Mpaka sasa suluhisho mojawapo ni katiba,katiba ya sasa,kwa mujibu wa nyerere,angeweza kuwa dikteta,nyerere alijizuia,hawa waliomfuata je? Nyerere ndio mzizi wa matatizo ya nchi kiuchumi,kisiasa,kijamii,kielimu na mila kitu,katuachia katiba mbovu,kaiacha Ccm imekaa kinafikinafiki,nchi aliiacha haina taasisi imara japo aliitawala kwa miaka 27,kwa muda wote huo alikuwa kama anatawala Shamba tu....madhara yake ndio haya,hatuwezi kumlaumu kiongozi yeyote bila kupata mzizi wa tatizo....mzizi ni nyerere,huyu aliwafanya wazee wetu wafe maskini,kwa kuua uchumi wa mtu mmoja mmoja,kafanya watanzania wawe wavivu,kaua vyama vya ushirika,ni mtu wa kwanza kuua viwanda vya sekta binafsi,kaua sekta ya Nyumba.....mengine ongezeaYote hayo hayana maana yoyote bila katiba bora inayo akisi maoni ya Wananchi.
Wanabodi,
Hapa simzungumzii mtu yoyote bali nazungumzia hulka za watu wenye tabia za udikiteta katili, kitu kinachoitwa "character assassinations" ndio "modus oparandi" ya madikiteta wote duniani, na huanza kwa kuwa populist kwa kuonyesha heroick actions hivyo kushangiliwa sana kama mashujaa na kupendwa sana na watu!.
Hulka hizo za udikiteta zinatokana na kitu kinachoitwa "deep rooted neurosis" kwa madikiteta hawa kuwa waliteswa sana utotoni!, baadhi yao walikataliwa ndani ya familia, na hii hutokea baba kuhisi mtoto huyo sii wa kwake kwa kumhisi mke alichepuka, mama kamwe hawezi kukiri kuchepuka hata kama ni kweli alichepuka, hivyo baba anakuwa anamtesa sana mtoto, na mama hawezi kuingilia!, mtoto wa aina hiyo anakuwa amekulia katika usongo mkubwa wa mawazo, unaomtia hasira kusoma kwa bidii na huku ana visasi ili kuonyesha mateso hayo ni jambo la kupita tuu, na kweli wengi hufanikiwa, na wakiishafika at the top!, ndipo ile "deep rooted neurosis" ya kumbukumbu ya mateso iliyohifadgiwa kwenye "sub conscious mind" inaibuka na kupelekea kumfanya mtu huyo kuwa katili!, kwa ku inflict pain kwa njia za character assassinations, anaumiza ukiumia yeye ndio anapata furaha!.
Madikiteta wa Roma ya kale, waliandaa michezo ya kupigana ya ma gladiators mnapigana hadi mmoja afe!. yule gladiators mwenye nguvu kuliko wote, anakuja kuletwa pale kwenye Colosium (stadium) na kusakiziwa simba watatu wenye njaa ya siku 7, huku watu wamejaa kushuhudia jinsi binadamu anavyoraruwa na simba huku watu wanashangilia!.
Adolf Hitler yeye alikuwa akinyoosha mistari ya jeshi lake kwa risasi za moto, anayepindisha tuu, anakula hapo hapo!. Idi Amini Dada yeye alikuwa anatumia kikosi kinachoitwa "firing squad", lengo ni kuogofya!.
Hivyo wandugu, tusije wote tukawa washangiliaji wa hiki kinachoendelea tukitaraji tutafika mwisho na wote watanyooka, kumbe huu ukawa ndio kwanza ni mwanzo tuu wa makubwa yajayo!.
Naomba kumalizia kwa msisitizo, kuna aina mbili za madikiteta!. Kuna Madikiteta Katili na Masikiteta wazuri!. Mada hii inawazungumzia madikiteta katili!, hivyo nawaomba wachangiaji msije kuchanganya madawa mkaanza kuwadhania watu humu!.
Namalizia kwa swali, jee wote tunaoshagilia hizi character assassination za sasa, ambazo we take them as "the sweet", jee tuko tayari to "swallow the bitter with the sweet" wakati wa vidonge vichungu ukifika, au tutaendelea tuu kuchagua vidoge vitamu ndio tumeze, lakini vichungu tuteme?!.
Nawatakia Jumatatu Njema.
