Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Ila kwenye makocha waliofanikiwa hawa watoe aiseee Ole Gunnar Solskjær,Julian Nagelsmann & Mikel Arteta. Kupeleka timu big4 ni mafanikio?
Amesema kuwa timu inayopigania mataji, ukilinganisha na timu ilipotoka. Mbona huelewi simple logic wewe
 
Ila kwenye makocha waliofanikiwa hawa watoe aiseee Ole Gunnar Solskjær,Julian Nagelsmann & Mikel Arteta. Kupeleka timu big4 ni mafanikio?
Unadhani ni rahisi hayo mafanikio. Kuna timu hazijawahi hata kucheza uefa.

Kuna hizo timu kubwa kutokushiriki uefa tu inapoteza thamani.

Jiulize pamoja na Arsenal kutokuchukua ubingwa kwa nini bado inakuwa ni timu bora zaidi.

Usikariri sana.
 
Ila kwenye makocha waliofanikiwa hawa watoe aiseee Ole Gunnar Solskjær,Julian Nagelsmann & Mikel Arteta. Kupeleka timu big4 ni mafanikio?
Tofauti na hao waliobeba makombe, Arteta na pia Liam Rosenior wanaikuta timu iko hovyo kabisa, so wanatakiwa kujenga na kuweka mentality ya ushindi, ukatili, kucheza kama timu, nidhamu, mbinu, akili na vitu vingi
 
Jana sikuangalia mpira nilikuwa safarini ila kwa maoni ya mashabiki na maeelzo muhimu ya kilichojiri mimi naona makosa makubwa mawili
1) Cucurella kaizamisha mazima Chelsea jana, hakutakiwa kumkamata yule mshambuliaji Wilson, hata angefunga tungekuja kurudisha na inshalla tungefunga la ushindi. Poor decision making kwa mchezaji mzoefu kama Kuku
2) Kosa la pili ni la kocha la team magement, kwenye Line-up ile, Neto hakutakiwa kabisa kucheza kwa sababu alicheza vibaya sana mechi na Man city, badala yake, Estevao alitakiwa kuwepo na Garnacho sub ya second half. Sub ya Hato kwaa kumtoa Andrey Santos ni uamuzi wa kijinga sana, yeye ndiye tegemeo la kuweka balance kuwin mipira pale katikati wakisaidiana na Caicedo. Palmer angetolewa badala yake au hata Delap Chelsea ingekuwa na balance nzuri kama striker ndie angetoswa. Tumsamehe bure kwa sababu ni kocha wa Academy tu

Mambo mazuri kwa mechi ya jana, Palmer anaonyesha kuanza kurudi mdogo mdogo kwenye fitness yake.

Jambo baya: Chelsea ni ya 8 Man U, Newcastle na Brenford wakiwa juu yetu. Hata hivyo muda kama huu msimu uliopita Chelsea ilikuwa napoints 31 katika mechi 21 na kushika nafasi ya 8. Hii ni duplicate ya msimu uliopita. Msimu uliopita tulifanya vibaya December na Jan kwa sababu Nicolaous Jacson na Palmer walikuwa majeruhi. Safari hii Colwill naPalmer walikuwa majeruhi na Colwil bado kurudi. Palmer fitness bado haijarudi, Pia Jackson hatunaye na pengo lake ni dhahiri hata kama haters watakataa, Pressing ya Jackson, positioning yake na uwezo wa kuondoka na mpira na kuwachezeshga wenzake unakosekana sana. Joao Pedro, Delap hawawezi kufany hivyo vitu

Maoni yangu:
Chelsea waingie sokoni kumnunua striker na CB. Yule striker wa Brentford Igo Thiago Chelsea ilipe hata mil 70
Pia Tunahitaji CB, Kumtegemea Tosin na Chalobah ni aibu kubwa na hawa wamiliki roho ngumu kila mechi wapo, tumecheza mechi 5 hatujashinda hata moja, form yetu iko kama ya Burnley iliyo kwenye nafasi ya 19
 
Ila kwenye makocha waliofanikiwa hawa watoe aiseee Ole Gunnar Solskjær,Julian Nagelsmann & Mikel Arteta. Kupeleka timu big4 ni mafanikio?
🤠🤠🤠....unahaha sana mkuu....ngoja anyanyue kwapa msimu huu ndo uelewe show sasa....tunawakumbusha zimebaki siku kadhaa tukutane tena
 
