Yani kila chelsea ikichukua ubingwa wa epl basi msimu unaofuata tunazembea kwenye usajili. Conte amesema anataka wachezaji wengine 4 ili aongeze nguvu kwenye kikosi. Msimu uliopita chelsea ilitumia wachezaji 13 tu kwenye msimu mzima, msimu huu tuna mashindano mengi hivyo itakua ngumu kwa wachezaji tulio nao.
Nadhani umefika wakati sasa mmiliki atafute kocha anayeweza kutumia wachezaji vijana maana chelsea academy na scouting team inafanya kazi nzuri ya kuleta vijana ila timu kubwa hawapewi nafasi. Nawaangalia tammy abraham, loftus-cheek, ake na chalobah kwa umakini msimu huu kisha utagundua jinsi tulivyozembea.
Kwa siku chache zilizobaki nadhani wajitahidi kuongeza angalau mchezaji mmoja kila nafasi ili mambo yawe msawazo. Win,loose aor tie chelsea till i die. Blueblood.
Sent using
Jamii Forums mobile app