Ni kweli unachosema kaka, lakini ukiangalia aina ya wachezaji waliopo kwenye hizo timu bado unaweza kupredict top three, kwa mtazamo wangu, Chelsea, Liver na United ndio watagombea nafasi tatu za juu,
Arsenal wanashida ya Kocha kukosa mbinu za kimchezo hasa ikifikia kipindi hichi cha round ya pili, yeye huwa habadiriki kwa lolote, mfano anapofanyaga sub ya kumwingiza Giroud huwa hamuandalii mazingira ya kuweza kufunga kwa maana ya kubadirisha aina ya mpira anaocheza na kwenda kwenye mpira wa cross ili jamaa apige vichwa, jamaa ni mzuri wa vichwa lakini huwa anafunga kwa bahati na sio kwa malengo
City bado wanashida ya Kocha kuwa mgeni wa league na pia wanashida ya kina toure na Fenarndinho, hao jamaa wana uzito fulani ambao wakipata timu zenye kukimbiza na middle wepesi watapata shida, cha pili cocha bado anaangaika na kupata timu ya kudumu 1st 11, mechi ya mwisho waliyocheza na Hull city, dakika ya 30 tu ya kipindi cha kwanza alishamwita Fenandinho kwenye benchi, Fenandinho alibakia ndani kwa sababu kuna mtu aliumia hivyo ilibidi atoke na Fena akacheza mpaka mwisho, so kocha anaweweseka
Man united kwa sasa wanacheza mind game, Mou anaanza kutumia uwezo wa wachezaji na uwezo wake binafsi, hivyo kwa huo utundu na ubunifu wa Mou timu itafika top 3
Liver wapo fit, pamoja na mapungufu ya hapa na pale ila watafika top 3