Mawazo, maoni, hoja zinakosolewa kwa hoja. Sio kukashifu, kutukana, kukoseshwa haki ya kuchangia jukwaa hili.
Nilishwahi kuandika kule jukwaa la Arsenal kwamba mashabiki wa timu flani siku zote hawawezi kuwa na mawazo yanayofanana.
Nikatoa sababu kwamba kwenye timu kila shabiki kuna jambo huwa linamvutia na ushabiki wake ndio umeangukia hapo, mwisho wa siku ukionganisha mivuto yote hiyo lengo kuu linakuwa kwa mafanikio ya timu na kubeba makombe.
Nikatoa mfano kuna shabiki wa Chelsea anayeshabikia mfumo na mbinu za kocha.
Shabiki anapenda sana kocha awe na mbinu bora za kushinda mechi na mbinu hizi ziwe zinabadilika kuendana na mechi bila kujali aina ya wachezaji atakaowapanga kwenye kikosi, mwisho wa siku team ipate matokeo mazuri
Kuna mashabiki wanaoshabikia wachezaji kwenye timu. Siku akichungulia kikosi akamuona mchezaji wake flani, hajapangwa, shabiki huyu anakasirika, anaponda mchezaji aliyechukua nafasi anamponda kocha hajui kupanga kikosi n.k
Kuna mashabiki wa Hazard naamini mpaka leo bado wanaumia mioyoni mwao hahahahaha
Kwahiyo mawazo, maoni ya mashabiki yanatolewa kwa kuegemea shabiki ana interest gani kwenye ushabiki wake.
Lakini mwisho wa siku wote wanaitakia timu mafanikio.
Sent using Cash Money Wings