Channel 10 Live: Jenerali on Monday

Channel 10 Live: Jenerali on Monday

tangu lini mwigizaji akaitwa mwandishi wa habari?
 
Only in Tanzania.... waandishi wa habari makanjanja!!!
 
Baada ya kuendelea kusikiliza kipindi hili cha leo trh 27/01/2014.
Kuna mtu anaitwa simalenga ametambulishwa kama mwandishi wa habari.
Mwana habari huyu anasema tume imelazimisha serikali 3 na si mawazo ya watz,
Anasema watu laki tatu hawakustahili kuamua juu ya katiba,
Anadai baadhi wajumbe wa tume ya katiba walikuwa wana G55 ameambiwa awataje ameshindwa

Mtazamo wangu, UAMDISHI WA HABARI INATAKIWA KUWA NA WATU WENYE DIVERSITY OF PROFESSION, nafikiri hoja ya kipindi ingepata mwandishi wa habari ambaye ana taaluma ya sheria/historia/au hata uchumi ua hata fani nyingine angeweza kuleta changamoto za maana.

NI VYEMA PIA WAANDAAJI WA VIPINDI KUALIKA WATU WENYE UJASIRI BILA KUONGEA KWA HOFU NA HISIA TU.

NAWAKILISHA KIZALENDO
Simalenga mwandishi wa habari? mmh
 
jamaa kapwaya vibaya mimi nilidhani labda mimi ndio mwenye matatizo ya kumuelewa huyo jamaa.

kumbe yeye ndio haeleweki?

Jeneral katuletea mtu asie jiweza kabisa
 
Pasco is the other one! Teh teh
Mkuu Punjabi, pole sana!. Politics is my area of specialization, hivyo endelea kujifariji!.

Najua hizi ni hasira za jinsi nilivyotoa siri za amasikini uliotopea wa mababu zenu, na jinsi baba zenu wa wa lowest caste kule kwenu, walivyoponea kwa kuletwa nchini kama makuli wa kujenga reli, ndipo mkatoka na nyinyi kuzaliwa huku mkujidai huku tuu, lakini ndani ya miyo yenu ni wabaguzi wakuu!.

Usiendelee kukakisirika, pia si niliwasifu mna bidii sana, na ni waaminifu?!, Sasa hasira za nini kunilinganisha na watoto wa juzi?.

Please be fair to me!.

Pasco
 
Sidhani Kama ni Kweli ila Nionavyo tu ni Kwamba hatuna Competent Journalists Japo Kielimu Wanaweza Wakawa Wana Elimu Kubwa tu tena hata Kushinda Ya Kwako. Kwa Mfano huyo Dotto Bulendu alikuwa Mbele Yangu Chuo Kikuu chetu Kile cha Papa Francis Kanda Ya Ziwa na Sasa ana Masters Yake na Kama Sijakosea Simalenga Alimaliza Diploma Yake Ya Habari DSJ ambapo hata Mke Wake alikuwa ni Mwanafunzi Mwenzake hapo hapo DSJ Chuoni na Sasa Anasoma Shahada Yake Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere. Elimu Wanazo tena Nzuri tu ILA TATIZO KUBWA LA WAANDISHI WETU WENGI WA HABARI TANZANIA HAWASOMI ISSUES MBALIMBALI, HAWAWEZI KUCHAMBUA MADA na WALICHOKALIA NI UMBEA na UZUSHI NA WANADHANI KUWA NA VYETI PEKEE NDIYO UANDISHI WA HABARI. Specialisation inatakiwa sana Kwa Waandishi Wetu Lakini pia Kuna Matatizo Makubwa Sana ktk Vyuo Vyao Kuanzia Wakufunzi Wao, Vitendea Kazi na Haswa Mazingira Ya Kusoma na Pia Ipo Haja Journalism Nayo iwe na Chombo Maalum cha Ku Screen Waandishi Kama ilivyo Kwa Fani za Sheria, Uhasibu na Madaktari ili Kabla Hawajaanza Kazi basi Wawe Wameshachujwa Vya Kutosha. Mwisho hata Huku Kuajiriwa Kwa Kujuana au Kwa Rushwa Ya Ngono Napo Kunaiponza Fani hiyo! Chuoni Mwanafunzi Anahonga Penzi Kwa Mwalimu au Anatoa Pesa Ananunua Paper au Cheti na Hapo Hapo tena Akitafuta Kazi napo Mziki ni huo huo wa Kuhonga Kwa Pesa au Ngono Je Mnategemea Nini hapo? Bado Safari ni Ndefu Sana na Inasikitisha!!!!!!!

