Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Mtalaumu wachezaji mpaka mchoke, tatizo la Chelsea liko kwa Boehly na genge lake lote. Boehly na genge lake toka wameinunua Chelsea plani ama maono yao yako katika biashara ya kununua na kuuza wachezaji.

Ndio maana leo hii Chelsea ina nunua wachezaji wa hovyo kuwahi kutokea hapo kabla. Lengo lao ni kuwaongezea thamani na kuwauza kwa faida hapo baadae. Huyu Boehly hala maono ya Chelsea kuwa mshindani katika michuano inayo shiriki, ilikuwa ni kosa kubwa sana kumuuzia timu yule tapeli.

Chelsea ya sasa kuanzia kocha mpaka wachezaji wote ni matakataka, huo ndio ukweli mtupu ukubali ama ukatae utajua wewe.
 
Kocha uwezo mdogo
Screenshot_20250126_223928_Instagram.jpg
 
Unaambiwa yule mwarabu mechi ya kwanza TU kaanza kuwatoa chelsii kamasi
 
Mtalaumu wachezaji mpaka mchoke, tatizo la Chelsea liko kwa Boehly na genge lake lote. Boehly na genge lake toka wameinunua Chelsea plani ama maono yao yako katika biashara ya kununua na kuuza wachezaji.

Ndio maana leo hii Chelsea ina nunua wachezaji wa hovyo kuwahi kutokea hapo kabla. Lengo lao ni kuwaongezea thamani na kuwauza kwa faida hapo baadae. Huyu Boehly hala maono ya Chelsea kuwa mshindani katika michuano inayo shiriki, ilikuwa ni kosa kubwa sana kumuuzia timu yule tapeli.

Chelsea ya sasa kuanzia kocha mpaka wachezaji wote ni matakataka, huo ndio ukweli mtupu ukubali ama ukatae utajua wewe.
Sikubaliani na wewe
Hawa wachezaji wengi wa Chelsea wanatakiwa na timu kubwa kubwa
Matakataka pale ni wachache sana na hawawezi kuichafua squad nzima. Wachezaji wengi pia hawana uzoefu akiwemo kocha na bodi, SDs na wamiliki
Hii squad akip[ewa kocha anayejua kutumia vipaji inaweza kutinga top 4 hata bila kuwanunua wengine
Tukinunua striker na CB wazuri tunaweza kupigania kombe, lakini sio na huyu Maresca, hana uzoefu kabisa na anaonekana hajali
 
Hivi angekubali kutua mjini Merseyside, Anfield pale ingekuaje cop? 😂😂
Huyo bado anasumbuliwa na wenge la kuwanyang'anya Caicedo, atamchafua anavyotaka ila kelele za mlango hazimnyimi Caicedo usingizi
 
Tangu mwanzo timu imenunuliwa nilisema management ni mbovu katika uendeshaji wa timu.

Huwezi kununua Toyota vits ukataka ikimbie kama Subaru, uliona wapi?

Hiyo vits hata uibadilishe rims, ufunge mziki mzigo, maspoila, uandike ubavuni subaru evolution 12 bado spidi yake itabaki ile ile ya vits.

Wamiliki + SD Walitusajilia wachezaji kibao vits, matokeo yake mtaishia kutoa lawana kila siku, mkitaka wawe Subaru.

Kocha mwenyewe ni Engine ya kicarry iliyofungwa kwenye Fuso (The Blues).
Unajua hawa wamiliki wanataka waue ndege kwa jiwe moja. Wanataka kuwa kama Brighton kwa kununua chjipukizi na kuwauza bei ya juu lakini hapo hapo watengeneze timu ya kubeba makombe baada ya miaka 3-5. Sasa si9si mashabiki kwa vile sio wawekezaji hatuna habari na hilo lengo la kufanya biashjara ya faida. Sisi tunachojali ni kubeba makombe asubuhi kama ilivyo desturi ya Chelsea kitu ambacho hakityawezekana. Tuwe wavumilivu hadi 2026/27 ndipo tuanze kuwaza makombe hata yale ya mbuzi
 
Hii ina maana kwamba sisi mashabiki tumekuwa hatumtendei haki Enzo Maresca.

