Black listed
Senior Member
- Apr 6, 2023
- 182
- 252
Juzi nimesafiri kutoka mkoa wa Dar es Salaam kwenda mkoa wa Shinyanga. Kijiografia, ni umbali mrefu, ambapo magari ya abiria hutumia si chini ya masaa 16 kufika mwisho wa safari.
Sasa kuna jambo moja nimeliona katika safari hii ndilo nataka wajuvi wa mambo ya wanyama watueleze, kwani ni jambo la kufikirisha kidogo!
Mnyama mbwa, ni miongoni mwa wanyama wanaotumiwa na binadamu katika shughuli mbalimbali za kijamii, kama ulinzi, kunusa, nk. Lakini pia, mnyama huyu anaweza kufundishwa michezo mbalimbali na akamudu kuicheza sawia.
Kwa muktadha huo, inaonyesha kuwa, mbwa ana akili pengine kuliko wanyama wengine, na ndiyo maana ni rahisi kwake kufundishika, tofauti na wanyama wengineo (most).
Sasa juzi katika safari yangu hiyo, nimeshuhudia si chini ya mbwa 6, mahala tofauti tofauti, wamegongwa na magari. Hapo ndio najiuliza, inakuwaje mnyama mwenye akili kuliko wengine; kama mbuzi, punda, paka, kuku, nguruwe, kondoo, ng'ombe, nk, anagongwa na magari wakati hawa wenye akili kidogo hawagongwi?!
Wakati tunajibu swali hili, majibu yetu tuhusianishe na ubongo wa mbwa, na sio factor nyingine kama uwingi wao, kukosa matunzo, kichaa cha mbwa, nk; kwani hizi ni hoja nyepesi. Mbwa wanaoongelewa hapa ni wakamilifu kwa mitazamo yote.
Mtu anaweza kuona nimeuliza jambo la kijinga, lakini wataalamu wa wanyama najuwa watakuja na sababu za msingi kuhusiana na jambo hili! Au wenzangu hamjawahi kijiuliza kwanini mbwa anagongwa kirahisi sana na magari kuliko wanyama wengine?
Sasa kuna jambo moja nimeliona katika safari hii ndilo nataka wajuvi wa mambo ya wanyama watueleze, kwani ni jambo la kufikirisha kidogo!
Mnyama mbwa, ni miongoni mwa wanyama wanaotumiwa na binadamu katika shughuli mbalimbali za kijamii, kama ulinzi, kunusa, nk. Lakini pia, mnyama huyu anaweza kufundishwa michezo mbalimbali na akamudu kuicheza sawia.
Kwa muktadha huo, inaonyesha kuwa, mbwa ana akili pengine kuliko wanyama wengine, na ndiyo maana ni rahisi kwake kufundishika, tofauti na wanyama wengineo (most).
Sasa juzi katika safari yangu hiyo, nimeshuhudia si chini ya mbwa 6, mahala tofauti tofauti, wamegongwa na magari. Hapo ndio najiuliza, inakuwaje mnyama mwenye akili kuliko wengine; kama mbuzi, punda, paka, kuku, nguruwe, kondoo, ng'ombe, nk, anagongwa na magari wakati hawa wenye akili kidogo hawagongwi?!
Wakati tunajibu swali hili, majibu yetu tuhusianishe na ubongo wa mbwa, na sio factor nyingine kama uwingi wao, kukosa matunzo, kichaa cha mbwa, nk; kwani hizi ni hoja nyepesi. Mbwa wanaoongelewa hapa ni wakamilifu kwa mitazamo yote.
Mtu anaweza kuona nimeuliza jambo la kijinga, lakini wataalamu wa wanyama najuwa watakuja na sababu za msingi kuhusiana na jambo hili! Au wenzangu hamjawahi kijiuliza kwanini mbwa anagongwa kirahisi sana na magari kuliko wanyama wengine?