Well said mkuu,sio kila mwenye shahada ni mahiri kwenye fani yake wengine wamehonga kuwa nayo.Hiko chuo DSJ kiko wapi maana kuna watu wengi wamepita hapo tena hawapo vizuri.
 
jamaa kapwaya vibaya mimi nilidhani labda mimi ndio mwenye matatizo ya kumuelewa huyo jamaa.

kumbe yeye ndio haeleweki?

Jeneral katuletea mtu asie jiweza kabisa

Waliomwalika ndiyo wenye makosa
 
Niliamua kubadilisha channel. Hana ufahamu wa kutosha kuhusu masuala mapana ya kile anachokizungumzia. Ila ninachokumbuka kuhusu yeye ni kwamba alikuwa Msanii wa kundi la KAOLE.
 
Naangalia kipindi cha Jenerali Ulimwengu sasa hivi na mgeni leo ni Simon Simalenga ambaye ni mwanahabari (Producer wa kipindi cha Jahazi cha Clouds FM).

Kipindi cha leo kinahusu rasimu ya pili ya katiba. Simalenga nashangaa kwanini alienda kwenye kipindi wakati anapwaya sana kwenye suala hili la katiba.

Jamaa kila swali analoulizwa anaweweseka kujibu kiasi ambacho mzee Jenerali inabidi aanze kumuelimisha.

Huyu jamaa amezoea kule clouds fm utani mwingi akajua ataweza kuchambua masuala ya katiba.

Leo mzee Ulimwengu umetuletea boya katika kipindi chako.

We acha tu mimi jana nimecheka mpaka mbavu zikauma, jamaa hadi akawa anatunga maswali ambayo Jenerali hajamuuliza halafu anaanza kuyajibu mwenyewe. Baada ya Jenerali kuona kuwa jamaa anapwaya sana, Jeneali hadi ilibidi yeye aone aibu ila hakupenda kumuumbua. Angekuwa mhojiwa ni mwanasiasa halafu ayumbe hivyo, Jenerali asingefanya makosa ya kumlea! Nilimuona pia kwenye Malumbano ya Hoja, point of departure aliyoitoa jana ndiyo ile ile aliyoitumia kwenye Malumbano ya Hoja. Yaani nilicheka hakuna mfano. Lakini mimi wito wangu watu naomba sana waziheshimu media ukionekana kwenye media hakikisha una point zenye mashiko!
 
Wakuu.

Mengi yamesemwa kumhusu huyo anayeitwa "mwandishi" wa habari. pengine mimi nijielekeze katika upande wa pili wa mwandaaji wa kipindi hicho cha "Jenerali on Monday". Nafikiri ilikuwa bora kwake kumwalika Nape Mnauye au Peter Kisumo kutoa maelezo juu ya Muundo wa serikali tatu kwa muktadha wa CCM

Nasema Nape na Kisumo kwa sababu wao ndio walio/ wanaoendesha propraganda dhjidi ya serikali tatu kama ilivyopendekezwa na tume ya Warioba. Simalenga amedhihirisha kuwa "Mwepesi" katika uelewa wake wa mambo mbali ingawa waliobahatika kupiga simu wengi wao walionekana kumwunga mkono kwa hoja dhaifu za kupinga serikali tatu.

Lakini pia, imezoeleka ( lakini sio sheria) kuwa mwandaaji na mgeni wa kipindi hukubaliana juu ya mada itakayojadiliwa na hivyo hutoa fursa ya kuelewa uwezo wa mgeni husika na kuangalia uwezekano wa kumwongoza vizuri katika mada husika. Lau kama hilo lilishindikana sitaki kuamini kuwa Ulimwengu alilenga kumuumbua kada huyo wa CCM kwa namna aliyofanya. Ndio maana nasema katika mada kama iliyojadiliwa jana ilikuwa vyema kabisa kuwatafuta Nape na Kisumo na kuwahoji maswali hayo, sio huyo ambaye alishindwa kuunganisha Mantiki juu uhalali wa wanaounga mkono na wanaopinga.

Vinginevyo imetusaidia wengine kuwafahamu "waandishi" lakini uzuri mwingine wa taasisi anayotoka kama inaweza kuwa na mwandaaji wa vipindi wa kiwango hiki sipati picha ya anaowaongoza wako katika kiwango gani cha uelewa. Hongera Ulimwenfu kwa kumfunua, itamsaidia ( kama ana akili) kujifunza zaidi ( sio lazima kukaa darasani) lakini pia kujipima mwenyewe kama kweli anao uwezo wa kuwa mwakilishi wa wananchi wa jimbo.
 
Jamaa kachemka mbaya hadi nikamuonea huruma....Huenda huyu ni kielelezo cha wanahabari waliojaa nchini!

Kuwe na bodi ya kusajili waandishi wa habari, "Journalists Registration Board" kama kulivyo na bodi ya wahandisi au wahasibu nk. Siku hizi hata DJ anajiita muandishi wa habari.

Jenerali naye naona aliamua tu kumuumbua maana ukitaka umhoji mtu live inabidi ujue na akili yake ikoje.
 
Mkuu Punjabi, pole sana!. Politics is my area of specialization, hivyo endelea kujifariji!.

Najua hizi ni hasira za jinsi nilivyotoa siri za amasikini uliotopea wa mababu zenu, na jinsi baba zenu wa wa lowest caste kule kwenu, walivyoponea kwa kuletwa nchini kama makuli wa kujenga reli, ndipo mkatoka na nyinyi kuzaliwa huku mkujidai huku tuu, lakini ndani ya miyo yenu ni wabaguzi wakuu!.

Usiendelee kukakisirika, pia si niliwasifu mna bidii sana, na ni waaminifu?!, Sasa hasira za nini kunilinganisha na watoto wa juzi?.

Please be fair to me!.

Pasco
Pasco unaamanisha huyu kilaza simalenga ni mtoto kiumli au mtoto kwenye tasnia nzima ya habari? nimecheke sana mnavyoanza kukimbiana
 
Last edited by a moderator:
mh, nilimsikiliza na kumshangaa kukubali kuongelea kitu ambacho hawezi kujenga hoja wala kuwa na mtiririko wa kueleweka. NI KAMA ALIENDA KUUMBUKA PALE. asifanye mchezo kama huo siku nyingine
 
Naangalia kipindi cha Jenerali Ulimwengu sasa hivi na mgeni leo ni Simon Simalenga ambaye ni mwanahabari (Producer wa kipindi cha Jahazi cha Clouds FM).

Kipindi cha leo kinahusu rasimu ya pili ya katiba. Simalenga nashangaa kwanini alienda kwenye kipindi wakati anapwaya sana kwenye suala hili la katiba.

Jamaa kila swali analoulizwa anaweweseka kujibu kiasi ambacho mzee Jenerali inabidi aanze kumuelimisha.

Huyu jamaa amezoea kule clouds fm utani mwingi akajua ataweza kuchambua masuala ya katiba.

Leo mzee Ulimwengu umetuletea boya katika kipindi chako.
Huyo Simalenga nadhani hoja aliyokwenda kuijadili inampwaya sana. Maana kila alichokuwa anaongea kilikuwa ni cha kufikirika zaidi na sio uhalisia. Jana Jenerali ndio akawa mtoa mada jamaa akabaki na kuongea mambo kwa jumla jumla tu.
 
Pasco unaamanisha huyu kilaza simalenga ni mtoto kiumli au mtoto kwenye tasnia nzima ya habari? nimecheke sana mnavyoanza kukimbiana
Mkuu Mzee wa Rock, japo jina lako ni Mzee, ila na wewe pia utakuwa ni hawa hawa wa juzi, kwanza sio haki kumuita Simalenga ni kilaza, this is the brain behind the most popular radio series kwa sasa, Jahazi la Clouds .FM, namfahamu tang akiwa na kina Ray na Kanumba kwenye drama, hivyo kutobobea katika siasa sio kilaza.

Kwa wale wa zamani, ukikitaja kipindi cha Kitimoto, wanalielewa jina la Pasco, ulizia ni kipindi gani kilichopo sasa chenye level ile. Nimesema asinilinganishe mimi na vijana wa Leo kwa jinsi ile huwezi kuilinga RTD na Clouds FM au TBC na TV, that was then, tulikuwa wazuri kwa wakati wetu, sasa hawa vijana wa Leo ni wazuri kwa wakati wao. Ni sawa kumlinganisha Zahir Zorro na Banana Zorro, enzi za Zahir , alikuwa Zahir sasa hizi ni enzi za Banana!. Enzi za RTD zimepita sasa hizi ni enzi za Clouds FM!.
Usilinganishe !.
Pasco
 
Mkuu Mzee wa Rock, japo jina lako ni Mzee, ila na wewe pia utakuwa ni hawa hawa wa juzi, kwanza sio haki kumuita Simalenga ni kilaza, this is the brain behind the most popular radio series kwa sasa, Jahazi la Clouds .FM, namfahamu tang akiwa na kina Ray na Kanumba kwenye drama, hivyo kutobobea katika siasa sio kilaza.