Pasco
Magufuli hana udikteta wowote. Hata mimi huwa natamani sana siku moja kuwa na dikteta lakini siyo kwa demokrasia hii. CCM bado ipo intact kwahiyo Magufuli ataendeleza sera za chama na si vinginevyo. Hizi ngonjera za kufukuza mawaziri ndiyo mnaziita udikteta? Hivi mbona vitu vya kawaida tu.Ila jamani acheni utani kwa nchi yetu tulikokuwa tumefikia......inatakiwa awepo dikteta mzuri na nadhani huyu jamaa kama anareflect hivyo kwenye huo udikteta ila natakiwa aandae mfumo bora asiwe totally dikteta anatakiwa awaandae na wenzie wamuige au wafanye kama anavyofanya.......namuona Majaliwa kama ameshakamata kasi yake sasa wanaenda sambamba
Ngoja twende hivi hivi tutafika!!!
Wanasema #HuuMchezoHauhitajiHasiraPasco nakubaliana na wewe
Katiba bora bila rasilimali watu, bila kupata mtu mwenye uthubutu wa kuisimamia hiyo katiba ni kazi bure.Yote hayo hayana maana yoyote bila katiba bora inayo akisi maoni ya Wananchi.
Mpaka mama lishe wanasema nchi haina mwelekeo.....vurugu,kutukanana,ulevi wa viongozi,uchumi mgumu,kutofata sheria,bunge laivu,kuingilia mahakama....Mkuu Pasco bandiko lako si rahisi mtu kulielewa ikiwa atakimbilia itikadi.Jana nilikuwa nimealikwa mahali,kikao kilikuwa na watu kama 50 hivi lakini nilishangaa kila mtu alikuwa akiijadili serekali ya Dr yaweza kutupeleka ambako ndiko siko kabisa.
Zipo dalili za wazi kabisa nchi inaenedeshwa pasipo kufuata sheria bali utashi wa mtu na hii si dalili nzuri hata kidogo.
Waangalie watu watatu hawa,Magufuli,Agrey Mwanri na Lyatonga mrema,compare and contrast,anything common amon them? Kuna jambo utagundua tu.Maelezo yako yote yamehitimishwa na paragraph ya tano.
Tanzania ilipofika na mazingira yaliyopo hatuwezi kufika huko unakodhani. Huu ni woga ambao ulitegemewa kwa sababu kinachofanywa na Rais kwa sasa kiko nje ya comfort zone za baadhi ya watu.
Ninafahamu ni wachache sana waliamini kama Rais Magufuli anaweza kumtumbua Kitwanga achilia mbali kumtumbua kwa aina kama ile huku Ikulu ikitoa Press Release yenye paragraph mbili ambazo ni fupi.
Hii imekuwa ni shock hasa ikichuliwa kuna wengine walisha bet na kusema watavua nguo au watatembea uchi kama Kitwanga atafukuzwa kazi.
Watu wanaomfahamu kwa karibu Rais Magufuli hawashangai kwa kile anachokifanya.
Ninakuhakikishia subiri mahakama ya mafisadi ianze utashangaa watakao kamatwa na kushitakiwa.
Hizi unazoziita character assassination itabidi wazizoee na njia ya kuepuka fanya kazi kama mkataba wako unavyotaka au achana na public sector na ingia kwenye private huku ukifuata sheria za nchi.
Kwa sasa kuna watu hali zao kifikra ni mbaya sana kwa sababu hawafahamu hatima yao kutokana na madhambi yao.
Rais Magufuli ni mtu anayechukia sana uonevu na uzembe lakini anaheshimu sana watenda mema kwa jamii hasa ya chini.
Kama kuna watu wanadhani wanaweza kupambana naye ili kumkwamisha ni bora wasahau hilo wazo kwa faida ya freedom zao.
mode of operation"modus oparandi"
Ya kawaidaa????Magufuli hana udikteta wowote. Hata mimi huwa natamani sana siku moja kuwa na dikteta lakini siyo kwa demokrasia hii. CCM bado ipo intact kwahiyo Magufuli ataendeleza sera za chama na si vinginevyo. Hizi ngonjera za kufukuza mawaziri ndiyo mnaziita udikteta? Hivi mbona vitu vya kawaida tu.
Huyo kwe picha ndo nani mkuu??View attachment 350124
Kwa wenye uwezo wa kusoma sura za watu. Sisi tuna bahati sana maana inaonyesha kwa sura hii kijana huyu alikuwa na maisha ya "furaha" sana enzi hizo.
Au mie sijui kusoma sura?
Huyo kwe picha ndo nani mkuu??