Kocha huyo alikuwa na kikao na bodi siku moja kabla ya jana ambapo walijadili kuhusu usajili wa wachezaji na matokeo mabaya ya hivi karibuni.

Alitaja hitaji la mshambuliaji mahiri tena, angalau kwa mara ya tatu sasa, na anaamini hatuna wasifu katika nafasi ya 6.

Kwa kifupi, ameitaka bodi kwa mara ya tatu kusajili mshambuliaji mwenye uwezo wa kumalizia nafasi zinazotengenezwa.

Pia ameomba kusajiliwa kwa kiungo mkabaji katika namba 6.

Taarifa zinaeleza kuwa kocha huyo huwasifu na kuwalinda wachezaji kwenye vyombo vya habari tu, lakini mambo ni tofauti sana nyuma ya pazia.

Kwa upande wao, wakurugenzi wa michezo wanaamini kuwa hakuna mshambuliaji mzuri sokoni wakati wa dirisha hili la Januari hadi dirisha la kiangazi.

1738052991005.png
 
Bournemouth hawajapoteza tangu Dean Huijsen (19) na Illya Zabarnyi (22) walianza kucheza pamoja michezo 10 iliyopita.

Mhimili wa walinzi wachanga zaidi katika Ligi ya Uingereza wanaosimama kidete kulinda lango la timu yao isifungwe kiholela.

1738054972798.png
 
Liam Rosenior juu ya Santos:

"Andrey atakuwa na taaluma nzuri ya mpira. Andrey anacheza kama ana umri wa miaka 32. Ninamwita Dunga. Yeye ni Mbrazil lakini hachezi kama mbrazili.

Yeye ni mjanja na makini sana na takwimu zake ziko juu sana, kwa suala la kufunga mabao, kushinda mipira ya juu. Atakuwa na taaluma bora."
~
@TheAthleticFC

1738058632566.png
 
Sporting directors ndio wanampanga Sanchez kila siku golin?
Mashabiki wengine wanaamini kuwa Kocha wa Makipa, Ben Roberts ndiye mwenye shinikizo la Sanchez kuwa golkipa namba 1.

Ben Roberts alikuwa ni kocha wa makipa huko Brighton
Kaja kuwa kocha wa makipa katika Chelsea (chini ya Potter na Pochettino)
Sasa amepandishwa cheo na kuwa Mkuu wa Kipa wa Kimataifa.👀

Yeye ndiye mwenye msukumo nyuma ya uhamisho wa Sanchez Chelsea wakati huo huo sababu kwa nini Sanchez anaendelea kuwa kipa wa kwanza hata baada ya performance yake kuwa mbaya wiki hadi wiki.
1738237571213.png
 
Nani aliyemsajil ???? Kipq anasajiliwa ashapoteza namba kwa team km brighton kwa sabab ya makosa yake
Nikurekebishe mkuu.
Kapewa demotion na Roberto De Zerbi kwa sababu ya makosa yale yale yan ayojirudia. Katika umri wake wa miak 27 tusitegemee atabadilika
 
The Blues kwa sasa haina tofauti na Brighton, Bournemouth. Imekuwa timu ya daraja la kati kiushindani. Imekuwa timu ya kusaka vipaji kununua na kuuza kwa faida.
Ondoa Borenamouth wao wako vizuri
Chelsea imeiga model ya Brighton na wamiliki wa Chelsea walishakiri kuipenda model ya Brighton
A mid tgablke team yenye kulipa wachezaji mshahara mdogo lakini inapata faida kubwa.
Ndio maana imekazana kuwanunua wachezaji wadogo hata ambao hawatapata nafasi ya kucheza ili iwauze.
Ila hawajui kuwa mchezaji asipopata nafasi ya kucheza hakun a timu itakayomtaka.
Mchezaji akicheza sana na kuonyesha uwezo wake ndipo timu zitamfuatilia.
Caicedo tuliweza kumfuatilia Brighton kwa sababu alikuwa akicheza kila mechi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom