Msolo
JF-Expert Member
- Oct 19, 2008
- 3,829
- 5,270
Natamamani kukiona hivi huwa wana-upload vipidi vyao ili tuone wengine tupo mbali na TVHv iki kipindi kina marudio siku za weekend,maana mmeponda mpaka nimecheka usiku huu .
Natamamani kukiona hivi huwa wana-upload vipidi vyao ili tuone wengine tupo mbali na TVHv iki kipindi kina marudio siku za weekend,maana mmeponda mpaka nimecheka usiku huu .
Pasco is the other one! Teh tehJamaa kachemka mbaya hadi nikamuonea huruma....Huenda huyu ni kielelezo cha wanahabari waliojaa nchini!
Watu kama hawa ni wengi sana nchi hii.Wanaongea bila hoja na wanatetea sana ujinga wao.Mtu anafikia kusema hata katiba mpya si ya lazima eti watanzania wanataka maisha mazuri!!ajabu hii!Haya maisha bora watayapataje bila katiba imara isiyotetea maisha yao?Katiba ambayo haiwawajibishi viongozi wababaishaji bado kuna watu wanaitetea?Hawa watanzania wa jinsi hii wasipoelimika nchi hii ni majanga sidhani tutafika tuendako!
Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
Uyu jamaa si alikuaga msanii wa Kaole au macho yangu?
Baada ya kuendelea kusikiliza kipindi hili cha leo trh 27/01/2014.
Kuna mtu anaitwa simalenga ametambulishwa kama mwandishi wa habari.
Mwana habari huyu anasema tume imelazimisha serikali 3 na si mawazo ya watz,
Anasema watu laki tatu hawakustahili kuamua juu ya katiba,
Anadai baadhi wajumbe wa tume ya katiba walikuwa wana G55 ameambiwa awataje ameshindwa
Mtazamo wangu, UAMDISHI WA HABARI INATAKIWA KUWA NA WATU WENYE DIVERSITY OF PROFESSION, nafikiri hoja ya kipindi ingepata mwandishi wa habari ambaye ana taaluma ya sheria/historia/au hata uchumi ua hata fani nyingine angeweza kuleta changamoto za maana.
NI VYEMA PIA WAANDAAJI WA VIPINDI KUALIKA WATU WENYE UJASIRI BILA KUONGEA KWA HOFU NA HISIA TU.
NAWAKILISHA KIZALENDO
Huyu jamaa alikuwa kwenye mchezo wa kuigiza wa kaole .jina lake la kisanii ni dumelo .ni mtoto sana kuhusu maswala haya .ni mtoto wa kupakatwa that's what I can say .nina maana ametumwa
Huyu jamaa alikuwa kwenye mchezo wa kuigiza wa kaole .jina lake la kisanii ni dumelo .ni mtoto sana kuhusu maswala haya .ni mtoto wa kupakatwa that's what I can say .nina maana ametumwa
Tunahitaji waendesha vipindi vya mahojiano kama Jenerali Ulimwengu. Akija mtu kama mtu aina ya Semalenga anapigwa maswali kama ya Ulimwengu ili ajiaibishe mwenyewe. Leo mimi nilikuwa naangalia kipindi kama hicho kuhusu muungano wenye muundo wa serikali 3 kwenye kipindi cha agenda 2015 startv ilikuwa vituko vitupu. Waendesha kipindi DOTO BULENDU kituko na mwenzake Mpangala kituko. Nimeamini Startv haina waandishi wenye maarifa kwa maana wenye uwezo mkubwa kielimu. Wageni wao walikuwa ndg Mkinga, mpayukaji na ndg Alikazi mwandishi wa habari radio moja huko shinyanga. Watu ni kama wanaandaliwa vipindi kuja kupotosha watanzania kwa sababu badala ya kujadili rasimu wanamjadili mzee Warioba. Watu wa aina hii ni hatari. Nawapongeza waandishi kama Ulimwengu na Dr. Ryoba. Tatizo la watangazaji aina ya DOTO wa startv ni kutojisomea mambo mbalimbali nje ya taaluma zao ili kujiongezea maarifa.
Huyo jamaa anadhalilisha hata taasisi ikiyomwajiri. Wote wanaonekana hamna kitu ni usanii tu.
Hilo ndio tatizo la kulishwa mawazo.
kwanza kawapotosha watanzania kuwa serikali tatu sio maoni ya watanzania bali ni kikundi cha watu wachache kilichoidhinisha serikali tatu,hapo hanma mwandishi wa habari,kwanza ameidhalilisha tasinia ya uandishi wa habari.
Dogo amebanwa mbavu macho yamemtoka. Nimemwonea huruma. Akome asirudie tena. Anadhani hapo ni kaole.
Tunahitaji waendesha vipindi vya mahojiano kama Jenerali Ulimwengu. Akija mtu kama mtu aina ya Semalenga anapigwa maswali kama ya Ulimwengu ili ajiaibishe mwenyewe. Leo mimi nilikuwa naangalia kipindi kama hicho kuhusu muungano wenye muundo wa serikali 3 kwenye kipindi cha agenda 2015 startv ilikuwa vituko vitupu. Waendesha kipindi DOTO BULENDU kituko na mwenzake Mpangala kituko. Nimeamini Startv haina waandishi wenye maarifa kwa maana wenye uwezo mkubwa kielimu. Wageni wao walikuwa ndg Mkinga, mpayukaji na ndg Alikazi mwandishi wa habari radio moja huko shinyanga. Watu ni kama wanaandaliwa vipindi kuja kupotosha watanzania kwa sababu badala ya kujadili rasimu wanamjadili mzee Warioba. Watu wa aina hii ni hatari. Nawapongeza waandishi kama Ulimwengu na Dr. Ryoba. Tatizo la watangazaji aina ya DOTO wa startv ni kutojisomea mambo mbalimbali nje ya taaluma zao ili kujiongezea maarifa.
Mkuu,picha zinajieleza,kama Juma Nkamia kashamuona mwenye mbwa anayefanya mbwa abwake bwake hovyo!! Clouds siku hizi imekuwa kama radio Uhuru,naanza kuamini kuwa wamesaini MoU na CCM kuelekea 2015 kwa kufanya indirect propaganda kwa kuwalenga Vijana!!!