Meneja wa Chelsea Antonio Conte ameeleza ni kwa nini Cesc Fabregas anacheza mechi nyingi msimu huu
Kabla ya mechi tano za mwanzo msimu uliopita, kiungo huyo alikuwa ameanza mechi nne tu chini ya bosi huyo wa Kiitaliano.
Mwisho wa yote, Muhispania huyo alikuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Blues wakishinda taji na kwenye kampeni za 2017-18, Fabregas amecheza mechi 21 katika michuano yote, ikiwa ni pamoja na kuanza mechi 12.
"Nadhani Cesc mwanzoni hakucheza sana, lakini nilikuwa na furaha kwa sababu kupitia kazi anayofanya amejaribu kubadili akili yangu na imekuwa," Conte aliwaambia waandishi.
"Kama utakumbuka ngwe ya pili ya msimu uliopita alianza kucheza mara kwa mara. Sehemu ya kwanza ya msimu niliamua kucheza karibia kila mechi na [N'Golo] Kante na [Nemanja] Matic lakini sehemu ya pili ya msimu nadhani Cesc alicheza mechi nyingi.
"Nadhani alikuwa muhimu sana kwetu kutwaa taji msimu uliopita. Msimu huu ameendelea na kazi nzuri na kujituma na ameonyesha uwezo mkubwa na tabia njema."
Fabregas ametengeneza mabao manne na kufunga mawili katika kampeni za msimu huu.