Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Hiu mpira tuliocheza mpaka tunascore hizi goal mbili hapa mwisho ndio mpira tunatakiwa kucheza tukikutana na timu za calibre ya Liverpuru.

Ni mwendo wa kupiga mawe tu.

Tumekosa goal mbili za wazi kabisa.
Hii game iliisha kipindi cha kwanza kama Pulisic angeweka kambani zile mbili.

Yaani Liverpool wangekuwa watumwa na pressure kubwa, ila hii come back imependeza mno

Tushuhudia game ya maana sana kipindi cha pili.
 
Hivi jamani Chalobah pale alikuwa anataka kutuonyesha mbwembwe zipi?. Mpira uko level ya goti yeye anataka kuupiga kichwa kwa sakarasi style. Poor decision making.
 
Defender pembeni ya Chelsea inakuwaje tena?

Mendy atachoka kuokoa sasa, kuweni imara nyie...!
 
Kufika sasa ni kichaa pekee ndo atoamini man city sio bingwa.
Man City ana faida, ila kusema kuwa anaweza asiwe bingwa ni kichaa, hapo hauko sawa. Mpirani chochote huweza kutokea. Ilikuwa the same kwa Chelsea kabla ya majeruhi na ma Covid kuvuruga kila kitu. So Yeah, wana faida ambayo waki maintain watakuwa mabingwa. Ila michezo inaendelea bado!
 
Leo Makipa walikuwa vizuri sana.
Kwa Chelsea Rudiger, Kante, Pulisic na Kovacic wamekuwa fire sana
Liverpool: Kanoute, Jotta, Salah na Mane ni fire sana

Game imekuwa njema sana. Niwatakie usiku mwema!
 
Kufika sasa ni kichaa pekee ndo atoamini man city sio bingwa.
Chelsea yangu mimi nilishaiondoa kwenye ubingwa. Nilishasema Chelsea ikidrop point mechi tatu december ubingwa tena basi.
Alidrop kwa Westaham, ikaja kwa Everton, ikaja kwa Wolves mwisho kwa Brighton. December tu kadrop point 9 kwa mechi 4 halafu unategemea aje kushindana na City aliyeshinda mechi 11 mfululizo na bado anaendelea kushinda.

Chelsea kwa sasa waungane tu bila kuona aibu na Spurs, Arsenal na Liverpool kwenye top 4
 
Halafu kuna kipindi Chelsea fans wanakuambia mendy hafai bora kepa nahis wanakuwa wanatania tu na sikweli
Mendy kuna wakati anaboa, hata goli la Salah hakuweka juhudi yeye na Alonso na Chalobah.

Mchezaji akishakuwa mzuri haina maana ataendelea kuwa mzuri wakati wote. Yule Mendy wa mwanzo wa msimu si huyu wa sasa. Yule Mendy aliyetupa UCL sio huyu wa sasa, labda kama wewe hufuatili kwenye details
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom