Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Nafikiri ungekuwa unafikiri kabla ya kuandika jambo, hivi kweli CCM ni makini kwa kuwatumikia wananchi kwa yepi au makini kwa kushinda uchaguzi, tofautisha kushinda uchaguzi na utekelezaji wa ilani yake.

Umeandika kwa ushabiki zaidi ya mantiki yenyewe labda ungesema CCM huwa makini linapokuja suala la chaguzi inaweza ikapata hizo 70% lakini si kwa kuwatumikia wananchi.

Dah! Kaazi kweli kweli hivi mtu Makini atayesoma post yangu anaweza kufikiria kwamba mimi ni Mshabiki wa CCM? May be for those who think Locally, soma tena post yangu kwa Umakini rudia tena tena tumia akili yako may be utaelewa nini nazungumzia
 
Ndege ya Uchumi
Sijakutusi ila ni mtazamo wangu kwamba uchambuzi ulioufanya sio sahihi.Nimekusoma kwa makini na nimekuelwa vizuri sana.Rejea tena uchambuzi wako halafu tafakari kwa kina utagundua kwamba umekosea.Umekipa CCJ 10% halafu ukavipa CUF na CHADEMA 8% kitu amabcho sio sahihi.Umekaa kishabiki zaidi.

Mkuu Gender huwa nakuaminia sana katika kuelewa Mambo, Mkuu wangu ukisoma kwa makini uchambuzi wangu namaanisha kwamba CCJ laweza kuwa changa la Macho ili kuuwa Upinzani wa Kweli ambao umeanza kuota mizizi hapa Tanzania

Yale ni maono yangu tu mkuu, kwani akina Akwilombe, Tambwe walirudi CCM hawakuimba Umakini wa CCM?

Sasa kwa uelewa wako umekimbilia kuniweka katika Kundi la mashabiki wa CCJ, halafu ukisoma kwa Umakini utagundua wewe ndiye Mshabiki

Mimi najaribu kuangalia ishu in three dimension wewe unaangalia in one dimension bana, hebu rudi katika post yangu, usisome maandishi bali soma katikati yake
 
This is a very stupid analysis ambayo sijawahi kuiona.Kweli wewe unaongozwa na hisia zaidi kuliko kufanya uchambuzi wa kina.CCJ hata kama kitakuwa na nguvu vipi hakitaweza kupata Wabunge kwahizo asilimia ulizoziweka,kwani sio rahisi kama unavyodhani....kutangaza chama cha siasa sio kazi rahisi....inahitaji angalau miaka 3 ili kujitambulisha vya kutosha kwa watanzania...kumbuka hapa ni Tanzania na sio nchi Marekani wala Uingereza...Hata hao wabunge watakaokianzisha wengi wao watapoteza ubunge wao wakigombea kupitia CCJ....

GS,

Kushinda chaguzi kunahitaji nguvu ya kisiasa, hautaweza kupata kura zaidi ya nguvu za kisiasa uliyonayo kwa wapiga kura husika, nguvu hizo zinaweza kuwa za chama(ambazo zinahitaji muda kuzijenga) au nguvu za mtu(watu) waliopo/watakaokuwepo kwenye chama husika.

Kwa hili la pili, everything is possible, Kumbuka mwaka 1995 NCCR from nothing waliweza kupata wabunge 19 na 28% za urais,hii ilitokana na mtu mmoja tu maarufu Mrema,fikiria kungekuwa na kina mrema 15 wakatoka pamoja kujiunga NCCR?

Never say never in politics.
 
GS,

Kushinda chaguzi kunahitaji nguvu ya kisiasa, hautaweza kupata kura zaidi ya nguvu za kisiasa uliyonayo kwa wapiga kura husika, nguvu hizo zinaweza kuwa za chama(ambazo zinahitaji muda kuzijenga) au nguvu za mtu(watu) waliopo/watakaokuwepo kwenye chama husika.

Kwa hili la pili, everything is possible, Kumbuka mwaka 1995,NCCR from nothing waliweza kupata wabunge 19 na 28% za urais,hii ilitokana na mtu mmoja tu maarufu Mrema,fikiria kungekuwa na kina mrema 15 wakatoka pamoja kujiunga NCCR?

Never say never in politics.

To Add on that

Nguvu zaweza kutoka huko huko CCM ili kiweze ( CCJ) kupambana na vyama vingine na baada ya Uchaguzi CCJ kijibomoe na kurudi kilikotoka. This can be conspiaracy, but it works
 
Hebu tusubiri tuwasikie wana lipi jipya. Lakini inawezekana pia ni njia mojawapo ya kupata maruzuku kwenye uchaguzi ujao. Lets watch.
 
To Add on that

Nguvu zaweza kutoka huko huko CCM ili kiweze ( CCJ) kupambana na vyama vingine na baada ya Uchaguzi CCJ kijibomoe na kurudi kilikotoka. This can be conspiaracy, but it works
Kwa nguvu ya CCM za sasa ukulinganisha na udhaifu wa upinzani tulionao hakuna sababu ya CCM kufanya hivyo, hilo kwa sasa halipo.
 
To Add on that

Nguvu zaweza kutoka huko huko CCM ili kiweze ( CCJ) kupambana na vyama vingine na baada ya Uchaguzi CCJ kijibomoe na kurudi kilikotoka. This can be conspiaracy, but it works


Sidhani kama CCM imefikia hatua ya kuwa na wasi wasi kiasi hicho vyama vyenyewe vya upinzani viko wapi hadi iji-risk namna hiyo.
 
Sasa watu hawa ni wale mafisadi wanaona hawapati walichokitarajia kutoka CCM au ni wale wakereketwa wanaona nchi inaelekea kuwekwa rehani? Sijaelewa hapo hao vizito ni wa aina gani.
 
Karibu CHAMA CHA JAMII(CCJ).

MI HUWA SI MWANASIASA, LAKINI KWA HABARI HII YA CCJ, NIMEAMUA KUWA legend wa siasa, na ninaomba Mungu kila kukicha, akisimamie chama hiki, kianze kwa kusimama na si kutambaa!

Kimekuja wakati muafaka sana, na haya ni matumaini ya wazi kwa Watanzania...Wenzetu Kenya walipita huku zamani, na hawaogopi mabadiliko!

Karibu CCJ, imani yangu ni kwamba utaleta mabadiliko kwa nchi hii!
Kuna watu wana\sema kwamba chama hiki kitakuwa hakina tofauti na CCM, maana kitaundwa na watu waliotoka CCM!..

Mimi nasema kwamba hao wanaotoka CCM ndo wazuri sana, maana wanajuana wao kwa wao, na uzuri ni kwamba wanaondoka huko kwa hasira na si kwa mema, kwahiyo tutarajie mabadiliko makubwa sana.

Ogopa sana wezi wawili wanapokuwa mahasimu, zao litakalotoka hapo ni Utakatifu, aidha kwa mmojawapo kuamua kujisalimisha na kuwa sobber!

CCM inahitaji sana uwepo wa CCJ, maana wataelewa wazi kuwa saa ya ukombozi imefika, na hatimaye watajaribu kuwakumbuka wapiga kura wao kwa kujaribu kuwapa maisha bora!

Karibu SAANA CCJ, TUNAPENDA KUJUA HATUA KWA HATUA ZA UZINDUZI WENU, NA KWAMBA KADI ZA UANACHAMA ZITAPATIKANA WAPI..!NITAKUWA KATI YA WANACHAMA WA MWANZO KABISA KWA ENEO NINALOISHI...NIMECHOKA NA KUBURUZWA!
 
Ndugu yangu,i kina nani waanzilishi wa messiah huyu-CCJ ?
Ni watu kibao, vigogo wa CCM, na wengineo prominent.
Tuwe wapole, tutapata LIST ya majina yao huenda ndani ya wiki hii ijayo!
Lakini kwa ujumla, ni jambo la ukombozi kwa mtu yeyote rational!
 
Ni watu kibao, vigogo wa CCM, na wengineo prominent.
Tuwe wapole, tutapata LIST ya majina yao huenda ndani ya wiki hii ijayo!
Lakini kwa ujumla, ni jambo la ukombozi kwa mtu yeyote rational!

Mtu yoyote rational hawezi kusupport chama cha siasa bila kujua ni wakina nani wapo nyuma yake. Ngoja tupate kwanza hiyo list ndiyo tusupport siyo kwenda kichwa kichwa. Vigogo wa CCM waweza kuwa wa aina nyingi. Wanaweza kuwa wale mafisadi au wanao tetea maslahi ya wananchi na taifa.
 
Mtu yoyote rational hawezi kusupport chama cha siasa bila kujua ni wakina nani wapo nyuma yake. Ngoja tupate kwanza hiyo list ndiyo tusupport siyo kwenda kichwa kichwa. Vigogo wa CCM waweza kuwa wa aina nyingi. Wanaweza kuwa wale mafisadi au wanao tetea maslahi ya wananchi na taifa.
MwanaFA we are sailing in the same boat!

Nilichofurahia unaonyesha hamu kubwa ya kutafiti chama hiki ili kama vp..basi iwe vp..! ..i know it!

Ninachokwambia, in any way, pamoja na wao waasisi kuwa anonymous, kwa kusoma katiba yao, wanaonyesha kurudi kwenye misingi ya awali ya taifa hili, kuleeee- enzi za mwalimu!...Thats where i saw them brilliant!

Kama ulivyosema, tuwe patient, japokuwa mi ninaona nchi ya maziwa na asali kupitia chama hiki!
 
Ni watu kibao, vigogo wa CCM, na wengineo prominent.
Tuwe wapole, tutapata LIST ya majina yao huenda ndani ya wiki hii ijayo!
Lakini kwa ujumla, ni jambo la ukombozi kwa mtu yeyote rational!

Ni vizuri sasa tukawa sote tunapigania rasimali za nchi zitumike kuboresha maisha ya wananchi wote kuanzia kwanza vijijini kuja mijini. Sie tunangoja kusikia kitakachofuata katika kuingia katika medani ya siasa ili kuleta uwajibikaji na utoaji huduma nzuri. Uongozi wa CCM umepoteza dira na mwelekeo kwa kupachika viongozi ambao hawajali wananchi wao na wala hawana mapenzi nao. Wadau tupeane tu "updates".
 
hiki chama kimeshaanza kuonesha kina Walakini, hivi kweli kama kuna wapiganaji wa kweli kwenye hichi chama inakuwaje mpaka sasa wanashindwa kujiweka wazi, kwa nini wanakuwa mguu ndani nje?, nadhani kila mtu amwamini mwenzie,
viongozi wenye nia mbilimbili hawatufai Tanzania,
 
"Kwa Kizungu hali hii hutwa 'dilemma'"; ni utatizi wa uamuzi, kama penye njia panda:

Kifo cha maji kushoto,
Kulia kifo cha moto:
Kukubali, kukataa,
Kila moja ni balaa!
Kote uko hatarini,
Hujui ufanye nini. "

- Julius K. Nyerere, Uongozi wetu na Hatma ya Tanzania, uk. 54
 
"Kwa Kizungu hali hii hutwa 'dilemma'"; ni utatizi wa uamuzi, kama penye njia panda:

Kifo cha maji kushoto,
Kulia kifo cha moto:
Kukubali, kukataa,
Kila moja ni balaa!
Kote uko hatarini,
Hujui ufanye nini. "

- Julius K. Nyerere, Uongozi wetu na Hatma ya Tanzania, uk. 54

Got you broda!
Mbona ni rahisi kuamua?
Kifo cha maji kushoto waweza ukaogelea na kupona.
Mi naona at least kuna nafuu huku!...Thats CCJ!
 
Back
Top Bottom