Kwa wale wa zamani, ukikitaja kipindi cha Kitimoto, wanalielewa jina la Pasco, ulizia ni kipindi gani kilichopo sasa chenye level ile. Nimesema asinilinganishe mimi na vijana wa Leo kwa jinsi ile huwezi kuilinga RTD na Clouds FM au TBC na TV, that was then, tulikuwa wazuri kwa wakati wetu, sasa hawa vijana wa Leo ni wazuri kwa wakati wao. Ni sawa kumlinganisha Zahir Zorro na Banana Zorro, enzi za Zahir , alikuwa Zahir sasa hizi ni enzi za Banana!. Enzi za RTD zimepita sasa hizi ni enzi za Clouds FM!.
Usilinganishe !.
Pasco

Upofu upo katika sura na maumbo tofauti.

KAMA NI MIND BEHIND JAHAZI SASA NIMEELEWA KWANINI KIBONDE ANAENDELEA KUPOTOSHA UMMA NA BADO ANACHEKEWA

NAWAKILISHA KIZALENDO
 
Kitu cha kujadiliana hapa ni kwamba akihitimisa alisema hivi kama wabunge wa bunge la katiba watalazimisha serikali tatu yeye atakuwa wa kwanza kuhamasisha vijana kuikataa na kubaki kwenye serikal mbili
Tayari na msimamo nisikai mbili
Anapotosha umma kwa mausudi anasema tume iliweka mawazo yake hakuna mtanzania aliulizwa kuhusu serikali tatu, hii spinning ni kwa manufaa ya nani

Anasema G55 ndio wajumbe wa tume
watanzana wenzangu hiz propaganda zimeanza ukweli tuwe naplan B maana hakuna katiba mpya kwa sasa tujiuize
Namna ya kuboresha na Lazima kuwa na tume huru ya uchaguzi
Namna ya kusjaili na kuwa na datary jipya a wapiga kura mane tulilonao limechakachuliwa mno
 
Kitu cha kujadiliana hapa ni kwamba akihitimisa alisema hivi kama wabunge wa bunge la katiba watalazimisha serikali tatu yeye atakuwa wa kwanza kuhamasisha vijana kuikataa na kubaki kwenye serikal mbili
Tayari na msimamo nisikai mbili
Anapotosha umma kwa mausudi anasema tume iliweka mawazo yake hakuna mtanzania aliulizwa kuhusu serikali tatu, hii spinning ni kwa manufaa ya nani

Anasema G55 ndio wajumbe wa tume
watanzana wenzangu hiz propaganda zimeanza ukweli tuwe naplan B maana hakuna katiba mpya kwa sasa tujiuize
Namna ya kuboresha na Lazima kuwa na tume huru ya uchaguzi
Namna ya kusjaili na kuwa na datary jipya a wapiga kura mane tulilonao limechakachuliwa mno

Hapo ndio nilimshangaa sana Simalenga, namnukuu "Bunge la katiba likipitisha serikali tatu sisi vijana tutaipinga hiyo rasimu na kurudi kwenye serikali mbili". Sehemu nyingine aliponishangaza ni aliposema "Mh. Rais alikosea sana kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya katiba, katiba iliyoko sasa haina kasoro zozote na ni bora tukaendelea kutumia katiba ya sasa" Kama huyu jamaa ndio think tank ya Clouds Media Group basi hii nchi inaelekea kuzimu.
 
Naangalia kipindi cha Jenerali Ulimwengu sasa hivi na mgeni leo ni Simon Simalenga ambaye ni mwanahabari (Producer wa kipindi cha Jahazi cha Clouds FM).

Kipindi cha leo kinahusu rasimu ya pili ya katiba. Simalenga nashangaa kwanini alienda kwenye kipindi wakati anapwaya sana kwenye suala hili la katiba.

Jamaa kila swali analoulizwa anaweweseka kujibu kiasi ambacho mzee Jenerali inabidi aanze kumuelimisha.

Huyu jamaa amezoea kule clouds fm utani mwingi akajua ataweza kuchambua masuala ya katiba.

Leo mzee Ulimwengu umetuletea boya katika kipindi chako.

Ulimwengu hata kama kaleta boya anamulika hawa makajanja wa mjini wanaojinadi kama waandishi wa habari.
 
Back
Top Bottom