Chanzo halisi cha mbwa (Origin of dogs)

Afrocentric view

JF-Expert Member
Jun 19, 2022
1,373
2,267
Bonobo!

Canis Lupus Familiaris ndiyo jina la hii specie tunayoijua na kuipenda..Almaaruf kama Mbwa!!

Wengi mkiulizwa mbwa wametokea wapi kwa haraka haraka mtasema waliumbwa na Mungu.

Lakini kama maswali mengi kwenye hii dunia, majibu yake huwa sio rahisi kihivyo. Leo tuingie deep zaidi ya hapo tujue hawa mbwa wametokea wapi hasa. Chukua popcorn kabisa, it's history time.

Miaka laki 2 iliyopita, binadamu (Homo sapiens) alianza kuwepo huko Africa,(unaweza kufuatilia pia Chanzo halisi cha binadamu (Origins of mankind))

Miaka laki 1 mpaka 50,000 iliyopita hawa binadamu wa kale wakaamua kuondoka Africa na kwenda Ulaya na Asia kutafuta maisha bora.

Kwakuwa kipindi hiko binadamu kazi kuu waliyokuwa wanaifanya ilikuwa kuwinda na kukusanya matunda (Hawakuwa na kazi kama madaktari, Mainjinia, Wanamziki na maslay queens)

Walipofika Asia (hasahasa Siberia) walikutana na adui mkubwa sana ambaye aliwakwamisha katika kazi yao kuu ya uwindaji..Naye si mwingine bali ni..........(drumroll please🥁).........Canis Lupus (Grey wolf) kwa kizaramo anaitwa Mbwa mwitu

Screenshot_20230104_185305.jpg


Hawa wanyama waliwasumbua sana watu. na pia, watu waliwasumbua sana hawa mbwa mwitu..Tuwaite Wolves.

Hawa wolves waliwachukia sana binadamu maana walileta competition kwenye kutafuta chakula. Wolves waliona Hawa viumbe wapya waliokuja huku Siberia walikuwa wanauwezo mkubwa sana wa kuwinda kwa kuweka mitego na kushirikiana kwa hali ya juu kuliko wao mbwa mwitu(Wolves).

Kwa msiojua, mbwa mwitu pia huwa wanawinda kwa kushirikiana na kutengeneza plan za kumshambulia/kumvizia au kumkibiza adui mpaka achoke. ni ngumu sana kwa Mbwa mwitu kuwinda peke yake.

Wale mbwa mwitu waliofukuzwa kwenye ukoo (Packs) kutokan na tabia zao mbovu walikuwa wanaishi kwa kuwinda vimnyama vidogovidogo. Lakini kutokana na ujio wa huyu kiumbe mpya (binadamu), competition ya chakula ikawa kubwa, hata hawa wanyama wadogo wadogo ikawa ngumu kupatikana tena.

Wale mbwa mwitu waliofukuzwa na ukoo wakawa wanapata tabu kupata chakula, wakawa wanaishi kwa kutafuta makombo. Kwakuwa Binadamu walikuwa wanaishi kwenye makambi na wanakula nyama na kutupa mifupa (since hawana meno makali ya kutafuna mifupa.)

Hawa mbwa mwitu wasio na packs wakawa wanawavizia binadamu wakitupa makombo wao wanakula. Na hapo ndo ikawa mwanzo wa interaction kati ya binadamu na wolves.

katika wale wolves waliokuwa wanakuja kutafuta makombo, Binadamu wakawa wanachagua wale wasio tishio kwao (wapole, wenye miili midogo, watiifu) na wakagundua kuwa wanaweza kuwatumia kwa faida yao.

Wakaanza kugundua kuwa hawa wolves wanaweza kutumiwa kama walinzi akija Adui wanawahi kumsikia, kwahyo binadamu akaamua kuwa anakaa na hawa wolves ili apate kuzitumia faida zake, with time wakaanza kugundua faida nyingi za hawa wolves ikiwemo kunusa mbali na hata kujua wapi kuna wanyama wa kuwinda, Kupambana na dubu na wanyama wengine wakali, kuchunga mifugo nk.

Watu wakaanza kuwa wanachukua wale wolves wenye tabia na sifa wanazotaka na kuanza kuwabreed wao kwa wao. Hiki kitendo cha kuchagua mbegu za kufuga/kulima zenye sifa unazotaka na kuzitenga ili kupata matokeo unayotaka inaitwa Artificial selection.

Kwa hiyo kati ya miaka 30,000-23,000 iliyopita.. watu walikuwa wanachukua wolves na kuchagua sifa wanazopenda.

Watoto wakizaliwa na hizo sifa zinazotafutwa (Za kimbwa) ndiyo wanafugwa na kuwa bred tena na tena... Hivyo wolves wakawa wanabadilika, na wakibadilika wanachukuliwa tena wale wenye sifa zinazotafutwa mpaka tukafikia kupata mnyama anayeitwa leo Mbwa.

Lakini hizi breed tofauti tofauti za mbwa tunazojua leo zimetengenezwa less than miaka 400 iliyopita.
Hiyo hiyo formula ya artificial selection watu waliitumia (Na bado wanaendelea kuitumia) kutengeneza breed tofuti za mbwa wenye sifa tofauti wanazozitaka.

Unataka mbwa mwenye mbio? Chukua wale wenye miguu mirefu uwabreed wao kwa wao na watoto watakaozaliwa unawachagua wale wenye mbio tu na kuwafuga.
Screenshot_20230104_194030.jpg

Unataka mbwa mwenye nguvu?? Tafuta wenye sifa hizo na kuwabreed pamoja na watoto wasio na nguvu unawatupa pembeni. Unaendelea na wale wenye nguvu
Screenshot_20230104_194243.jpg

Je, untaka mbwa wa kukaa naye na kumchezea?
Screenshot_20230104_194418.jpg

Ukitaka mbwa mwenye sifa mbili labda Awe na nguvu na Manyoya mengi, Unachukua mbwa wawili wenye sifa Hizo na kuwabreed pamoja huku ukichukua wale watoto wenye sifa unazotaka na kuwabreed hao tu.
Screenshot_20230104_194712.jpg

Mpaka leo mbwa na Wolves wanaweza kuzaa pamoja lakini yule mtoto hawezi kuzaa.
Ule mstari unaowaunganisha kama specie moja umeshakatika.

Ipo siku mstari unaowaunganisha German shepherd na Bulldog unaweza kukatika vikaonekana kama viumbe viwili tofauti..

Hii artificial selection haijatuletea Mbwa tu, imetuletea pia Ndizi, Matikiti, Maparachichi, Kuku wa kisasa, Ng'ombe wa kisasa Nk. Nk.
 
Sawa. Nani aliumba wolves sasa
Ni nje kidogo ya mada, maana hapa tunaongelea mbwa., nilitaka tujikite kwenye mbwa.

*ila kwa kifupi wolves walitokana na miacids,(from Miacidae family)... hawa miacids na wao walitokana na insectivores wadogo kutoka kipindi cha cretaceous era.(enzi za Dinasours hizo, around 60 million years ago)

Hawa Miacids wameshapotea kwenye uso wa dunia, lakini walikuwa na maumbo tofauti tofauti makubwa kwa madogo, walievolve kutoka kuwa insectivores(wala wadudu) na kudevelop traits zilizowafanya kuwa carnivores(wala nyama) kama Makucha, meno nk.
wajukuu zao ni wengi kama canids (Wolves,dogs, Foxes, Vivverids, Genets (wa Afrika),coyotes, Jackals etc.),
Screenshot_20230105_004411.jpg
Na pia felines kama Paka, Chui, simba pia walitokana na miacis(Genus ndani ya family ya miacidae)
Screenshot_20230105_004431.jpg
...Hawa miacids ndio babu wa carnivores wote wa ardhini.
Screenshot_20230105_002807.jpg
 
Usafiri gani walitumia kutoka Africa kwenda ulaya na kwa muda gani?
 
Mkuu kwa hyo mchanganyiko wetu na wazungu tukiendelea kuzaana kuna siku uzi wa kua Jamii moja utakatika? Nmependa hii elimu
Yes indeed, uko sawa.Tungeendelea kutengana vile bila kuchangamana uzi ungekatika.

Kilichotusaidia sisi(na kinachoendelea kutusaidia) ni akili yetu na teknolojia zetu zilizoturahisishia kusafiri na kukutana jamii mbalimbali na kumix.

Kusafiri kwa Mitumbwi, ngamia, Farasi, Meli, Magari, na sasa ndege.

Hivi vinafanya jamii zetu mbalimbali zichangamane.

Ndege na magari vingengundulika zamani kabla hatujaanza kutofautiana sana huenda hata hizi race zisingekuwepo.

Na hivi tunavyoendelea kuchangamana na kukutana kwa utandawazi huenda hizi races nyingi zikapotea..
Huenda ukifa ukafufuka Baada ya miaka 30, 000 ukakuta duniani kuna race chache zaidi.... tena ambazo sasaivi hazipo (Za kichotara)

Kwa wanyama uzi zilikatika sana kwakuwa wakiachana kidogo tu inakuwa ngumu kukutana tena.

Hata ukiangalia tu hapa Bongo makabila mengi yanakufa saivi, Watu wanachangamana wanasahau hata kilugha chao...Sasaivi vijana wengi hawajui lugha wala mila zao, So inawezekana hata vizazi 6 vijavyo tukawa na makabila machache sana bongo tena yale makubwa makubwa tu. Madogo yote yakawa yamekufa.
 
Auroch walishakufa wote, wa mwisho aliuliwa miaka ya 1600s.

Nini kilisababisha hadi kufa wote, na huyo wa mwisho aliuliwa kimakosa au makusudi kwa lengo fulani?
 
Bonobo!

Canis Lupus Familiaris ndiyo jina la hii specie tunayoijua na kuipenda..Almaaruf kama Mbwa!!

Wengi mkiulizwa mbwa wametokea wapi kwa haraka haraka mtasema waliumbwa na Mungu.

Lakini kama maswali mengi kwenye hii dunia, majibu yake huwa sio rahisi kihivyo. Leo tuingie deep zaidi ya hapo tujue hawa mbwa wametokea wapi hasa. Chukua popcorn kabisa, it's history time.

Miaka laki 2 iliyopita, binadamu (Homo sapiens) alianza kuwepo huko Africa,(unaweza kufuatilia pia Chanzo halisi cha binadamu (Origins of mankind))

Miaka laki 1 mpaka 50,000 iliyopita hawa binadamu wa kale wakaamua kuondoka Africa na kwenda Ulaya na Asia kutafuta maisha bora.

Kwakuwa kipindi hiko binadamu kazi kuu waliyokuwa wanaifanya ilikuwa kuwinda na kukusanya matunda (Hawakuwa na kazi kama madaktari, Mainjinia, Wanamziki na maslay queens)

Walipofika Asia (hasahasa Siberia) walikutana na adui mkubwa sana ambaye aliwakwamisha katika kazi yao kuu ya uwindaji..Naye si mwingine bali ni..........(drumroll please🥁).........Canis Lupus (Grey wolf) kwa kizaramo anaitwa Mbwa mwitu

View attachment 2469009

Hawa wanyama waliwasumbua sana watu. na pia, watu waliwasumbua sana hawa mbwa mwitu..Tuwaite Wolves.

Hawa wolves waliwachukia sana binadamu maana walileta competition kwenye kutafuta chakula. Wolves waliona Hawa viumbe wapya waliokuja huku Siberia walikuwa wanauwezo mkubwa sana wa kuwinda kwa kuweka mitego na kushirikiana kwa hali ya juu kuliko wao mbwa mwitu(Wolves).

Kwa msiojua, mbwa mwitu pia huwa wanawinda kwa kushirikiana na kutengeneza plan za kumshambulia/kumvizia au kumkibiza adui mpaka achoke. ni ngumu sana kwa Mbwa mwitu kuwinda peke yake.

Wale mbwa mwitu waliofukuzwa kwenye ukoo (Packs) kutokan na tabia zao mbovu walikuwa wanaishi kwa kuwinda vimnyama vidogovidogo. Lakini kutokana na ujio wa huyu kiumbe mpya (binadamu), competition ya chakula ikawa kubwa, hata hawa wanyama wadogo wadogo ikawa ngumu kupatikana tena.

Wale mbwa mwitu waliofukuzwa na ukoo wakawa wanapata tabu kupata chakula, wakawa wanaishi kwa kutafuta makombo. Kwakuwa Binadamu walikuwa wanaishi kwenye makambi na wanakula nyama na kutupa mifupa (since hawana meno makali ya kutafuna mifupa.)

Hawa mbwa mwitu wasio na packs wakawa wanawavizia binadamu wakitupa makombo wao wanakula. Na hapo ndo ikawa mwanzo wa interaction kati ya binadamu na wolves.

katika wale wolves waliokuwa wanakuja kutafuta makombo, Binadamu wakawa wanachagua wale wasio tishio kwao (wapole, wenye miili midogo, watiifu) na wakagundua kuwa wanaweza kuwatumia kwa faida yao.

Wakaanza kugundua kuwa hawa wolves wanaweza kutumiwa kama walinzi akija Adui wanawahi kumsikia, kwahyo binadamu akaamua kuwa anakaa na hawa wolves ili apate kuzitumia faida zake, with time wakaanza kugundua faida nyingi za hawa wolves ikiwemo kunusa mbali na hata kujua wapi kuna wanyama wa kuwinda, Kupambana na dubu na wanyama wengine wakali, kuchunga mifugo nk.

Watu wakaanza kuwa wanachukua wale wolves wenye tabia na sifa wanazotaka na kuanza kuwabreed wao kwa wao. Hiki kitendo cha kuchagua mbegu za kufuga/kulima zenye sifa unazotaka na kuzitenga ili kupata matokeo unayotaka inaitwa Artificial selection.

Kwa hiyo kati ya miaka 30,000-23,000 iliyopita.. watu walikuwa wanachukua wolves na kuchagua sifa wanazopenda.

Watoto wakizaliwa na hizo sifa zinazotafutwa (Za kimbwa) ndiyo wanafugwa na kuwa bred tena na tena... Hivyo wolves wakawa wanabadilika, na wakibadilika wanachukuliwa tena wale wenye sifa zinazotafutwa mpaka tukafikia kupata mnyama anayeitwa leo Mbwa.

Lakini hizi breed tofauti tofauti za mbwa tunazojua leo zimetengenezwa less than miaka 400 iliyopita.
Hiyo hiyo formula ya artificial selection watu waliitumia (Na bado wanaendelea kuitumia) kutengeneza breed tofuti za mbwa wenye sifa tofauti wanazozitaka.

Unataka mbwa mwenye mbio? Chukua wale wenye miguu mirefu uwabreed wao kwa wao na watoto watakaozaliwa unawachagua wale wenye mbio tu na kuwafuga.View attachment 2469039
Unataka mbwa mwenye nguvu?? Tafuta wenye sifa hizo na kuwabreed pamoja na watoto wasio na nguvu unawatupa pembeni. Unaendelea na wale wenye nguvuView attachment 2469040
Je, untaka mbwa wa kukaa naye na kumchezea?View attachment 2469041
Ukitaka mbwa mwenye sifa mbili labda Awe na nguvu na Manyoya mengi, Unachukua mbwa wawili wenye sifa Hizo na kuwabreed pamoja huku ukichukua wale watoto wenye sifa unazotaka na kuwabreed hao tu.View attachment 2469044
Mpaka leo mbwa na Wolves wanaweza kuzaa pamoja lakini yule mtoto hawezi kuzaa.
Ule mstari unaowaunganisha kama specie moja umeshakatika.

Ipo siku mstari unaowaunganisha German shepherd na Bulldog unaweza kukatika vikaonekana kama viumbe viwili tofauti..

Hii artificial selection haijatuletea Mbwa tu, imetuletea pia Ndizi, Matikiti, Maparachichi, Kuku wa kisasa, Ng'ombe wa kisasa Nk. Nk.
Sasa hawa mbwa aina ya Basenji walitokea wapi? Maana kwenye michoro ya Irangi Kondoa wapo
 
Auroch walishakufa wote, wa mwisho aliuliwa miaka ya 1600s.

Nini kilisababisha hadi kufa wote, na huyo wa mwisho aliuliwa kimakosa au makusudi kwa lengo fulani?
Its intresting, Hawa Aurochs ndio kiumbe wa kwanza tuliyempoteza na kurekodi.(Tushapoteza wengi nyuma bila kurekodi)

Julius ceasar 53BC aliandika kuwa hawa Aurochs wapo ujerumani huko na wajerumani walikuwa wanawakamata kwenye mashimo na kutumia mapembe yao kama vikombe vya kunywea.

Binadamu ndio waliopelekea hawa Aurochs kupotea kwenye uso wa dunia kupitia shughuli kama ufugaji, kuna report moja ya 1564 inasema kuwa hawa Auroch hawazaliani vizuri kwakuwa binadamu walipokuwa wanapeleka ng'ombe zao malishoni walipunguza maeneo ya hawa Aurochs kuwa wanaishi na kula, Aurochs wakawa wanakosa mahala pa kukaa na pia wakawa wanawindwa sana.
Kuna Document ilionesha kuwa by 1599 kulikuwa na Auroch 24 tu waliobaki duniani, na majangili wakawa wanaona ukiwa na Pembe lake ni dili kubwa (Kama ilivyo sasa kwa Vifaru).
By 1620 Dume la mwisho likafa...Na lile jike lililobaki la mwisho liliwindwa na kuuliwa 1627.

It is sad, lakini Binadamu tumechangia na tunaendelea kuchangia kupoteza viumbe wengi hapa dunianj kupitia shughuli zetu kama deforestation, pollution nk.

All in all wanyama waliowahi kuishi duniani wakafa na kupotea ni wengi mara 99 kuliko wanyama tuliopo sasaivi.
Yani asilimia 99% ya wanyama wote waliowahi kuwepo duniani wameshapotea.
 
Back
Top Bottom