Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

I agree with you kuwa The timing of forming a new political party a few months before the general election leaves alot to be desired. Zaidi ya hapo inaonesha kuwa wahusika wa hii CCJ huenda hawako makini na wamekosa dira nzuri na hatimaye kujikuta kumbe na wao ni walewale wanaofanya mambo ya kizimamoto.

May be what they want ni platform ya uchaguzi na wala siyo kufanya kazi ya kisiasa hasa kama opposition. I stand on chama tawala side lakini I have to pay my tributes to the opposition parties ambao wamekuwa katika kazi nzuri na ngumu ya kuwatumikia wananchi for the past four years baada ya uchaguzi wa mwisho.

Kati ya vyama hivyo tumeona jinsi ambavyo wamewafikia watanzania na wakawaelewa. Sasa kama hawa wengine nia yao ni kupunguza au kugawa kura za opposition ambao wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana nitasikitika sana japo siwezi kuwalaumu kwani wanatumia haki yao ya kikatiba hata kama hawaitumii kwa maslahi ya watanzania walio wengi.
Mawazo yako ni mazuri. Ila cha kukumbuka ni kwamba katika siasa hakuna kanuni kama ilivyo katika masomo mbalimbali ya kisayansi kama hesabu,physikia na chemia.

Hivyo CCJ sio chama cha kubeza katika mapema hii chochote chaweza kutokea. Upinzani dhaifu unaoonyeshwa na vyama vingi vya siasa vilivyopo sasa kisiwe kigezo cha kubeza kila jaribio hivyo tutegemee chochote.
 
Mawazo yako ni mazuri. Ila cha kukumbuka ni kwamba katika siasa hakuna kanuni kama ilivyo katika masomo mbalimbali ya kisayansi kama hesabu,physikia na chemia.

Hivyo CCJ sio chama cha kubeza katika mapema hii chochote chaweza kutokea. Upinzani dhaifu unaoonyeshwa na vyama vingi vya siasa vilivyopo sasa kisiwe kigezo cha kubeza kila jaribio hivyo tutegemee chochote.

Mkuu Ahsante sana kwa maoni yako. Lakini nadhani umeshau kuwa siasa ni sayansi na uchambuzi wa masuala ya kisiasa pia ni hutoa majibu na mwelekeo halisia ya mambo yatakavyotokea.

Nadahani kama umeshasikia kuwa au kuona majopo mbalimbali huwa yanakaa na kuzungumzia hali za kisiasa ambazo matokeo yake huwa ni over 80%.

Kwahiyo kadri mawazo yanavyotolewa kutoka kwa watu wa kada mbalimbali yakikusanywa huwezesha kutoa taswira nzima ya mwelekeo wa jambo linalozungumzwa. Lakini hata hivyo kikubwa zaidi ni hoja ambazo unadhani zinabeza hicho chama cha jamii. Kwa mfano unaweza kuangalia je ni integrity ipi anayoweza kuwa na mwanasiasa makini aliyekuwepo katika chama chake chenye nguvu akaondoka kwenda CCJ katika kipindi?

Could understand kama mwanasiasa anayeelewa masuala ya siasa za Tanzania angeweza kwenda CCM au Chadema au CUF but not CCJ.

Kama yuko wa kwenda huko basi ni kweli itakuwa ni sehemu ya maajabu, lakini haitarajiwa kwa mujibu wa wachunguzi wa mambo.
 
Mkuu Ahsante sana kwa maoni yako. Lakini nadhani umeshau kuwa siasa ni sayansi na uchambuzi wa masuala ya kisiasa pia ni hutoa majibu na mwelekeo halisia ya mambo yatakavyotokea.

Nadahani kama umeshasikia kuwa au kuona majopo mbalimbali huwa yanakaa na kuzungumzia hali za kisiasa ambazo matokeo yake huwa ni over 80%.

