Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Unafki umeanza lini? 😄😄😄 kwetu umekuja kusema Chelkenge wanasema watatupiga nyingi. Nakuja huku kuwachimba biti nakuta umesema sisi tumesema tutawapiga nyingi

😂😂
 
Bila mchango wa Cole Palmer wa mabao 29 kwenye Premier League, Chelsea wangekuwa kwenye eneo la kushushwa daraja 😬

Mauricio Pochettino amewataka wachezaji wake kuthibitisha kuwa sio tu 'Cole Palmer Football Club'.

Je, The Blues wamemtegemea sana nyota wao mchanga Cole Palmer kwenye ushindi wa mechi zake?

Leo kuanzia saa nne usiku tutajua pale Emirate

1713890324722.png
 
Imeripotiwa kuwa Pochettino hachukulii maanani sana juu ya tatizo la uchezaji wa mpira (IQ ya mpira) wa Mudryk na tena hamwamini Mudryk katika safu ya ulinzi na anaamini hana akili nzuri.

Nadhani unaweza kudai kuwa ni kazi ya Pochettino kuboresha huo udhaifu, lakini tena tumesikia kuwa Pochettino hufanya vizuri sana katika kuboresha vipaji vya wachezaji wachanga. Hata ikitokea Mudryk akauzwa nadhani Pochettino atafurahia sana. hii itakuwa mbaya sana kwa kocha ambaye kakaa muda wote huo na mchezaji mwenye kipaji na aliyefanya vizuri kwa makocha wengine ila yeye akashindwa.

Ndiyo, ameshindwa kwa sababu Inaonekana kama matatizo ya Mudryk, sio ya Pochettino na hatapata msaada wowote wa kuendelezwa kimpira kutoka kwake au kwa wasaidizi wake. So hii dhana ya kwamba Pochettino ni mzuri kwenye kukuza viapji vya wachezaji wachanga ni upuuza uliotukuka na kwamba hata akina Harry Kane na Dele Ali walikua vizuri kwa uwezo wao binafsi na ndio uliwafanya wakafika hapo walipo.

Kufeli kwa Mudryk ni taswira ya wazi ya mapungufu ya Pochettino. Ni kama taswira ya jinsi kocha wetu anavyofanya kazi katika kukuza vipaji. Ikiwa hawezi kuwa na imani na mchezaji mchanga mwenye kipaji kama Mudryk, kwa njia kama hii, tutawezaje amini kuwa atakuza vipaji vya akina Palmer, Paez, Angelo, Santos, Carney, Colwill, Jackson, Omari na wengineo na wale watakaosajiliwa?
 
Watu wengi wanawabeza hawa watu
Arne Slot
Ruben Amorim
Xabi Alonso
Sebastin Hoeness wa Stuttgart

Hawa wote niliowataja nibora na wazuri kuliko kocha tulienae sasa Poch
 
Watu wengi wanawabeza hawa watu
Arne Slot
Ruben Amorim
Xabi Alonso
Sebastin Hoeness wa Stuttgart

Hawa wote niliowataja nibora na wazuri kuliko kocha tulienae sasa Poch
Wanatoa Hoja gani ya kumbeza Alonso?
 
Kwa hiyo huu uzi ni lawama na kulalamika tu ila mkija majukwaa ya timu zingine mnajitunisha 🤣🤣🤣🤣

Pathetic
 
Oya wanangu wa Darajani leo tutoe wasiwasi leo Arsenal tunamla vizuri tu wala hatotusumbua ili tumshushe Manure nafasi ya 8 huko hata Conference League asishiriki.
 
Oya wanangu wa Darajani leo tutoe wasiwasi leo Arsenal tunamla vizuri tu wala hatotusumbua ili tumshushe Manure nafasi ya 8 huko hata Conference League asishiriki.
Pochetino ashabet😂 kwa combo ya badiashil n disasi

Muwaombee manure
 
Yuko team ndogo + sio top coach😂😂😂😂
Watu wana masihara. Hawaoni kazi anayoifanya? Kuitransform team kua ya ushindani, anasababisha hadi top talents za timu zigome kuuzwa zinabaki pale pale
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom