REPOSTED
Mashabiki wenzangu wa THE BLUES bado tuna mlima mrefu sana kumaliza TOP 4 kutokana na changamoto inayotukabili kwa sasa ya uchache wa ufungaji wa magoli.
Nadhani kwa sasa katika jambo linamuumiza kichwa kocha wetu TT ni jinsi gani atawaboresha wafungaji wetu wafunge magoli mengi.
1. Abraham - 6
2. Werner - 4
3. Mount - 3
4. Giroud - 2
5. Odoi - 3
6. Ziyech - 1
7. Harvetz - 1
8. Pulisic - 1
Tunahitaji wafungaji wetu waanze kufunga magoli mengi zaidi kule mbele atleast timu iwe na asilimia kubwa ya kushinda mechi.
Hivi vigoli vimoja vimoja vya Azipu, Jognho (Penati) na Alonso yawe magoli ya nyongeza, kuna siku vitakosekana tuanze kutafutana hapa.
Binafsi naona tuna hali mbaya sana kiufungaji, bado hatuwezi kujigamba tunaweza kutamaliza TOP 4 wakati wafungaji wetu wanakata viuno kule mbele.
Werner, Giroud, Ziyech, Odoi, Pulisic, Abraham waamke usingizini tunahitaji mabao na sio kula mshahara bure.