Kwahiyo kadri mawazo yanavyotolewa kutoka kwa watu wa kada mbalimbali yakikusanywa huwezesha kutoa taswira nzima ya mwelekeo wa jambo linalozungumzwa. Lakini hata hivyo kikubwa zaidi ni hoja ambazo unadhani zinabeza hicho chama cha jamii. Kwa mfano unaweza kuangalia je ni integrity ipi anayoweza kuwa na mwanasiasa makini aliyekuwepo katika chama chake chenye nguvu akaondoka kwenda CCJ katika kipindi?

Could understand kama mwanasiasa anayeelewa masuala ya siasa za Tanzania angeweza kwenda CCM au Chadema au CUF but not CCJ.

Kama yuko wa kwenda huko basi ni kweli itakuwa ni sehemu ya maajabu, lakini haitarajiwa kwa mujibu wa wachunguzi wa mambo.
Sawa sawa mkuu, ila uana mapinduzi wa kweli sometimes ni risk taking are we together on this?
 
Ni wale wale tu,hakuna mpiganaji katika ufisadi................Wa tanzania tutaendelea kuliwa mpaka siku ya mwisho!!!
Ndugu yangu hakuna dhambi kubwa kama kukata tamaa. cha msingi ni kuwa ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunachagua individual ambao tuna imani na usafi, uadilifu na uthubutu wa fikra mpya. let us not let these vyama's bog us.
INAWEZEKANA KUPATA VIONGOZI BORA TZ. kama kuna mapungufu ni kuwa sisi hatufanyi kazi ya kuwaelimisha wananchi sifa za viongozi bora ni zipi ili wao waweze kufanya maamuzi sahihi.
 
Kuna mawazo na propaganda kuwa eti CCJ ni chama ambacho kimesheheni Vigogo wa CCM.
Huu si ukweli.
Ukweli ni kwamba CCM iko pale pale na vigogo wake bado wako ngangari ndani ya CCM.

CCJ ni chama kilichoanzishwa ili kuwachanganya wapinzani wadhani kuwa CCM imekuwa dhaifu.

Wapinzani wakawaza kuwa CCJ ni mgawanyiko wa CCM, basi watashindwa kirahisi na CCM kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Wapinzani unganisheni nguvu zenu badala ya kupumbazwa na CCJ kisha mkalala usingizi.

Natoa hoja.
 
Ni mawazo yako komredi.... Au ndio ulivyotumwa na kikao cha dharura jumapili ya jana? And what is the objective, mnataka proof ili muwasulubu....si walipoulizwa walikana...kwa hiyo mnataka tuwape scanned originals hapa?

Wapiganaji kwa uchokozi!!!!!??????duh!!!!!!!
 
CCJ ni chama cha wale watakaofulia CCM, watakaoshindwa kura za maoni ambao hawakubaliani na vyama vya upinzani vilivyoko sasa
 
Ok.Kama haijatoka ndani ya CCM kimetoka wapi basi...Mbona wajikanyaga?umesema CCJ kimeanzishwa ila kuwachanganya wapinzani kwahiyo maana yake kimeanzishwa na CCM.......na je do you thimk kwamba wapinzani wakijua kuwa CCJ ni tokeo la mpasuko ndani ya CCM kwahiyo wataogopa?
 
CCJ ni chama kilichoanzishwa ili kuwachanganya wapinzani wadhani kuwa CCM imekuwa dhaifu.

Kwa hiyo kwa kifupi unasema CCJ sio chama chenye lengo la kushindana na CCM? Kama ndivyo hivyo mbona CCM wameanza 'kuweweseka'? Au ni usanii tu?
 
Ni mawazo yako komredi.... Au ndio ulivyotumwa na kikao cha dharura jumapili ya jana? And what is the objective, mnataka proof ili muwasulubu....si walipoulizwa walikana...kwa hiyo mnataka tuwape scanned originals hapa?

Wapiganaji kwa uchokozi!!!!!??????duh!!!!!!!

Mkuu AKASHUBE,
Mimi siko huko kwa kikao cha dharura hata kidogo.
Ni masuala ya kuwa wakweli tu.
 
Kwa hiyo kwa kifupi unasema CCJ sio chama chenye lengo la kushindana na CCM? Kama ndivyo hivyo mbona CCM wameanza 'kuweweseka'? Au ni usanii tu?
Kuweweseka hakupo mkuu.
Huo ni usanii ili kuwapumbaza wapinzani.
 
CCJ ni lazima iwe na wanachama ambao tayari ni wanasiasa. Sasa kwa upande wa upinzani hakuna upepo mkubwa uliovuma kuashiria kuwa wametoka watu wakaunda CCJ. Kura inabaki kuwa hawa wengi wao watakuwa wametoka CCM.!!!
 
Ok.Kama haijatoka ndani ya CCM kimetoka wapi basi...Mbona wajikanyaga?umesema CCJ kimeanzishwa ila kuwachanganya wapinzani kwahiyo maana yake kimeanzishwa na CCM.......na je do you thimk kwamba wapinzani wakijua kuwa CCJ ni tokeo la mpasuko ndani ya CCM kwahiyo wataogopa?
Wapinzani wakidhani kuwa CCJ ni matokeo ya mpsuko ndani ya CCM watadhani kuwa ni rahisi kuishinda CCM hivyo wata dilute nguvu zao wenyewe(wapinzani)
 
CCJ ni chama cha wale watakaofulia CCM, watakaoshindwa kura za maoni ambao hawakubaliani na vyama vya upinzani vilivyoko sasa
Mkuu Mtu B,
Watakao fulia CCM wamejijua na kujianzishia chama kabla?
Hii inachekesha japo sipati Logic.
 
Hivi tukijaribu kuwa wakweli kuna chama cha siasa hapa nchini ambacho hakijatokana na ccm? Angalia cuf ni nani hajawahi kuwa ndani ya ccm? Chadema, ni nani ambaye hajaahi kuwa ndani ya ccm? Tlp, nccr mageuzi. Nk na kwa nyakati tofauti waote hawa walipotoka ccm waliacha makovu. Ni nani asiye jua kuwa kaka chiligati ni mtu wa propaganda? Kuwa eti hakuna kigogo mwenye mpango wa kutoka ccm? Si alitishia tena kwa kufoka sana kumpeleka slaa mahakamani hivi karibunu kuhusiana na ccm kukwepa ushuru wa magari yake? Imeeishia wapi? Ukweli hofu lazima ipo hata wajifanye majasiri kiasi gani kwani malumbano ya hivi karibuni yanatishia uhai ndani ya chama. Mimi naamini huu ni mwanzo wa ccm kumeguka tena.
 
CCJ ni chama kilichoanzishwa ili kuwachanganya wapinzani wadhani kuwa CCM imekuwa dhaifu.
"CCJ ni chama kilichoanzishwa ili kuwachanganya wapinzani wadhani kuwa CCM imekuwa dhaifu"

yale yaleeeeeeeeeeeeeeeee...
kwa mwendo huu bora nikae pembeni...
fisadi ni fisadi tu hata akiingia kanisani au msikitini bado anabaki kuwa fisadi tu!
 
Kuweweseka hakupo mkuu.
Huo ni usanii ili kuwapumbaza wapinzani.

Sioni hao wapinzani wa kuwapumbaza na chama kipya! Itakuwa sawa na kuatafuta AK47 kwa ajili ya kuua panya!

Kina Cheyo tumeshawasikia wanaimaba 'nyimbo' ambazo CCM inataka waimbe. CUF ndio hao wanataka CCM Zanzibar iendelee kutawala! Chadema ndo hiyo nayo inachechemea!

Bado siamini kama CCJ ni strategy ya CCM. Tuvute subira tu ukweli utakuwa bayana muda si mrefu!
 
Back
Top Bottom