Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Mwalimu Nyerere hakukianzisha Chama cha CCJ. Isipokuwa hawa watu walioanzisha CCJ wanamtaja Mwalimu katika Katiba yao,wanamweka Mwalimu katika Katiba yao,kama njia ya kupata baraka ya Watanzania.
Hawajajitokeza,kwa nini tusisubiri wajitokeze kabla ya kutoa maoni kuhusu CCJ. Tusibiri. Tunachoweza kusema tu sasa,hatuoni hitilafu yoyote katika jinsi hiki Chama kipya kinavyoanzishwa...

Na kama wana nia nzuri kwanini wasijitokeze?Hii sio operesheni ya kijasusi kumkamata Osama or something like that.

As to kuwasubiri,why should we?Tumesubiri ujio wa Maisha Bora kwa Kila Mtanzania,na sasa ni mwaka wa tano hatujayaona.Hayo yanatokea wakati baadhi ya Watanzania kama mie(Wakristo) tunasubiri ujio wa pili wa Yesu.I don't see the logic kusubiri kujitokeza kwa "vigogo" wa CCJ just like sioni mantiki ya wao kujificha muda huu
 
ogopa sana maishani kuishi kwa kudhania....kuamini au kutoamini ni juu yako heri kuwa katikati ya A na B kuliko kuwa mtu wa kudhani

Naogopa sana watu wanaoamini kila wanachoona na kusikia. Hawa ndio walioambiwa A mwaka 2005 na hawajaiona hadi leo,na waliahidiwa B na haijapatikana hadi kesho. Same people watasikia sio A na B pekee bali alphabets zote mpaka Z hapo Oktoba, na kwa wepesi wa kuamini kila wanachosikia na kuona, wataaminishwa.

Ukiwa mwanataaluma utaelewa umuhimu wa kudhania (ku-hypothesize).
 
As I said before, I might be wrong lakini....
YES, you are; I will be back and state why. Mkuu, kumradhi, I need a little time (and hopefully you understand this).

Lakini, good analysis, nimegonga "THANKS" kuonyesha kuwa nimeukubali mchango wako!
 
YES, you are; I will be back and state why. Mkuu, kumradhi, I need a little time (and hopefully you understand this).

Lakini, good analysis, nimegonga "THANKS" kuonyesha kuwa nimeukubali mchango wako!

Nakuaminia mkuu.Tuko pamoja
 
CCM ikigawanyika ni health for our democracy ..afadhali lipasuke pasuke safi sana..kwanza li-chama hilo limekuwa kubwa mno..hakuna fair competition

Unakumbuka hata NBC ilivunjwa kwa ajili ya kuruhusu fair banking competition the same line of thinking.
 
TUHUMA za kuwepo kwa wanasiasa waandamizi na wakongwe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaopanga kujitoa katika chama hicho tawala na kujiunga na chama kipya wanachodaiwa wamekiandaa kinachoitwa Chama Cha Jamii, zimeendelea kutoa sura tofauti miongozi mwa wanasiasa hao.

Wakati juzi Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Mtera, John Malecela alikanusha vikali kuhusika na uasisi wa chama hicho, jana Habari Leo liliwapata viongozi wengine waandamizi wanaotuhumiwa kuazisha chama hicho ambao hawakuthibitisha kuwa miongoni mwa waasisi wa chama hicho wala kukana tuhuma hizo.

Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba alizungumza na Habari Leo kuhusu tuhuma kwamba yeye ni mmoja wa mawaziri wakuu watatu wanaotuhumiwa kuunda CCJ, alisema hawezi kuzungumzia chochote kuhusiana na madai kuwa yeye ni miongoni mwa waasisi wa chama hicho.

“Siwezi kusema chochote kuhusiana na taarifa zinazosambazwa na mtu asiyejulikana,” alisema.

Aidha Waziri Mkuu huyo wa zamani alishauri mwandishi wa habari hizi kuwasiliana na uongozi wa CCJ kuhusiana na shauri hilo.

Habari Leo lilimpata mwanasiasa mwingine mkongwe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku na kumuuliza iwapo anahusika na uanzishwaji wa chama hicho, kama ilivyo katika waraka wenye tuhuma hizo na yeye alisema hajaona nyaraka zinazomuhusisha yeye na CCJ.

“Sijaona nyaraka hizo,” alisema Butiku na kukataa kuendelea na mahojiano na mwandishi wa habari hii hata baada ya kuhakikishiwa kuwa waraka huo upo.

Mwandishi wa habari alitaka kujua kama mwanasiasa huyo alikuwa ameona nyaraka za chama hicho na kama ana maoni yoyote kuhusiana na madai kwamba anahusika katika kuiasisi CCJ.

Kuomba usajili kwa chama hicho kipya cha siasa kumezua maswali mengi miongoni mwa watu kadhaa wakiwemo wanasiasa kutokana na madai kuwa viongozi wakubwa wa CCM wamekiandaa na wanapanga kujiunga nacho kwa nia ya kuiangusha CCM katika uchaguzi mkuu ujao.

Tayari Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba ametoa kauli kuwa CCJ hakiwatishi huku Katibu wa Uenezi wa Kamati Kuu ya CCM (NEC), John Chilighati akisema kuwa watakaotoka CCM, watakuwa wamejimaliza wenyewe.

Licha ya viongozi hao waliokwisha zungumzia CCJ, viongozi wengine wanaodaiwa kuhusika nacho ni pamoja na kundi la wabunge wanaojipambanua kuwa makamanda wanaopiga vita rushwa.

Kutokana na misimamo ya vigogo hao wanaotuhumiwa kutaka kujiunga na chama hicho, ilidaiwa pia kuwa vigogo hao wameandaa kongamano la kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere, litalaotumika kama uwanja wa kukitangaza chama hicho.

Kongamano hilo limedaiwa kuwa lingefanyika kwa mgongo wa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Aford ambayo haijapata usajili lakini lengo lake likiwa kutoa ishara za awali za chama hicho cha CCJ.

Habari Leo lilifanikiwa kumpata kiongozi wa taasisi hiyo ya Aford, Julius Miselya ambaye alianza kuvishutumu vyombo vya habari kwa kutumia vibaya jina la taasisi yake kuisakama serikali ya Rais Jakaya Kikwete.

“Ni nyie waandishi wa habari mnaosambaza taarifa hii inayotoka kwa mtu asiyejulikana na kuleta mtafaruku nchini,” alisema.

“Mimi sifungamani na chama chochote, nimewatambua watu wanaojihusisha na CCJ kwa kusoma magazeti asubuhi hii,” alisema Miselya.

Amesema kongamano hilo ambalo bado lipo katika maandalizi limeibuliwa kwa waandishi wa habari kwa lengo la kupotosha ukweli.

“Muulize Waziri Mkuu kama amethibitisha kushiriki, sitazungumzia kitu hicho,” alisema. Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ametajwa katika waraka huo kuwa ndiye atakayefungua kongamano hilo.

Alipohojiwa kama kongamano hilo litaendelea kama lilivyopangwa, alisema kwamba hatasema chochote kwa vyombo vya habari.

Baadhi ya viongozi wa CCM waliounganishwa na uanzaji wa chama kipya cha siasa nchini walipoulizwa walisema kwamba ndio kwanza wanajua kuwa kuna chama kipya.

Mwanasiasa mwingine aliyehusishwa na chama hicho kipya na kukanusha ni mbunge wa Maswa, Magale Shibuda.

Juhudi za gazeti hili kupata maoni ya wahusika wengine zilishindikana jana na bado zinaendelea.

Juzi Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, aliliambia Habari Leo kuwa chama hicho kipya kina safari ndefu kwa kuwa taratibu za kusajili chama huchukua muda.

Alisema licha ya chama hicho, tayari kuna vyama vingine vingi ambavyo vinasubiri kupewa usajili na kuongeza kuwa huenda CCJ kikapata usajili wa muda kabla ya Machi mwaka huu.

SOURCE: http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=5391
 
Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba alizungumza na Habari Leo kuhusu tuhuma kwamba yeye ni mmoja wa mawaziri wakuu watatu wanaotuhumiwa kuunda CCJ, alisema hawezi kuzungumzia chochote kuhusiana na madai kuwa yeye ni miongoni mwa waasisi wa chama hicho.
I would prefer it termed as madai, and not tuhuma!

Neno hili linanyonga dhana ya demokrasia, na kutisha, likipanda mawazo mgando kuwa mtu kuhamia chama kingine ni dalili ya uhaini...huh!
 
CCJ mbona kimeanzishwa kwa mizengwe???tunahitaji kujua nani wanaunda chama hicho.
 
I would prefer it termed as madai, and not tuhuma!

Neno hili linanyonga dhana ya demokrasia, na kutisha, likipanda mawazo mgando kuwa mtu kuhamia chama kingine ni dalili ya uhaini...huh!

Ni kweli, si unajua waandishi wetu wa habari? Kwao tayari zimeshakuwa tuhuma!
 
Hiki chama naona ni kama vile ku-test zari! Let's wait n c!

Hamna kitu hapa. Wanatingisha kiberiti tu. Kama wangekuwa kweli wana nia wanaogopa nini kusema wazi? Si haki yao ya kikatiba? Pengine kuna kitu wanataka ndani ya chama chao na hii ndiyo strategy wanayotumia.

Amandla......
 
CCJ inanikumbusha zile 'Bendi za Sikukuu' ambazo huanzishwa zinapokaribia sikukuu za Idd au Krismas. Ama baada ya sikukuu bendi hizo hupotea na kutokomea.
Tunapokwenda kwenye uchaguzi mkuu 2010, vyama vya msimu wa uchaguzi vitajitokeza na hata vile vilivyokuwa vimelala vitaanza kupandisha bendera zao kuonesha kuwa wapo kwa ajili ya watanzania.
Lakini swala la msingi ni kwamba hawaoni kuwa uwepo wao ndani ya miaka 4 bila ya kufanya kazi ya siasa kama vile inayofanywa na Chadema, CUF, TLP na NCCR-Mageuzi ni dalili za ubabaishaji.
Haya yangu macho, wapiga kura ndiyo watakaotoa hukumu!
 
The timing of forming a new political party a few months before the general election leaves alot to be desired. If at all the so called VIGOGO within ccm are disgruntled with what ever is happenning in their party, the best thing they should do at the moment as a short term measure is root for the PRIVATE candidate impasse to be resolved under certificate of urgency at the court of appeal!! It is in the best interests of ccm that the case stalls for eternity!! I believe if private candidates are allowed, we shall see many of the current sitting MPs left out on the wayside enabling our parliament to be more effective than it is now!!
 
nijibu au nijadili nini? nini wakati Chama Tunakisikia katika Vyombo vya habari kije tukijadili sawa Mkubwa
 
The timing of forming a new political party a few months before the general election leaves alot to be desired. If at all the so called VIGOGO within ccm are disgruntled with what ever is happenning in their party, the best thing they should do at the moment as a short term measure is root for the PRIVATE candidate impasse to be resolved under certificate of urgency at the court of appeal!! It is in the best interests of ccm that the case stalls for eternity!! I believe if private candidates are allowed, we shall see many of the current sitting MPs left out on the wayside enabling our parliament to be more effective than it is now!!

I agree with you kuwa The timing of forming a new political party a few months before the general election leaves alot to be desired. Zaidi ya hapo inaonesha kuwa wahusika wa hii CCJ huenda hawako makini na wamekosa dira nzuri na hatimaye kujikuta kumbe na wao ni walewale wanaofanya mambo ya kizimamoto.

May be what they want ni platform ya uchaguzi na wala siyo kufanya kazi ya kisiasa hasa kama opposition. I stand on chama tawala side lakini I have to pay my tributes to the opposition parties ambao wamekuwa katika kazi nzuri na ngumu ya kuwatumikia wananchi for the past four years baada ya uchaguzi wa mwisho.

Kati ya vyama hivyo tumeona jinsi ambavyo wamewafikia watanzania na wakawaelewa. Sasa kama hawa wengine nia yao ni kupunguza au kugawa kura za opposition ambao wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana nitasikitika sana japo siwezi kuwalaumu kwani wanatumia haki yao ya kikatiba hata kama hawaitumii kwa maslahi ya watanzania walio wengi.
 
As long as there are no known names named, CCJ will remain a 'Much ado about nothing/ A storm in tea cup projects. Nothing will come out of it. Let us Look for Genuine ways to overhaul CCM. Not these 'bendi za sikukuu' (Thanx!) ghost Parties!!
 
Waheshimiwa,
Pilikapilika za waandishi na michechoto ya baadhi ya viongozi wa CCM, vyama vya Upinzani na wananchi wengine kwa ujumla kuhusu CCJ inaashiria nini kama chama hicho kipya hakina jipya na hakiwatishi CCM? Vitisho kutoka kwa viongozi wa CCM kwamba watakaojiunga na CCJ watajimaliza wenyewe inadhahirisha jinsi viongozi hao wasivyotaka ushindani wa kweli. Watakaojiunga watajimalizaje wakati wameamua wao wenyewe kuunda chama kipya wakiwa na malengo yao na Katiba ya nchi inawaruhusu wafanye hivyo? Au CCM ina dhamira ya kuua demokrasia nchini?
 
Waheshimiwa,
Pilikapilika za waandishi na michechoto ya baadhi ya viongozi wa CCM, vyama vya Upinzani na wananchi wengine kwa ujumla kuhusu CCJ inaashiria nini kama chama hicho kipya hakina jipya na hakiwatishi CCM? Vitisho kutoka kwa viongozi wa CCM kwamba watakaojiunga na CCJ watajimaliza wenyewe inadhahirisha jinsi viongozi hao wasivyotaka ushindani wa kweli. Watakaojiunga watajimalizaje wakati wameamua wao wenyewe kuunda chama kipya wakiwa na malengo yao na Katiba ya nchi inawaruhusu wafanye hivyo? Au CCM ina dhamira ya kuua demokrasia nchini?

