Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Kocha sio mwenye mamlaka kwenye usajili anachofanya ni kutoa list ya wachezaji anaowahitaji na alishafanya hivyo tangu dirisha la usajili lililopita.
Kumsajili ama kutomsajili mchezaji ni maamuzi ya director,Marina Granovskaia ambae ana deal na uhamisho wa wachezaji.
Hana mamlaka lakini ana ushawishi wa kitaalamu, maoni yake yanazingatiwa sana
 
Nan mgeni hapa?????? Mshazoea kukimbilia profile za watu kucheki yasiyowahusu......Nina miaka mitano humu....
Namaanishi sio raia wahapa Mimi nimtanzania
Sisi Watanzani tunaupendo mkubwa sana tunachukuliana kwa Upendo mkubwa sana
Uvumilivu
Ndio maana ninakupenda Sana Kama binadamu mwenzangu
 
Tetesi

Real Madrid inapanga kuwasajili Eden Hazard, 27 na kipa Thibault Courtois, 25, kutoka Chelsea ifikapo mwisho wa msimu. Lakini watasubiri kuona hatma ya Harry Kane wa Tottenham. (Sky Sports)
 
Tetesi

Chelsea wanamtaka mshambuliaji wa Borussia Monchengladbach na Ubelgiji Thorgan Hazard, 24, kujiunga na ndugu zake Eden, 27, na Kylian, 22, huko Stamford Bridge. (Bild - in German)
 
Tetesi

Mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 26, ataitisha pauni 400,000 kwa wiki kuzuia ofa ya Chelsea ili kujiunga na Manchester United. (Sun)
 
Tetesi

NewCastle wana matumaini ya kumaliza kumsaini wing'a wa Chelsea mbrazil Kenedy, 21. (Newcastle Chronicle)
 
736d02235841ca80ca9fc10fa9b6962b.jpg


Serie A
Premier League
Serie A Coach of the Year
PL Manager of the Month
PL Manager of the Season
LMA Manager of the Year
The Beat FIFA Mens Coach 2017

Chelsea Win Percentage: 71.3%

The best man for the job!
 
wazima hapa, nilipotea kidogo kutokana na sehemu niliyokuwepo huko nchini Botswana,
Botswana kwenye bar nyingi story tulikuwa tunapiga ni ujio wa huyu beki kitasa andreas christensean na usajili wa ross barkley.
Ila raia wengi hawamuelewi bakayoko wanasema ikiwezekana atolewe hata kwa mkopo westham or any other weaker team.
Wanadai kwenye match na Barcelona bakayoko akianza tunakula mkono ingawa na mwenyewe bakayoko simkubali ila sio kula mkono kwa Barcelona.
 
Tetesi

Chelsea, Arsenal & Man Utd zamwania Bailey



Chelsea, Manchester United na Arsenal zinataka kuingia vitani kuwania saini ya Leon Bailey, kwa mujibu wa Mirror.
Winga huyo wa Leverkusen anaweza kupatikana kwa ada ya uhamisho ya kiasi cha £40 milioni, ingawa klabu inasita kumuuza.
 
Timu ya daraja la chini Yeovil Town imepangwa na Manchester United kwenye raundi ya 4 ya kombe la FA
Timu hiyo ambayo ipo daraja la pili ilifanikiwa kuiondoa klabu ya Bradford City kwa magoli 2-0 wikendi iliyopita na sasa watawakaribisha United kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Huish Park mwishoni mwa mwezi huu
Pia klabu nyingine ya daraja la chini ya Newport Country, ambao waliwaondoa Leeds United nao watavaana dhidi ya Tottenham mechi ambayo inatarajiwa kufanyika nyumbani kwa Newport
Aidha Liverpool nayo imepangwa na West Bromwich Albion mechi itakayo pigwa kwenye dimba la Anfield, wakati Chelsea ambaye bado ana mchezo wa marudiano dhidi ya Norwich, anatarajiwa kukutana na Newcastle endapo atashinda mechi ya marudiano
Vinara wa msimamo wa Ligi Kuu Manchester City wao wana msubiri mmoja wapo kati ya Cardiff City au Mansfield Town, huku wababe wa Arsenal klabu ya Nottingham Forest watavaana na Hull City
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom