[emoji117]Chelsea yangu bora ni ile ambayo ilianza msimu na kuongoza ligi kabla JAMES na CHILWELL kuumia.
[emoji117]JAMES na CHILWELL waliongeza nguvu kubwa sana kwenye ushambuliaji, ndio maana wakati ule Chilwell, James na Azpi walifunga magoli mengi kuliko washambuliaji wetu kule mbele.
[emoji117]James na Chilwell walivyopata injuries + Corona + injuries za wachezaji wengine + uchovu, timu ilipitia wakati mgumu sana kiushindani, mwisho kitu kizito kikatua kichwani baada ya Roman kutangaza anauza timu + vikwazo
[emoji117]Pamoja na changamoto zote hizo tumejitahidi kufika fainali mbili mfulilizo (CARABAO + FA), tunapambana kumaliza TOP 4. HONGERENI SANA
[emoji117]Binafsi naamini safu ya USHAMBULIAJI + KIUNGO imetuangusha sana msimu huu. Safu ya ULINZI nitailaumu kwa mistake ndogo ndogo ambazo utaziona kwa kuwa tulishindwa kufunga magoli mengi.
[emoji117]Kama msimu ujao tutaenda na viungo na washambuliaji hawa hawa tusahau kuchukua kombe la EPL mbele ya LIVER na CITY. TUSAHAU KABISA.
[emoji117]Ili kuboresha viwango vya wachezaji waliopo ni kuingiza maingizo mapya yenye ubunifu/uwezo mkubwa, nguvu na kasi.
[emoji117]Pale mbele tukipata winga 1 yenye uwezo wa kuassists 10+ na kufunga magoli 10+ anaweza kuwaamsha usingizini Kai, Werner na Lukaku. Winga mpya anaweza leta muunganiko flani ambao unakosekana kwa sasa.
[emoji117]Pale katikati tukipata kiungo mmoja mkabaji haswa, Kovacic na Kante wataoperate vizuri sana very comfortable. Jog, Saul & cheek watupishe.
[emoji117]Pale nyuma usajili wa mabeki sio chini ya watatu.
[emoji117]Kuna blanket la kocha TT tumejifunika nalo hatuoni nje, tunaona kwamba kwa sasa tunao wachezaji wazuri sana ila hawajitumi au viwango vimeshuka.
TUNAJIDANGANYA SANA, WACHEZAJI WETU WENGI WANA VIWANGO VYA KAWAIDA SANA.
[emoji117]Jiulize swali ni wachezaji wangapi wa THE BLUES wanapata namba kikosi cha CITY au LIVER?
[emoji117] Ile safu yetu ya ushambuliaji kule mbele hakuna mchezaji hata mmoja mwenye uwezo wa kuingia kwenye kikosi cha CITY au LIVER achilia mbali viungo na mabeki.
[emoji117] TUJENGENI TIMU YETU [emoji123]
#Pride of London