LEICESTER CITY 2-2 CHELSEA, Premier League: Post-match reaction.
By Mlanzi
Bonge la performance kutoka kwa man of the match Antonio Rüdiger. Rüdiger anakuwa defender wa kwanza kuchana malinda mala mbili kwa upande wetu Chelsea katika Premier League tangia John Terry afanye hivyo dhidi ya Fulham mwezi April mwaka 2013; mabao yote yalikuwa ya kichwa pia.
Juhudi safi kutoka kwa Reece James zinahitaji Striker mzuri, zinahitaji finisher mzuri. Tammy Abraham anaweza lakini ukweli ni kwamba hana msaada pindi team inahitaji matokeo.
Nashindwa kuelewa malengo halisi ya board, nadhani kama Roman Abramovic amechoka kufanya investments ni bora auze hisa zake alafu amchukuwe Marina na Buck aende nao..!! Nini maana ya ku appeal hiyo transfer ban kwa ku spend pesa nyingi alafu unashindwa kufanya usajili

!
Anyway, first-half hususani dakika chache za mwanzo Chelsea ilikuwa imeutawala mchezo, team ilikuwa ina creat opportunities kibao ambazo zote ziliota mbawa kutokana kukosa umakini upande wa striker.
Leicester waliamka na kuanza kuwa threat, especially katika counter attack. Chelsea ilianza kupoteza momentum na kuanza kupoteza mipira kizembe katika eneo la midfield makosa yaliyopelekea Vardy kutukosa kosa na kumlazimisha Willy Caballero kufanya save moja ya hatari.
Willy Caballero alikuwa kati kati ya lango letu badala ya Kepa Arrizabalaga ambae amekuwa pazia siku za hivi karibuni.
Chelsea tuliendelea kupoteza chances, kupitia kwa Mason Mount, Tammy Abraham, pamoja na Callum Hudson-Odoi wote wakionyesha poor finishing katika hiyo game.
Baada ya kukosa chances katika first half, burudani ilihamia katika second-half ambapo mnyama mkali Antonio Rüdiger alipofunga bao safi kwa header fupi mpira uliokuwa umepikwa na Mason Mount kutokea kwenye corner dakika ya 46.
Speed ya Leicester City iliongezeka huku wakiyatumia makosa tuliyokuwa tukiyafanya katika defense hari iliyopelekea Barnes kuipatia Leicester City bao la kusawazisha dakika ya 54. Matokeo yakiwa Moja moja, team yetu ilionekana kuwa down huku Leicester City wakitumia mwanya huo kufanya attacks za haraka kitu kilichopelekea Chilwell kuongeza bao la pili katika dakika ya 64.
Chelsea tulipoteza matumaini kabla ya AntonioRüdiger kuipandia tena freekick iliyopigwa na Mason Mount dakika ya 71 na kufanya matokeo kuwa mbili kwa mbili.
Uwanjani kulikuwa na mabadiliko manne yaliyokuwa yamefanywa na Frank Lampard kutoka katika league game, Lampard alikuwa amemuanzisha big Willy Caballero mbele ya Kepa Arrizabalaga huku Pedro Rodriguez akianza mbele ya Willian.
Substitutions zilikuwa Willian upande wa Pedro Rodriguez, Mateo Kovačić upande wa Jorginho. Then Ross Barkley upande wa Tammy Abraham.
Kwa matokeo haya Chelsea tunabakia nafasi ya nne kwa tofauti ya points nane dhidi ya Leicester City walioko nafasi ya tatu. Wanaotutuatia tumewaacha points saba na wote wakiwa na points 34.
Next up team itakwenda katika Winter break kwa muda wa week mbili, then tukirejea tutakuwa na games tatu za nyumbani ndani ya siku nane. Tutaanza na Manchester United, Tottenham, na baadae dhidi ya Bayern Munich.
KTBFFH
Sent using
Jamii Forums mobile app