Niliwahi kusema zike mechi tulizokua tunapoteza kwa complications za Maresca gharama yake ndio hii sasa. Tunaanza round ya pili kwa ugumu wakati ambao timu nyingine zimeshapiga hesabu zao sawasawa. Sisi ndio tunakua wagawa point na top four ndio tushatoka
 
Si
Niliwahi kusema zike mechi tulizokua tunapoteza kwa complications za Maresca gharama yake ndio hii sasa. Tunaanza round ya pili kwa ugumu wakati ambao timu nyingine zimeshapiga hesabu zao sawasawa. Sisi ndio tunakua wagawa point na top four ndio tushatoka
Mwaka juzi jan tulikuwa namba 10 wakati wa Januari
League Position
  • Position: 10th
  • Points: 28
  • Goal Difference: +2
Match Record (21 Games)
  • Played: 21
  • Wins: 8
  • Draws: 4
  • Losses: 9
Mwaka jana January baada ya mechi 21 tulikuwa namba 5 kwa points 37

League Position
  • Position: 5th
  • Points: 37
  • Goal Difference: +15
Match Record (21 Games)
  • Wins: 10
  • Draws: 7
  • Losses: 4
  • Goals: 41 scored, 26 conceded
Mwaka huu January baada ya mechi 21 tuko namba 8 kwa points 31

League Position
  • Position: 8th
  • Points: 31
  • Goal Difference: +10
Match Record (21 Games)
  • Wins: 8
  • Draws: 7
  • Losses: 6
Tumefanya vibaya msimu huu
Mwaka jana Maresca alichaji timu kuanzia March hadi mei mechi kama 14 tlishinda 12
Sijui kama msimu huu tutaweza kuchaji tena na kocha mgeni, mchanga. Changamoto ni kubwa kuliko msimu uliopita
1767866098000.png
 
Unadhani ni rahisi hayo mafanikio. Kuna timu hazijawahi hata kucheza uefa.

Kuna hizo timu kubwa kutokushiriki uefa tu inapoteza thamani.

Jiulize pamoja na Arsenal kutokuchukua ubingwa kwa nini bado inakuwa ni timu bora zaidi.

Usikariri sana.
Kupeleka timu big4 ni mafanikio gani?! Ni utapeli, kama ni hivyo angeorodhesha makocha wote ambao walishapeleka timu big4.

Yaani uulizwe kati ya City na Arsenal ipi bora, useme Arsenal?! Ubora wa Arsenal upo kwnye nini? Kwenye kugombea big4?
 
Amesema kuwa timu inayopigania mataji, ukilinganisha na timu ilipotoka. Mbona huelewi simple logic wewe
Mbona kila timu inaenda kwnye mashindano kushindania mataji?, huyo tapeli kila siku anawadanganya na wameshakua kama mazuzu wake.
 
🤠🤠🤠....unahaha sana mkuu....ngoja anyanyue kwapa msimu huu ndo uelewe show sasa....tunawakumbusha zimebaki siku kadhaa tukutane tena
Nyie kubeba hamuwezi, kama una hivyo fikra zitoe usije ukapata kisukari mana chance y nyie kukosa ni kubwa kuliko kupata.

Ugopa sana kocha anaevaa miwani, mtapgwa mchakae.
 
Nyie kubeba hamuwezi, kama una hivyo fikra zitoe usije ukapata kisukari mana chance y nyie kukosa ni kubwa kuliko kupata.

Ugopa sana kocha anaevaa miwani, mtapgwa mchakae.
Uzuri ni kwmba ndani ya siku chache tunawafata pale kwenu🤠🤠🤠....makonzi ya ulimi ni lazima yatembee....Kocha avae miwani au Dera sisi hayatuhusu....kuwadunda kuko palepale....na safari hii atawatungua Kai mikazo
 
Matokeo ya mechi zilizopita 10 za Chelsea:
🟥 Leeds United 3-1 Chelsea
⬜ Bournemouth 0-0 Chelsea
🟥 Atalanta 2-1 Chelsea
🟩 Chelsea 2-0 Everton
🟩 Cardiff City 1-3 Chelsea
⬜ Newcastle 2-2 Chelsea
🟥 Chelsea 1-2 Aston Villa
⬜ Chelsea 2-2 Bournemouth
⬜ Manchester City 1-1 Chelsea
🟥 Fulham 2-1 Chelsea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom