OllaChuga Oc
JF-Expert Member
- Jul 4, 2016
- 21,935
- 25,245
Kwa muktadha huu basi na msimu ujao tunaenda tukidena dema hivi Hadi mambo yakae sawa tusubiri misimu angalau miwili ipite ..si ndio mkuu?? Hapa naona Chelsea yetu ikipotea zaidi dah😭😭 tutarudi kama liverkuku ya kipindi klopp anaikuta jinsi ilivyo struggle Hadi Sasa tunaona imeiva haswa.Na TT amesema tajiri mpya hawezi kuja na kutoa haraka £250M za usajili. Lazima kwanza aweke watu wake anaowaamini kwenye uongozi wa kusimamia pesa yake vizuri.
Kwahiyo TT amesema dirisha la usajili la kiangazi litakuwa gumu sana kwa hali ilivyo mmiliki mpya + mfumo mpya wa uendeshaji club + kikosi kibovu cha kuboresha
TT tunaamkubali sana lakini naona CV yake aliyojenga kwa muda mfupi unaweza kuchafuliwa na hii situation tunayoitia Sasa. Angalia Rudger anasepa, Christiansen na yeye mbioni kusepa, usajili kwetu ni kuzungumkuti ..hatuna hata jeuri ya kwenda sokoni sasa ..labda tuwarudishe akina Tammy, broja na madogo wengine tuanze nao taratibu huku tukitegemea matokeo mazuri mbeleni huko.
#CFC💙💙💙
