Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 303
Can u try talking anything new sometimes?
Just one new thing...a single!..huh!
PJ huyo Kibunango ameshakunywa maji ya bendera ya kijani hata umwambie nini atakufa na skafu ya CCM shingoni.
Can u try talking anything new sometimes?
Just one new thing...a single!..huh!
hiki chama kimeshaanza kuonesha kina Walakini, hivi kweli kama kuna wapiganaji wa kweli kwenye hichi chama inakuwaje mpaka sasa wanashindwa kujiweka wazi, kwa nini wanakuwa mguu ndani nje?, nadhani kila mtu amwamini mwenzie,
viongozi wenye nia mbilimbili hawatufai Tanzania,
mwambie broda...na mambo mazuri huwa hayataki haraka kihivyo!usiwe na haraka kumwona mwali
Walishajifunza kwa kilichompata Mrema NCCR-Mageuzi.Mimi naona ni bora wakaingia ndani ya vyama vipivyopo katika CHADEMA na vyama vingine kama CUF, TLP na vingine kama kweli wana nia ya dhati kwetu. Ila ni danganya toto to
Walishajifunza kwa kilichompata Mrema NCCR-Mageuzi.
Hivyo vilivyopo mi naona kama vyote ni scandalous!
CHADEMA - SKENDO YA U'KANDA
NCCR MAGEUZI- KIMESHADHIBITIWA FULLY, NA WANATANGAZA SERA ZA CCM SASA
TLP - ANOTHER CCM!
CUF- Full udini!
Kuna haja ya uanzishwaji wa chama kipya kabisa!
Tuangalie Kenya jinsi walivyofanikisha jamani!
Fastafasta walianzisha na kuua na kuunganishaunganisha mavyama hadi wakafikia muafaka, na kuchukua nchi!
Sasa hivi tusiangalie chama, tuangalie watu..huh!
Hivyo vilivyopo mi naona kama vyote ni scandalous!
CHADEMA - SKENDO YA U'KANDA
NCCR MAGEUZI- KIMESHADHIBITIWA FULLY, NA WANATANGAZA SERA ZA CCM SASA
TLP - ANOTHER CCM!
CUF- Full udini!
Kuna haja ya uanzishwaji wa chama kipya kabisa!
Tuangalie Kenya jinsi walivyofanikisha jamani!
Fastafasta walianzisha na kuua na kuunganishaunganisha mavyama hadi wakafikia muafaka, na kuchukua nchi!
Sasa hivi tusiangalie chama, tuangalie watu..huh!
Ndugu mlalahoi your analysis ni swaafi. Ingekuwa ni assignment kwa ajili ya dissertation basi ningekupa A+. Nakubaliana na wewe mia kwa mia. Hiyo CCJ ni kama ulivyosema ni CCM B. Unajua nchini Tanzania wengi wetu tumekuwa sehemu ya kizazi na kwa njia hiyo we are bonded to the system of TANU/CCM. Oxygen tunayoivuta ni ya CCM. Mimi naipenda kuitambua kuwa ni Yanga/Simba syndrome. Kama vile club zetu za mipira zinavyoshahabiana na Yanga au Simba, vivyo hivyo siasa za Tanzania vyama vyote vya upinzani ni part and parcel of CCM. Wanaenda upinzani kwa sababu wana malalamiko au manun'guniko. Hata hoja wanazotoa za kumlaumu JK za kitoto kweli. Just imagine kwenye ile kongamano ya MNF pale Karimjee zile hoja za kitoto. Mzee mstaafu analalamika kuwa hasikilizwi. Hii maana yake wanataka attention. Usipowasikiliza basi jawabu ni kulia na kupiga kelele. Haya tuone mambo yatakavyokwenda huko mbeleni.
Kwani Nyerere aliposema upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM alijua anasema nini. Mmesahau kuwa Edwin Mtei alikuwa CCM na akaunda CHADEMA. Na ndiyo maana Nyerere aliipenda CHADEMA.
Kuingoa CCM labda baada ya vijiji vya Tanzania kuwa urbanised. Otherwise peasants wengi ni proCCM kutokana na conservatism yao. Upinzani uko mijini kwa sababu watu wa mjini ni enlightened. So I agree with you CCJ is not a panacea for removing CCM
Yawezekana siko sahihi,lakini habari za ujio wa chama kipya cha siasa,Chama Cha Jamii (CCJ),zimenipa hofu hasa kwa namna zilivyopokelewa mithili ya habari njema.
Kwanza,kuna ulinganifu unaofanywa kuhusu kuzaliwa kwa CCJ na utabiri wa Nyerere kuwa upinzani wa kweli utatoka CCM.Pamoja na heshima kubwa niliyonayo kwa Baba wa Taifa,lakini mie na wewe tunafahamu kuwa Mwalimu alikuwa binadamu na si malaika,hivyo utabiri wake haumaanishi usahihi wa asilimia 100.Lakini la muhimu zaidi ni mchango wa Mwalimu katika kutufikisha hapa tulipo sasa.Sote tunakumbuka kuwa Nyerere alimpigia debe la nguvu Ben Mkapa kuwa rais wetu.Sihitaji kuingia kwa undani kuhusu namna Mkapa alivyolipeleka mrama taifa letu,huku akijitengenezea utajiri mkubwa kwa mgongo wa kubeba wawekezaji.
Je Mkapa alivaa ngozi ya kondoo kiasi kwamba Nyerere hakujua kuwa huyo ni mbwa mwitu?Kufupisha mjadala,kwa mantiki hiyo,hata kama kuzaliwa kwa CCJ ni kutimia kwa utabiri wa Mwalimu,haimaanishi kwamba tutarajie mapya sana kutoka kwa chama hicho kwa vile historia inatuonyesha kuwa si kila aliloamini Mwalimu lilizaa mema kwa taifa.
Kinachonipa hofu zaidi ni ukweli kwamba vigogo hao wako mguu mmoja ndani mguu mmoja nje katika mahaba yao na CCM.Wanaogopa hata kujiweka wazi hadharani.
Tatu,jambo moja ambalo wengi wetu hatulitilii maanani ni nafasi ya vyombo vya dola katika kuhujumu demokrasia.Na si kosa la makusudi kwa vile shughuli hiyo hufanyika kwa siri kama ambavyo nature ya vyombo hivyo ilivyo.Tayari kuna tetesi kuwa baadhi ya vigogo wanaosemekana kuwa waasisi wa CCJ wameshaanza kuhojiwa na vyombo vya dola.Changanya hilo na habari kwamba JK anadai hayuko tayari kuiona CCM ikimfia mikononi mwake,basi kuna uwezekano mkubwa wa kuwa na CCJ iliyopandikizwa vibaraka watakaopelekea yaleyale ya NCCR Mageuzi.Si ajabu pia CCJ ikawa kiini macho na usanii wa taasisi flani ku-deflect attention yetu kwenye vita dhidi ya ufisadi na kupata tumaini hewa kuwa "aaah sasa CCM lazima iwe tumbo joto kwa vile ikicheza tu inaondolewa na CCJ".Huu unaweza kuwa mchazo wa kuigiza,trust me!
Nne,hata kama CCJ is a real and genuine thing,si habari njema sana kwa akina sie tunaodhani kuwa kuna vyama pinzani,kama Chadema ambavyo angalau vimetuonyesha dhamira na uwezo wa kuchuana na CCM.
Mwisho,CCJ inakuja kugawa kura za Upinzani.Na hiyo si habari njema kwa wanaotaka kuona CCM inaondoka madarakani.As I said before,I might be wrong lakini....