Palmer walikuwa majeruhi. Safari hii Colwill naPalmer walikuwa majeruhi na Colwil bado kurudi. Palmer fitness bado haijarudi, Pia Jackson hatunaye na pengo lake ni dhahiri hata kama haters watakataa, Pressing ya Jackson, positioning yake na uwezo wa kuondoka na mpira na kuwachezeshga wenzake unakosekana sana. Joao Pedro, Delap hawawezi kufany hivyo vitu
Maoni yangu:
Chelsea waingie sokoni kumnunua striker na CB. Yule striker wa Brentford Igo Thiago Chelsea ilipe hata mil 70
Pia Tunahitaji CB, Kumtegemea Tosin na Chalobah ni aibu kubwa na hawa wamiliki roho ngumu kila mechi wapo, tumecheza mechi 5 hatujashinda hata moja, form yetu iko kama ya Burnley iliyo kwenye nafasi ya 19