Mkuu Boramaisha

Hiyo hali unayoita mchecheto ya baadhi wa viongozi wa CCM, vyama vya upinzani, wananchi nk ni ya kawaida hasa pale tukio linapokuwa ni 'news' baada ya muda litapita na kubaki kamatukio jingine na kuendelea kupata 'news' kama kawaida.

Kimsingi kauli ambazo unazisema kuwa zinatoka kwa viongozi wa CCM si tamko rasmi la CCM to the extent ya kusema kuwa hakitaki demokrasia ikue. Katika kipindi hiki chama miaka 4 iliyopita kuna kila dalili kuwa kumekuwa na mazingira mazuri ya kupanuka na kukuwa kwa demokrasi nchini mwetu. Na hayo mazingira hayajileti, bali hutengenezwa, na yametengenezwa na CCM kwa kushirikiana na opposition katika kipindi chote hicho cha miaka 4.

Kuhusu kauli ya kujimaliza, mimi nadhani ni usia mzuri, kwa mwanasiasa makini mwenye rekodi nzuri ya utendaji basi anaweza kwenda kwenye chama ambacho tayari kinarekodi nzuri ya kiutendaji. Unaweza kuwa mwanachama mzuri tu halafu ukaenda kwenye chama ambacho haki rekodi nzuri ya kazi au hakina kabisa...sasa hapo hujajimaliza mwenyewe!!!
 
Mwalimu Nyerere hakukianzisha Chama cha CCJ. Isipokuwa hawa watu walioanzisha CCJ wanamtaja Mwalimu katika Katiba yao, wanamweka Mwalimu katika Katiba yao, kama njia ya kupata baraka ya Watanzania.

Hawajajitokeza,kwa nini tusisubiri wajitokeze kabla ya kutoa maoni kuhusu CCJ. Tusibiri. Tunachoweza kusema tu sasa,hatuoni hitilafu yoyote katika jinsi hiki Chama kipya kinavyoanzishwa.

Sisi hatujafaidika sana na uongozi wa Jakaya Kikwete. Tunadhani kwamba viongozi ni lazima wawe watu of high moral calibre.Uongozi wa juu lazima wawe people of high moral calibre. We will not complain kama hatutapata nafasi ya kushiriki katika kuipora Nchi. Lakini at least we hope that there can be peace in our day to day life. Lakini yule kiongozi wa juu,akiwa siyo Mheshimiwa, in the real sense of the word,kwamba ni mtu anayefanya mambo ya heshima, ni mtu ambaye anataka kusikia mambo ya heshima yanafanyika katika himaya yake, basi, kutakuwa hakuna kipingamizi kwa minor official kufanya makosa, kama makosa ya kukiuka haki za binadamu.

Inakuwepo encouragement kwa watu wengi kufanya maovu wakati yule kiongozi wa juu anakuwa mtu of kukewarm morality.

Maadili mema yanapuuzwa, watu wanataka kushi maisha ya kidunia. Watu hawafanyi connection wanayotakiwa kufanya, kati ya ufisadi na hali yao duni ya maisha; tamaa za kutaka utajiri wa haraka, kuwasingizia makosa watu ambao hawana hatia, kwa sababu tu za kutaka kutajirika,au kwa sababu za kidunia, kuwatia hatiani watu ambao hawana hatia, matatizo yanayotokea kwa ajili ya ufuska na ukwere, mambo yote haya yanaonekana kuwa ni tofauti na dhiki zinazotufika katika Nchi. Kuzitakasa nafsi za watu ndio ufunguo wa maendeleo,siyo kitu optional. Haupaswi kuwepo huhur wa mawazo ambapo kila mtu yupo huru kufiria fiithy thoughts.

Kama Chama kipya kitaanzishwa na ahadi ya kuisafisha Nchi kwa nini wasiungwe mkono,kwa nini waitwe CCM B? Kwa hiyo tusubiri wiki chache tuone ni kina nani wanataka kuanzisha Chama kipya, na wana ajenda gani, na vyama vya Upinzani vilivyopo sasa hivi pia vina ajenda gani. Kwa sababu the time is nigh, Uchaguzi Mkuu ni lazima uanze sasa.

Ganesh,
Thumbs up man! You have said it all. Cha msingi ni kuona Chama hicho kipya kitakuwa na agenda gani za kuikwamua nchi yetu na wananchi kwa ujumla kutoka kwenye tope la ufisadi na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla. Chama hicho kitafanya nini kuweza kuleta matumaini ndani ya nyoyo za wananchi maskini wa nchi hii wanaoteseka kutokana na kuparaganyika kwa uongozi wa CCM. Tunazungumzia asilimia 80 ya Watanzania wasio na uhakika wa maisha yao na ya watoto wao.
 
Back
Top Bottom